MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 21,762
- 71,790
Waswahili husema unachokipanda ndio unakivuna. Wacha United of America ivuliwe nguo.Raisi Obama ni kiongozi wa taifa kubwa na lenye nguvu sana hapa duniani.
Kwenye masuala ya Ulinzi ndiyo usiseme kabisa. Wako mbele zaidi ya nchi nyingi hapa duniani kwenye masuala ya TEHAMA, miaka kama mitatu iliyopita tulisikia shutuma mbali mbali dhidi ya shirika la kijasusi la Marekani (N.S.A) kwamba lilikuwa linadukua mawasiliano ya viongozi wakubwa wa nchi tofauti hapa duniani.
Hata kwa kiburi zaidi satelaiti ya shirika hilo iliyorushwa mwaka juzi ilichorwa mnyama aina ya Pweza akiizunguka dunia na wakaandika maneno "NOTHING IS BEYOND OUR REACH" . Wamarekani walimdukua Waziri mkuu wa Ujerumani hata kabla hajawa waziri mkuu. Kiukweli kuyafanya haya inahitaji taifa liwe na uwezo wa kipekee sana katika teknolojia.
Lakini kuna msemo husema "MUOSHA HUOSHWA"
Marekani na yeye kadukuliwa tena kibaya zaidi siyo na taifa bali na genge la watu.
Kama taarifa za muhimu za Waziri wa mambo ya nje zinavuja vile Je nchi ya Marekani ipo salama kweli? Sasa kinacholeta maswali mengi ni kwamba wanaofanya hivyo ni akina nani?
Je, ni kweli Warusi? Wachina? Wikileaks? Wamarekani? au ni Edward Snowden?
Kudukuliwa kwa mtu kama Hillary Clinton kunaweza kusamehewa kwasababu yule mama alitumia barua pepe binafsi: Lakini hili la leo la mawasiliano ya barua pepe za raisi Obama kuvujishwa na WIKILEAKS limekuwa ni gumu kumeza. Kwa kifupi raisi wa Marekani anatumia anuani ya peke yake ya barua pepe ambayo mtu wa kawaida huwezi kujua. Lakini cha kushangaza mawasiliano ya Obama kabla na baada ya kuwa raisi yamevujishwa nje leo.
Kama hili lingetokea wakati wa vita wangepona kweli?
Na kuvuja kwa taarifa hizi siyo mkono wa mtu wa nje peke yake lazima Wamarekani wenyewe wanahusika moja kwa moja. Sasa wataalamu mtuambie kama Raisi Obama anadukuliwa kama mimi MALCOM LUMUMBA, bado tutaendelea kujiaminisha kwamba Marekani haigusiki na bado ipo salama?
Link:WikiLeaks - The Podesta Emails
CC: Bukyanagandi , Bowie , maalimu shewedy , Barbarosa
Finally Leo nimekuona aisee ulipoteaKikulacho ki nguoni mwako....!
Na ni Mungu pekee ndie asiyeweza kudukuliwa kwakuwa yeye si kazi ya mwanadamu
Nipo nimerejea nina siku ya tatu sasaFinally Leo nimekuona aisee ulipotea
Ukifuatilia ishu ya snowden utagundua kwamba tupo under surveillance hakuna usiriTutarudi kutumia barua na moshi kutuma ujumbe la sivyo hamna mtu yupo salama.
Ushasema marekani IPO mbele kwa tehama,"zaidi ya nchi nyingi",kwa maana hiyo kuna nchi zipo mbele ya marekani kwa masuala ya Tehama,sasa kwa nn asidukuliwe??Raisi Obama ni kiongozi wa taifa kubwa na lenye nguvu sana hapa duniani.
Kwenye masuala ya Ulinzi ndiyo usiseme kabisa. Wako mbele zaidi ya nchi nyingi hapa duniani kwenye masuala ya TEHAMA, miaka kama mitatu iliyopita tulisikia shutuma mbali mbali dhidi ya shirika la kijasusi la Marekani (N.S.A) kwamba lilikuwa linadukua mawasiliano ya viongozi wakubwa wa nchi tofauti hapa duniani.
