Sababu
1.Wanaume wengi ndiyo watafutaji hivyo ukiwa na nyota nzuri ya kipato kuwa zezeta ni rahisi kwani wachawi na walozi huihitaji kwa ajili ya kazi zao.
2.majukumu ya familia mazito huwafanya wengi kuzidiwa na hivyo kuona suluhisho ni ulevi ambao hupelekea wengi kuwa vichaa.
3.watumiaji wengi wa madawa ya kulevya ni wanaume hivyo possibility ya kuwa vichaa ni kubwa.
4.pesa za ndagu nyingi hutafutwa na wanaume hivyo ngoma ikigoma lazima uwe kichaa tu.
5.limbwata,wanaowekewa limbwata za mapenzi ni wanaume hivyo nazo zikibuma ukichaa nje nje.
6.kurithi,ktk familia ukoo hubebwa na mwanaume hivyo kama kuna ukichaa basi hutembea kizazi chote kuwadhuru wanaume japo na wanawake waweza kupata in rarely cases.
7.matambiko,siku zote matambiko hushikiliwa na wanaume hivyo asipotii lazime dish liyumbe tu.
8.Ajali,hii husababisha mtu kuwa kichaa ikiwa ataumia sehemu ya kichwa vibaya.Wasafiri wengi ni wanaume kuliko wanawake.
9.Ukali wa wanawake kuwatesa wanaume.Kuna wanaume ambao ndoa zao ni mateso mno mtu anatamani akaishi jela kuliko kuishi na mwanamke sampuli hiyo hivyo mwanaume kuwa kichaa ni kama kumgusa mlevi.Imagine baba aliyeenda kupora pesa benki ili afungwe jela akae mbali na mkewe lakn mahakama nayo ikamfunga kifungo cha nje na kuwa asitoke nyumbani bila idhini ya mke huko marekani.
10.wezi wengi ni wanaume hivyo ikitokea akarogwa basi ukichaa ni wake.
11.Malipizi,hii hutokea ikiwa ndoa imekufa na mwanamke hataki hivyo mme hurogwa kuwa kichaa na mengineyo.
12..Mengineyo,hapa zipo sababu zisizo onekana ambazo ni chanzo cha wanaume kuwa vichaa.
Nadhani sababu ni zaidi ya hizi ila wengine watafafanua zilizosalia.