Pole sana kijana, hii ni mara ya pili nauona huu ujumbe wako, em jaribu kuweka screenshot hapa labda utaeleweka zaid.
? Cheti ulikiscan na kuweka kwenye PDF..?! Uliupdate kabla ya dirisha kufungwa mana sidhan kama sasa hiv system inapokea mabadiliko yoyote.
Ni vema kwenda kuwaona wahusika
Kwenye account yangu hakukua na means ya Ku attach PDF certificate/any document ila nilikua natakiwa nijaze details zifuatazo;-
1. Jina la chuo nilichosoma.
2. Mwaka niliomaliza.
3. Kozi niliyosoma.
4. Admission number (examination no.)
Baada ya hapo inanipeleka moja kwa moja kuchagua kozi.
Baadae nikiangalia kwenye profile naambiwa nimeshakamilisha mchakato wa kuomba chuo na sasa nisubiri zoezi la uchaguzi (selection).
Lakini nikiangalia pale kwenye NTA LEVEL 6 Qualification bado kuna bar nyekundu yenye maandishi mekundu inayonitaka ni UPDATE, nikirudia hizo hatua nne hapo juu bado naambiwa UPDATE vilevile.
Imekua kama mchezo wa HANGAISHA BWEGE na mimi ndiye BWEGE MWENYEWE.
Nimejaribu kuwasiliana na NACTE kwa namba zote walizoziweka pale hawapatikani, nimewaandikia barua pepe hawajajibu.
Sasa nilichoamua ni kuagiza glasi ya juisi ya majani ya mipapai na kuketi kwenye kiti cha miguu mitatu chini ya kivuli cha mti wa malimao na kupumzika huku niki "WAIT FOR SELECTION"
Nisiyejua niendako njia yoyote itanifikisha.
NB:- Sijaambatanisha "screenshot" kwa sababu saizi system haifunguki hivyo siwezi kufika kwenye profile yangu.