Kwa Tanzania bunge la chama kimoja ni bora kuliko la vyama vingi

tikatika

JF-Expert Member
May 6, 2011
2,330
4,115
Kwa wafuatiliaji wa bunge la sasa watakubali kwamba bunge la zamani chini ya chama kimoja lilikua bora kuliko bunge la sasa.

Bunge la zamank wabunge wote walikua bize kutetea maslahi ya nchi na majimbo yao katika kutetea maslahi ya nchi walikua wanaungana kuisimamia Serikali na katika kutetea majimbo yao walikua bize kweli kweli kuwakilisha shida za majimboni kwao ili kutimiza ile dhana ya mbunge kuwa mwakilishi wa wananchi.

Lakini katika bunge la sasa imekua tofauti yaani wabunge wa chama tawala wamekua bize kuitetea Serikali kuliko nchi yao.

Hata ukitokea ufisadi ndani Serikali haikosi wabunge watetezi, rejea Esrow.

Hii imeingia mpaka kwenye bajeti hawana umoja hata pale mambo ya msingi yanapo achwa na kushughulikia mambo yasiyo ya kipaumbele.

Wamekua bize kutetea chama chao kuliko majimbo yao. Hii inatokana na kuhisi wakiponda utendaji wa Serikali watakosa ubunge na kwa siasa za sasa wanahisi watachujwa wasigombee kupitia chama cha CCM na ni ukweli CCM inafanya hivyo.

Tena kwa hii CCM ya huyu bwana mkubwa itakua maradufu kuwafyeka wapingaji wa utendaji wa Serikali maana wao hupenda zaidi kusifiwa tu.

Wabunge pekee ambao wamekua na jicho la tatu kuisimamia serikali ni wapinzani lakini sauti yao haifiki popote wanamezwa na wingi wa wabunge wa CCM ambao walipaswa kuisimamia Serikali ila sasa wameamua kuitetea Serikali bungeni.

Ndipo nasema bunge la sasa halifai kuliko lile la chama kimoja. Hii haimaanishi sipendi vyama vingi bali naisikitikia nchi yangu kuja kupata maendeleo itachukua muda mrefu sana mpaka wabunge waje waache kuyatumikia matumbo yao sio leo.

Jiulize kama mbunge ameshindwa kuwa mzalendo kwa nchi yake ambae ana uelewa mpana kutokana na kutembea kwake na kukutana na watu mbalimbali hivyo kuwa na uelewa mpana juu ya mambo ya msingi kwa nchi yake yuko hivi walivyo wabunge wetu je kwa mwananchi wa kawaida. Tunategemea mwananchi awe mzalendo huku wabunge wetu wako radhi nchi ife ila CCM ibaki?

Ukiona bunge linakubali kutoa keshi billion 500 zinunue ndege ila kwenye kilimo zinaenda billion 3 au billion 18 kwa nchi nzima tena kwa kutoa kidodo kidogo kwa nchi nzima utajua kuna mahala hatuko sawa.

Naupenda upinzani ila watawala wamefanikiwa kuuzika. Tuna safari kuusimamisha upinzani wa mawazo huru, zaidi ya upinzani wa vyama.

Maana kwa sasa walio na mawazo huru hata ndani ya vyama huonekana wanatumiwa na wapinzani wao hata kama wanachosimamia ni kwa masrahi ya nchi.

Mfano huyu mbunge Bashe na CCM wamekua na vitisho kwa wenye mawazo huru kutowarudisha kwenye kinyang’anyiro kwa awamu nyingine. Hivyo basi kwa wale wafuata maslahi huufwata na kubaki kusifia tuu.

Bunge la sasa ni la hovyo kuliko la chama kimoja.
 
2020 tujitahidini kuwaleta CCM wote bungeni,I mean this is a wake up call kwa LEMA na Sugu
 
..wabunge wa ccm wakati wa mfumo wa chama kimoja walikuwa makini, mahiri, na wazalendo, kuliko wabunge wa ccm wakati huu wa vyama vingi.
 
Linganisha mabunge factors nyingine zote zikiwa constant mfano, weledi wa speaker, dola kutojihusisha na wabunge nk
 
Sio tu liwe chama kimoja bora livunjwe kama serikali haisikilizi bunge na Bunge la sisiemu linaitetea serikali.
 
kwa wafuatiliaji wa bunge la sasa watakubali kwamba bunge la zamani chini ya chama kimoja lilikua bora kuliko bunge la sasa. bunge la zaman wabunge wote walikua bize kutetea maslahi ya nchi na majimbo yao. katika kutetea maslahi ya nchi walikua wanaungana kuisimamia serikali. na katika kutetea majimbo yao walikua bize kweli kweli kuwakilisha shida za majimboni kwao ili kutimiza ile dhana ya mbunge kuwa mwakilishi wa wananchi.

lakin katika bunge la sasa imekua tofauti. yaan wabunge wa chama tawala wamekua bize kuitetea serikali kuliko nchi yao. hata ukitokea ufisadi ndani serikali haikosi wabunge watetezi, rejea esrow!! hii imeingia mpaka kwenye bajeti hawana umoja hata pale mambo ya msingi yanapo achwa na kushughulikia mambo yasiyo ya kipaumbele. wamekua bize kutetea chama chao kuliko majimbo yao. hii inatokana na kuhisi wakiponda utendaji wa serikali watakosa ubunge. na kwa siasa za sasa wanahisi watachujwa wasigombee kupitia chama cha ccm.
na ni ukweli ccm inafanya hivyo. tena kwa hii ccm ya huyu bwana mkubwa itakua maradufu kuwafyeka wapingaji wa utendaji wa serikali maana wao hupenda zaid kusifiwa tuuuu.

