Kwa nini tuwekeane vikwazo, tunashindana na nani?

Kwa nini tuwekeane vikwazo, tunashindana na nani?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
37,104
Reaction score
55,514
Unajua kabisa hapa duniani tunapita, wengi kufikisha miaka 90 ni bahati nasibu, kwa nini sasa tunaishi kwa kuteseka?

Unaamka asubuhi unawahi kibaruani, mara ufokewe na bosi wako, hayo yote ni ya nini? Kwa nini usiishi kama ndege tu, katika kujipatia mahitaji yako ya kila siku huku ukingojea siku ya mwisho?

Mengi tunayoyafanya hapa duniani ni mbwembwe tu, mwisho wa siku mwili wako tu utavishwa vazi la kawaida na kufukiwa, sasa mbwembwe zote ni za nini?

Unamuajiri mwenzako, unampunja ujira wake kwa kumlipa malipo madogo, yote ni ya nini; tunashindana na nani?

Unaingia kwenye mahusiano, mnaanza kutanguliza hela mbele,wakati kila kitu mmepewa bure kwa muundo unaofanana, hasi na chanya; sasa Unashindana na nani?

Mi naona watu wote duniani waishi kwa uhuru tu, waende popote duniani wanapoweza kwenda bila vikwazo mipakani, pia wale chochote wanachokiona kinafaa kuliwa, wale matunda pori na wanyama pori bila kuwa na kizuizi chochote kile, wawe huru kuongea wayapendayo; huo ndio ubinadamu katika kuishi kwa siku zinazohesabika hapa duniani.

Kwa nini tuwekeane vikwazo, tunashindana na nani?​
 
vikwazo ni vingi sana
Screenshot_20250724-164215~2.jpg
 
Ukifikiria saaaana aya maisha, utaina bora ukakae zako Tukuyu uwe unalima na kula vizuri sio kuangaika na foleni za Kimara.
Kabisa mdau. Maisha yana mengi kiasi kwamba ukiyawaza unaishia kuhisi kama kichwa kinataka kypasuk
Inabidi kubadili mitazamo
The best option ni kuweka mpaka wa do and don'ts.. hii itasaidia katika kutowakanyaga binadamu wenzako
 
Maisha yanapaswa kuwa mepese tu. Na ndivyo Mungu alipanga na kutaka tangia zamani za Eden.
Tatizo tamaa ya mwanadamu kutaka kupata zaidi ya anachohitaji kuishi.
Fikirian mtu kama SAMIA, ana pesa pamoja na pension nzuri ya uraisi, lakini bado anangangana hata kutesa na kuua mwanadamu mwenzake ili apate zaidi na ziada ya malai ambayo hawezi kuitumia akaimaliza na ataiacha pindi atakapokufa.
 
Nafikiri ai itakuja solve haya matatizo yote tuliyojitengenezea yaliyoletwa na greedy people, wafia dini na wapumbavu
 
Uhuru ulio pitiliza ni chanzo Cha hatari katika Uhuru "TOO MUCH IS HARMFUL".
 
Back
Top Bottom