Hata kwa kiburi zaidi satelaiti ya shirika hilo iliyorushwa mwaka juzi ilichorwa mnyama aina ya Pweza akiizunguka dunia na wakaandika maneno "NOTHING IS BEYOND OUR REACH" . Wamarekani walimdukua Waziri mkuu wa Ujerumani hata kabla hajawa waziri mkuu. Kiukweli kuyafanya haya inahitaji taifa liwe na uwezo wa kipekee sana katika teknolojia.
Lakini kuna msemo husema "MUOSHA HUOSHWA"
Marekani na yeye kadukuliwa tena kibaya zaidi siyo na taifa bali na genge la watu.
Kama taarifa za muhimu za Waziri wa mambo ya nje zinavuja vile Je nchi ya Marekani ipo salama kweli? Sasa kinacholeta maswali mengi ni kwamba wanaofanya hivyo ni akina nani?
Je, ni kweli Warusi? Wachina? Wikileaks? Wamarekani? au ni Edward Snowden?
Kudukuliwa kwa mtu kama Hillary Clinton kunaweza kusamehewa kwasababu yule mama alitumia barua pepe binafsi: Lakini hili la leo la mawasiliano ya barua pepe za raisi Obama kuvujishwa na WIKILEAKS limekuwa ni gumu kumeza. Kwa kifupi raisi wa Marekani anatumia anuani ya peke yake ya barua pepe ambayo mtu wa kawaida huwezi kujua. Lakini cha kushangaza mawasiliano ya Obama kabla na baada ya kuwa raisi yamevujishwa nje leo.
Kama hili lingetokea wakati wa vita wangepona kweli?
Na kuvuja kwa taarifa hizi siyo mkono wa mtu wa nje peke yake lazima Wamarekani wenyewe wanahusika moja kwa moja. Sasa wataalamu mtuambie kama Raisi Obama anadukuliwa kama mimi MALCOM LUMUMBA, bado tutaendelea kujiaminisha kwamba Marekani haigusiki na bado ipo salama?
Link:WikiLeaks - The Podesta Emails
CC: Bukyanagandi , Bowie , maalimu shewedy , Barbarosa
Welcome back maana walishaanza kusema mshana ndio scorpion mbn tokea akamatwe scorpion mshana jr hatumuoni humuuNipo nimerejea nina siku ya tatu sasa
[emoji3] [emoji3] [emoji3] niliambiwa nikaishia tu kuchekaWelcome back maana walishaanza kusema mshana ndio scorpion mbn tokea akamatwe scorpion mshana jr hatumuoni humuu
Si walikuja hapa tukawakabidhi ikulu yetu wakapanda mpaka darini tena bila wanausalama wetuUkifuatilia ishu ya snowden utagundua kwamba tupo under surveillance hakuna usiri
Kweli, Enzi za Nyerere CIA waliweka submarine karibu na bandari bila sisi kujua wakawa wanaskiliza mazungumzo ya Magogoni.Ukifuatilia ishu ya snowden utagundua kwamba tupo under surveillance hakuna usiri
CIA wana submarine? Halafu kipindi cha nyerere mawasiliano makubwa yalikuwa ni ya offline sasa walikuwa wanadukua nini? Na ni nani aliyegundua uwepo wa submarine hiyo?Kweli, Enzi za Nyerere CIA waliweka submarine karibu na bandari bila sisi kujua wakawa wanaskiliza mazungumzo ya Magogoni.
Conspiracy theory kivipi?Conspiracy theory hiyo, hakuna chochote kilichovuja, na kama kuna taarifa zimevuja ni wao ndo wanavujisha tena zinakuwa ni za uongo ili kuwachanganya watu wasijue kinachoendelea.
Content za email tafadhali.
Ushasema marekani IPO mbele kwa tehama,"zaidi ya nchi nyingi",kwa maana hiyo kuna nchi zipo mbele ya marekani kwa masuala ya Tehama,sasa kwa nn asidukuliwe??
Jaribu kutafuta info jinsi CIA walivyokuwa wanajaribu kumtrack Che Guevera alivyokuwa Tanzania halafu utapata majibu yote ya maswali yako.CIA wana submarine? Halafu kipindi cha nyerere mawasiliano makubwa yalikuwa ni ya offline sasa walikuwa wanadukua nini? Na ni nani aliyegundua uwepo wa submarine hiyo?