Kwa nini serikali ya Tanganyika inaogopwa?

Kwa nini serikali ya Tanganyika inaogopwa?

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
9,571
Reaction score
35,484
Wataalam na wajuzi wa mambo nijuzeni,ni kwa sababu gani serikali ya Tanganyika inaogopwa,hususani na watawala waliopo madarakani?

Kwa kifupi Tume ya Jaji Francis Nyalali ilipendekeza serikali 3,tume ya Jaji Kisanga ilipendekeza serikali3,tume ya Jaji Warioba imependekeza serikali 3.

Zote hizi mapendekezo yake yalikataliwa na watawala tena kwa kashfa na kejeli.mfano,Jaji Kisanga alishutumiwa na Mkapa sana kuhusu mapendekezo yake ya serikali tatu.

Kwa mtindo uleule naye Kikwete kamshutumu Jaji Warioba na kumzodoa kwa ujanja wa panya wa kuuma na kupuliza.Nashangaa sana licha ya tume hizi kukusanya maoni ya wananchi na sio maoni ya wakuu wa tume hizo.

Isitoshe iweje maoni yote ya tume yafanane tene kwa nyakati tofauti lakini wakuu bado hawakubali maoni ya wananchi.

Hii tume ya warioba iliundwa na makada madhubuti wa ccm.mfano mkubwa ni Warioba mwenyewe na Salim Ahmed salim,lakini bado CCM wa leo hawakuridhika.

Wajumbe hao wawili niliowataja warioba na salim wangekua hawajulikani imani zao ingesemwa wametumwa na wapinzani.Hayo ni machache kati ya mengi yanayonishangaza.kuna nini kati ya watawala na uwepo wa Tanganyika?
 
Salm,Butiku,Paramagamba,jaji Agustino,profesa Baregu na wajumbe wengine wote mliokuwa kwenye hiyo tume ya kukusanya maoni jitokeza sasa mtueleze watanzania ukweli,kimya chenu ndo msingi mkuu ya porojo na propaganda za raisi Kikwete.
 
Serikali ya Tanganyika inaogopwa kwa sababu
-Itavunja muungano
-Gharama kubwa ya kuendesha serikali 3
-Hapatakuwa na usalama.
 
Wataalam na wajuzi wa mambo nijuzeni,ni kwa sababu gani serikali ya Tanganyika inaogopwa,hususani na watawala waliopo madarakani?

Kwa kifupi Tume ya Jaji Francis Nyalali ilipendekeza serikali 3,tume ya Jaji Kisanga ilipendekeza serikali3,tume ya Jaji Warioba imependekeza serikali 3.

Zote hizi mapendekezo yake yalikataliwa na watawala tena kwa kashfa na kejeli.mfano,Jaji Kisanga alishutumiwa na Mkapa sana kuhusu mapendekezo yake ya serikali tatu.

Kwa mtindo uleule naye Kikwete kamshutumu Jaji Warioba na kumzodoa kwa ujanja wa panya wa kuuma na kupuliza.Nashangaa sana licha ya tume hizi kukusanya maoni ya wananchi na sio maoni ya wakuu wa tume hizo.

Isitoshe iweje maoni yote ya tume yafanane tene kwa nyakati tofauti lakini wakuu bado hawakubali maoni ya wananchi.

Hii tume ya warioba iliundwa na makada madhubuti wa ccm.mfano mkubwa ni Warioba mwenyewe na Salim Ahmed salim,lakini bado CCM wa leo hawakuridhika.

Wajumbe hao wawili niliowataja warioba na salim wangekua hawajulikani imani zao ingesemwa wametumwa na wapinzani.Hayo ni machache kati ya mengi yanayonishangaza.kuna nini kati ya watawala na uwepo wa Tanganyika?
.....Zanzibar ni corridor ya kupokea na kutoroshea mali kutoka katika ukanda wote huu, mfano hivi majuzi tu si mmesikia pembe za ndovu zimekamatwa,je magogo?...sb ni kuwa Zanzibar haina sheria kupinga maovu hayo....ni hivi majuzi ndo wamefanya geresha.....lakini zenj inausika sana,pia watawala wanatumia zenj kuchota fedha sb gharama za kuchangia muungano...ktk serikali 3 haiwezekani pia zenj na tanganyika katiba zao itabidi katiba zao iendane na ya muungano....so watakuwa na sheria kali kuhusu pembe za ndovu,ngozi ya chui,etc
 
Serikali ya Tanganyika inaogopwa kwa sababu
-Itavunja muungano
-Gharama kubwa ya kuendesha serikali 3
-Hapatakuwa na usalama.
Muungano ukivunjika kuna tatizo gani,acha kukariri wanasiasa ,je kabla ya muungano Tanganyika hapakuwa na usalama?
 
