Kwa staili hii itatugharimu muda mrefu

oba

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
310
65
Ni ukweli uliowazi kuwa watanzania walio wengi wakipewa nafasi ya kueleza nini chanzo cha matatizo na umaskin wetu huitupia lawama serikali hasa kwa kushindwa kuratibu maendeleo na ukombozi wetu.
Moja ya mambo ambayo yananikera sana katika usimamizi na uendeshaji wa shughuri za serikali ni kitendo cha kuingia kwenye ofisi fulani ukiwa na shida na kukutana na askari kufuli akining'inia mlangoni eti kwasababu mhusika yuko kwenye kikao au amesafiri.
Huwa ninajiuliza ofisi ni ya serikali au ya mtu binafsi?iweje mtu akisafiri au kwenda kwenye kikao ofisi ifungwe?hakuna utaratibu wa mtu kubaki na ofisi atleast akaendeleza huduma kwa wateja?wafanyakazi kama hao wanachukuliwa hatua gani na wasimamizi wao?au wanaogopa kumwachia ofisa mwingine asije akagundua madudu na uozo unaofanywa kwenye ofisi hizo?
Kwa staili hii, na kwa kukosa uwajibikaji wa viongozi na wafanyakazi katika level zote,hatuwezi kupata maendeleo leo wala kesho.
Nawasilisha!
 
Ni ukweli uliowazi kuwa watanzania walio wengi wakipewa nafasi ya kueleza nini chanzo cha matatizo na umaskin wetu huitupia lawama serikali hasa kwa kushindwa kuratibu maendeleo na ukombozi wetu.
Moja ya mambo ambayo yananikera sana katika usimamizi na uendeshaji wa shughuri za serikali ni kitendo cha kuingia kwenye ofisi fulani ukiwa na shida na kukutana na askari kufuli akining'inia mlangoni eti kwasababu mhusika yuko kwenye kikao au amesafiri.
Huwa ninajiuliza ofisi ni ya serikali au ya mtu binafsi?iweje mtu akisafiri au kwenda kwenye kikao ofisi ifungwe?hakuna utaratibu wa mtu kubaki na ofisi atleast akaendeleza huduma kwa wateja?wafanyakazi kama hao wanachukuliwa hatua gani na wasimamizi wao?au wanaogopa kumwachia ofisa mwingine asije akagundua madudu na uozo unaofanywa kwenye ofisi hizo?
Kwa staili hii, na kwa kukosa uwajibikaji wa viongozi na wafanyakazi katika level zote,hatuwezi kupata maendeleo leo wala kesho.
Nawasilisha!


Mkuu nafikiri haya hayajaanzia kwa wafanyakazi wa ngazi ya chini yameanzia juu huko hakuna uwajibikaji mtu anahesabika ndio ofisi na kama hayupo ina maana ndio ofisi haipo
 
Back
Top Bottom