Mwaka jana. wazanzibari waliujadili muungano na kuamua kuuvunja kwa kuitambua Zanzbar kuwa ni nchi. Mipaka ya kuujadili ama kuhoji juu ya muungano wanawekewa watanganyika tu, maana wazanzibari walishaujadili siku nyingi na wakaamua kuuvunja. Yaani Zanzbar imekuwa dogo janja na Tanganyika Kubwajinga? Hili hatutakubali. Tunaitaka Tanganyika yetu au la mabadiliko ya katiba ya Zanzbar yanayoitambua Zanzbar kuwa nchi yafutwe na wote tubaki watanzania tu.