mimi napendekeza serikali moja
Kama vipi basi twende kwenye serikali tatu
Nawasahangaa sana wanaomkejeri Mtikila kwa hoja yake ya kuitaka Tanganyika
 
.....Zanzibar ni corridor ya kupokea na kutoroshea mali kutoka katika ukanda wote huu, mfano hivi majuzi tu si mmesikia pembe za ndovu zimekamatwa,je magogo?...sb ni kuwa Zanzibar haina sheria kupinga maovu hayo....ni hivi majuzi ndo wamefanya geresha.....lakini zenj inausika sana,pia watawala wanatumia zenj kuchota fedha sb gharama za kuchangia muungano...ktk serikali 3 haiwezekani pia zenj na tanganyika katiba zao itabidi katiba zao iendane na ya muungano....so watakuwa na sheria kali kuhusu pembe za ndovu,ngozi ya chui,etc

Kwaiyo Tanganyika kuna sheria ya kupinga maovu lakini haifanyi kazi au? Kwani izo pembe zinatoka wapi? Na zimekamatwa mara ngapi pembe izo katika ardhi ya Tanganyika? Usiongee pumba na usiogope kusema kweli, Tanganyika inaogopwa kwa sababu itachelewa sana kusonga mbele na madeni ilonayo
 
Serikali ya Tanganyika inaogopwa kwa sababu
-Itavunja muungano
-Gharama kubwa ya kuendesha serikali 3
-Hapatakuwa na usalama.
The betterment of human living haijumuishi hivi ulivyovitaja ndugu, ungelitaja kuwa itashusha ukuuaji wa uchumi ningelikubaliana nawe.
Mfumo wa utoaji maamuzi ya kitaifa katika mfumo wa sasa wa muungano ni swa na mtu anayetaka kwenda Mbeya akitokea DSM, akaanza kwa kwenda Bagamoyo - Kabuku - Segera - Mombo - Moshi - Arusha - Babati - Singida - Dodoma - Mtera - Ipogolo - Makambako - Mbeya. Huyu mtu atafika Mbeya lakini itakuwa tofauti na DSM - Chalinze - Moro - Mikumi - Ipogolo - Makambako - Mbeya.
Natumia mfano huu rahisi ili tuone kama tutaelewana. Lakini bahati mbaya sana ccm wanalijua hili bali wanajifanya hawalioni kwa kujidai kuwa wanalinda maslahi ya taifa kumbe wanalinda maslahi ya chama ambacho advantages zake ziko kwenye urasimu.
 
siyo tanganyika inaogopwa, swali kwanini viongozi wetu wanawaogopa wazanzibar?
 
Wataalam na wajuzi wa mambo nijuzeni,ni kwa sababu gani serikali ya Tanganyika inaogopwa,hususani na watawala waliopo madarakani?

Kwa kifupi Tume ya Jaji Francis Nyalali ilipendekeza serikali 3,tume ya Jaji Kisanga ilipendekeza serikali3,tume ya Jaji Warioba imependekeza serikali 3.

Zote hizi mapendekezo yake yalikataliwa na watawala tena kwa kashfa na kejeli.mfano,Jaji Kisanga alishutumiwa na Mkapa sana kuhusu mapendekezo yake ya serikali tatu.

Kwa mtindo uleule naye Kikwete kamshutumu Jaji Warioba na kumzodoa kwa ujanja wa panya wa kuuma na kupuliza.Nashangaa sana licha ya tume hizi kukusanya maoni ya wananchi na sio maoni ya wakuu wa tume hizo.

Isitoshe iweje maoni yote ya tume yafanane tene kwa nyakati tofauti lakini wakuu bado hawakubali maoni ya wananchi.

Hii tume ya warioba iliundwa na makada madhubuti wa ccm.mfano mkubwa ni Warioba mwenyewe na Salim Ahmed salim,lakini bado CCM wa leo hawakuridhika.

Wajumbe hao wawili niliowataja warioba na salim wangekua hawajulikani imani zao ingesemwa wametumwa na wapinzani.Hayo ni machache kati ya mengi yanayonishangaza.kuna nini kati ya watawala na uwepo wa Tanganyika?

Kwa wale wenye mawazo hasi na tanganyika tanganyika kwao ni sawa na jitu kubwa lenye kutia hofu lakini kwa wenye mtazamo chanya inamaanisha neema, heri, matumaini na amani (Kumbuka hii ni tafsiri yangu na wala haifungamani na tafsiri za wengine)
 
Back
Top Bottom