wabunge pekee ambao wamekua na jicho la tatu kuisimamia serikali ni wapinzani. lakin sauti yao haifiki popote. wanamezwa na wingi wa wabunge wa ccm ambao walipaswa kuisimamia serikali ila sasa wameamua kuitetea serikali bungeni. ndipo nasema bunge la sasa halifai kuliko lile la chama kimoja.hii haimanishi sipendi vyama vingi bali naisikitikia nchi yangu kuja kupata maendeleo itachukua muda mrefu sana.mpaka wabunge waje waache kuyatumikia matumbo yao sio leo.

jiulize kama mbunge ameshindwa kuwa mzalendo kwa nchi yake ambae ana uelewa mpana kutokana na kutembea kwake na kukutana na watu mbalimbali hivyo kuwa na uelewa mpana juu ya mambo ya msingi kwa nchi yake yuko hivi walivyo wabunge wetu je kwa mwananchi wa kawaida. tunategemea mwananchi awe mzalendo huku wabunge wetu wako radhi nchi ife ila ccm ibaki ??

ukiona bunge linakubali kutoa keshi billion 500 zinunue ndege ila kwenye kilimo zinaenda billion 3 au billion 18 kwa nchi nzima tena kwa kutoa kidodo kidogo kwa nchi nzima utajua kuna mahara hatuko sawa.

naupenda upinzani ila watawala wamefanikiwa kuuzika. tuna safari kuusimamisha upinzani wa mawazo huru, zaidi ya upinzani wa vyama.
maana kwa sasa walio na mawazo huru hata ndani ya vyama huonekana wanatumiwa na wapinzani wao hata kama wanachosimamia ni kwa masrahi ya nchi. mfano huyu mbunge Bashe.na ccm wamekua na vitisho kwa wenye mawazo huru kutowarudisha kwenye kinyang’anyiro kwa awamu nyingine. hivyo basi kwa wale wafuata masrahi huufwata na kubaki kusifia tuuu.

bunge la sasa ni la hovyo kuliko la chama kimoja.
sijaelewa unazungumzia wapinzani gani..hawa ambao ni wapingaji wa kila kitu au..wapinzani hawa ambao wamenunuliwa na.mafisadi..hahahahaha...hawa waliozika ajenda za ufisadi kwenye vyama vyao...wapinzani.wa ukweli wa sasa ni.wale walioenda ccm kum support Magufuli kwa namna ya kazi anayofanya...hii ndio wananchi walikuwa wakitaka..sio ule upinzani wa kununuliwa na.mafisadi na.kuwasafisha...huko hatupo mzee
 
Ungeandika hivi:Wabunge wa CCM ni wazembe na wapuuzi wakiwa bungeni.
sasa kama.wabunge wa ccm wazembe basi tena..maaana wabunge wa upinzani si walishanunuliwa na mafisadi na wakawasafisha wote...kuna kitu tena hapo...total workdone iliyofanywagwa na.kina Dr Slaa ni sawa na.zero...wabunge hawa ambao wanaongozana na Mr Zero..hahahah hivi huwa hawaoni aibu nashangaa sana..Mr zero eti leo anaitwa kamanda, mamvi naye kamanda..hivi tutaendaje kwenye uchumi wa kati kwa unafiki huu....hahahahahahahahahaha
 
sasa kama.wabunge wa ccm wazembe basi tena..maaana wabunge wa upinzani si walishanunuliwa na mafisadi na wakawasafisha wote...kuna kitu tena hapo...total workdone iliyofanywagwa na.kina Dr Slaa ni sawa na.zero...wabunge hawa ambao wanaongozana na Mr Zero..hahahah hivi huwa hawaoni aibu nashangaa sana..Mr zero eti leo anaitwa kamanda, mamvi naye kamanda..hivi tutaendaje kwenye uchumi wa kati kwa unafiki huu....hahahahahahahahahaha
Wanaotakiwa kuuleta huo uchumi wa kati ni CCM. Hao ukinzani ni wakosoaji na waelekeza njia tu.
 
sasa kama.wabunge wa ccm wazembe basi tena..maaana wabunge wa upinzani si walishanunuliwa na mafisadi na wakawasafisha wote...kuna kitu tena hapo...total workdone iliyofanywagwa na.kina Dr Slaa ni sawa na.zero...wabunge hawa ambao wanaongozana na Mr Zero..hahahah hivi huwa hawaoni aibu nashangaa sana..Mr zero eti leo anaitwa kamanda, mamvi naye kamanda..hivi tutaendaje kwenye uchumi wa kati kwa unafiki huu....hahahahahahahahahaha

hili ndio tatizo la kufanya nchi hii imekua tatizo kwa vile chadema wamewachukua magisadi. je kabla ya. hao unawaita mafisadi kwenda chadema ccm ilifanya nini? au unataka kusema kwamba tumepata uhuru 2015 na sasa tuko nchi huru baada ya wakoloni akina Lowasa kwenda nchi nyingine chadema,?? tumia akili
 
sasa kama.wabunge wa ccm wazembe basi tena..maaana wabunge wa upinzani si walishanunuliwa na mafisadi na wakawasafisha wote...kuna kitu tena hapo...total workdone iliyofanywagwa na.kina Dr Slaa ni sawa na.zero...wabunge hawa ambao wanaongozana na Mr Zero..hahahah hivi huwa hawaoni aibu nashangaa sana..Mr zero eti leo anaitwa kamanda, mamvi naye kamanda..hivi tutaendaje kwenye uchumi wa kati kwa unafiki huu....hahahahahahahahahaha
uchumi wa kati wa kufungua viwanda vya maji ya kunywa? au kukipa kilimo 22%
 
Back
Top Bottom