Kwa nini ni ulaya Tu na sio bongo

Kwa nini ni ulaya Tu na sio bongo

iphone 18 promax

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2012
Posts
2,918
Reaction score
2,151
Ulaya ununuzi wa vitu kuanzia simu ,magari wananunua kwa kulipia kidogo kidogo mpaka MTU wnamaliza na incase likatoka Toleo mfano jipya unafanya top-up je kwa nini kampuni za simu huku bongo haziwezi kufanya mpango huu na wakapata Faida kubwa Tu tatizo ni nini?
 
Ndiyo maana tunaanza na zoezi la anuani za makazi. Mpaka huu mfumo utengemae.

Pia kama alivyosema edwayne hapo juu, mfumo mzuri wa pension huhakikisha kila mtu ana namba yake ya pension tangu anazaliwa. Hiyo namba ndiyo inayotumika kukutofautisha wewe na wengine.
Kipato chako na ustahimilivu wa madeni yako hujulikana kwa kupitia namba yako ya pension.
Tanzania bado tuna imani za kishiriki a hata anuani hatutaki.

Ndiyo maana ni rahisi kuwakopesha wafanyakazi, kwa sababu wengi wao kipato kinaweza kujulikana kirahisi digitally na kutoa fedha.
Tujipe miaka 50 hadi 200.
 
Ndiyo maana tunaanza na zoezi la anuani za makazi. Mpaka huu mfumo utengemae.

Pia kama alivyosema edwayne hapo juu, mfumo mzuri wa pension huhakikisha kila mtu ana namba yake ya pension tangu anazaliwa. Hiyo namba ndiyo inayotumika kukutofautisha wewe na wengine.
Kipato chako na ustahimilivu wa madeni yako hujulikana kwa kupitia namba yako ya pension.
Tanzania bado tuna imani za kishiriki a hata anuani hatutaki.

Ndiyo maana ni rahisi kuwakopesha wafanyakazi, kwa sababu wengi wao kipato kinaweza kujulikana kirahisi digitally na kutoa fedha.
Tujipe miaka 50 hadi 200.
Hiyo anuani ya makazi ni mradi kwa walio na nyumba zao. Ila kwa mtu wa maisha ya kuhamahama yaani kambi popote. Huo mradi haufai. Maana mtu leo upo hapa, wiki ijayo umehamia mtaa wa nne, mwezi ujao upo kata ya tatu, miezi mitatu umehamia wilaya nyingine na mwakani upo mkoa mwingine 😂😂😂. Hiyo anuani watakuta manyoya
 
😂😂😂😂

Kwa ulaya na Usa wanamuona mchovu. Maana disposable income inakuwa kidogo. Disposable income ni pesa inayobakia baada ya kulipa kodi na matumizi yote ya kila siku.
Unazungumzia nchi ambazo kama Nyumba Haina a/c serikali inachukua watoto wako.
Kama Hamna Umeme inakuwa condemned.
Disposable income ya Africa inatokana na kuishi maisha ya hali ya Chini.
 
Hiyo anuani ya makazi ni mradi kwa walio na nyumba zao. Ila kwa mtu wa maisha ya kuhamahama yaani kambi popote. Huo mradi haufai. Maana mtu leo upo hapa, wiki ijayo umehamia mtaa wa nne, mwezi ujao upo kata ya tatu, miezi mitatu umehamia wilaya nyingine na mwakani upo mkoa mwingine 😂😂😂. Hiyo anuani watakuta manyoya
Huwezi kuhama bila kujulikana. Si rahisi kuuelewa mfumo huu mpaka utengemae. Ndiyo mwanzo wa kuishi kistaarabu na kidijitali. Anuani ni data.
Pia namba yako ya kustaafu huwezi kuikimbia ukienda hospitali au ukitaka huduma yeyote serikalini au kijamii utaitaja namba. Hapo utajulikana upo wapi.
 
Ulaya ununuzi wa vitu kuanzia simu ,magari wananunua kwa kulipia kidogo kidogo mpaka MTU wnamaliza na incase likatoka Toleo mfano jipya unafanya top-up je kwa nini kampuni za simu huku bongo haziwezi kufanya mpango huu na wakapata Faida kubwa Tu tatizo ni nini?
Kuna vitu vya msingi ambavyo US na Europe vipo kwa ajili ya kumfuatilia mteja ambavyo Afrika hakuna!! Sio kwamba Ulaya na Marekani watu hawaingii mitini, hell no... wapo wanaoingia mitini; and back in the days miongoni mwa freelancing jobs nilizowahi kufanya ni pamoja na Skip Tracing!!

Skip tracing ni kufuatilia watu walio-default!! Mwingine akiona mambo magumu, anahama hadi state kwahiyo unaanza tracing kufahamu kahamia state ipi, mji upi, na address yake mpya ni ipi!!

Sasa Kibongo bongo, mtu hata credit card hana, physical address hazieleweki, hata utlity bills history huwezi kuzipata! On top of that, sidhani kama tuna mfumo mzuri wa credit bureau!!

Sasa mtu kama huyo akishaingia mitini sijui utamtolea wapi!

Back in the days nilidhani Kibongo bongo ni rahisi kufanya hivyo kwa wafanyakazi, especially wa serikali... and YES, possible lakini sitamsahau mtu mmoja ambae alikuwa mfanyakazi wa serikali kwa jina Mike!

Wakati huo nilikuwa kwenye benki moja, sasa jamaa kaja kuomba mkopo! Mwana alikuwa mshikaji ile mbaya, kwahiyo fasta fasta tukampa mkopo!!

Kilichonishangaza, baadae akatupigia simu mimi na washikaji wengine wawili pale benki, akatuomba tukakutane nae kwenye hotel moja hivi ufukweni!

Nilichukulia kawaida tu lakini kufika kule, kumbe jamaa katuita kula bata!! Pesa iliteketea ile mbaya but I wasn't comfortable at all. Siku mbili tatu baadae tunapata taarifa Richie kahamishiwa mkoa!!

Kumbe wakati anakuja benki alifahamu kwamba anahama jiji! Making things worse, wiki chache baadae tunaletewa taarifa kwamba Mike kafariki! Tukashangaa kulikoni.

Kumbe jamaa alikuwa na ngoma, ndo maana akaomba uhamisho kwenda mkoa wa kwao, na piaalifahamu kwamba hakuwa na muda mrefu duniani though usingeweza kumgundua kwamba anaumwa!!

Sasa hao ndo Waafrika... of course, hata Ulaya na America wapo wa aina hiyo lakini kule ni mifumo mizuri ya kuweza kuwafuatilia!!
 
angalia mfano huko hakuna mtu halipi kodi tu,ije kuwa deni la kampuni au taasisi!!!utalipa tu as long as pesa zako ziko chini ya mfumo rasmi inafuatiliwa na inatambulika.

jina lako ulaya limebeba taarifa zako zote mpaka nyumba unayoishi kazi unayofanya na jumla ya kipato,na hakuna kuzurula na mahela kwenye mikoba maana pesa zote zinatembea kidigitali.
 
Back
Top Bottom