Kwa nini ccm isiwe na katibu mkuu mwanamke?

Kwa nini ccm isiwe na katibu mkuu mwanamke?

mlimbwa1977

Member
Joined
Feb 7, 2011
Posts
24
Reaction score
0
Wakati wa uteuzi wa mgombea kiti cha uspika ndani ya CCM mbiu ilikuwa ni wakati mwafaka kwa mwanamke kushika moja ya mihimili ya dola,ndipo tuliposhuhudia Ndugu Samwel Sita akienguliwa.

Ukiangalia safu ya uongozi mkuu wa chama hiki ukianzia mwenyekiti,m/mwenyekiti,Katibu mkuu,na wasaidizi wake wote ni wanaume.Je mbiu iliyokuwa ikiimbwa ya kuwapa wanawake madaraka makubwa ilikuwa hadaa kwa watanzania au ilikuwa ni chuki binafsi dhidi ya spika sita?

Kwa hakika sifurahii kabisa sera ya kupeana madaraka kama chakula,eti wabunge viti maalum!! mfumo huu unawadumaza wanawake na kujiona wao ni watu wa kupewa tu bila kuvuja jasho.Kadri watakavyojitokeza kwa wingi majimboni jamii itawakubali na hatimaye kuongezeka bungeni wakiwa na ajenda mahsusi zinazowapeleka kwa lengo la kuwakilisha jamii wanakotoka badala ya sasa.

Naomba tuchangie kwa masuala yote haya mawili.karibuni.ELEWA KADRI UNAVYOTOA MAWAZO YAKO CHANYA YANAWEZA KUSAIDIA KUIJENGA INCHI YETU.
 
Kama ccm wanataka kuweka mwanamke nafasi hiyo wasisite kumpa Sophiiiiiiiiii maana nae ana pumba sana kaama kaka yake alietoka!midomo mali yao wote hao akili na fikra hakuna
 
Mipasho ya bungeni haijakuchosha?

Wanajiandaa kwa vita ya 2015....na wakati huo ni vita....na kina mama wetu wa TZ bado hawajaonesha kama wanaweza kuchuna uso na kudanganya bila kusikia aibu katika medani ya siasa.
 
Ndg c umesema atapewa moja ya mhimili wa dola,sasa c kashapewa Bunge! ccm sio mhimili wa dola ni chama tawala.
 
maana yangu ni kwamba kama lengo ni kuwapa wanawake nafasi za juu katika uongozi,CCM kama chama kilichoonyesha nia hiyo kwa nafasi ya uspika nia hiyo ingeendelea hata ndani ya chama.
 
dah maamuz ya mwanamke ndan ya chama italeta pumba kibao kama bungen
 
Back
Top Bottom