Kwa Niaba ya Raisi: Maamuzi Magumu!

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
WanaJF,

Sasa tuache lawama, ushabiki, matusi, shutuma, umbea, uongo, uzandiki, ukada, udini, ukabila, uonevu na uchochezi. Tuache yote na tujenge nchi yetu. Kama ni lawama, matusi, shutuma, udhaifu, mapungufu nk tumeshayataja! Sasa tuseme tunaenda wapi.

Kwa niaba ya Raisi nachukua maamuzi yafuatayo;

1.Najiuzulu wadhifa wangu wa u-Raisi, ukuu wa majeshi na uenyekiti wa chama!

2.WanaJF waunde serikali kutoka miongoni mwao wanayoiona ina uwezo wa kutatua matatizo ya wananchi. Mawaziri hao watoe mipango kazi yao ya nini kifanyike na kifanyike vipi ili kuokoa taifa.

Mpaka sasa najua matatizo ambayo WanaJF wanayaona na kuyasema sana dhidi ya Serikali yangu, Ufisadi, Rushwa, Elimu, Ajira, Afya, Matumizi mabaya ya ofisi, Umeme, Miundombinu, Mfumuko wa bei, Ujambazi, Unyanyasaji wa kijinsia, Mauaji ya Albino, Mauaji ya Wazee, Malipo ya Wazee wa East Africa, Malipo ya Dowans, Migomo, Matatizo ya Walimu, Madaktari na Wafanyakazi wengine nk! Kwa kweli nakubali ni mengi!

Ni matumaini yangu viongozi wazuri watapatikana kwa mfano, Mzee Mwanakijiji, Waberoya, Mohamed Shossi, Michelle, Birigita, Denyo, Rev Masanilo, Voiceof Reason na wengineo wengi! Kila anayeonekana anafaa atoe mapendekezo ya kina kuhusu wizara yake!

Kelele za kupanda bei ya nishati zibadilike kuwa mapendekezo kuhusu nini kifanyike! Mikataba mibovu yatolewe mapendekezo mikataba hiyo ifanyweje!

WanaJF, forum yenu iwe chimbuko la suluhisho na sio mfereji wa lawama. Sio kwamba msilaumu au msifichue ufisadi bali kama viongozi sasa mtoe solutions kulingana na hali halisi.

Shutuma na lawama zenu zimenisababisha niwarudie niwaombe mnisaidie kuongoza kwani mnaonekana mnao uwezo mkubwa. Nadhani hilo mtaliweza. Semeni bila kuficha nini kifanyike kutatua matatizo hayo mnayoyapigia kelele kila kukicha. Imefika mahali kelele za mlango zinamzuia mwenye nyumba kulala! Sipati usingizi!
 
You are right mkuu,lakini inabaki kuwa imagination,we must act.
In order to conquer them we must dare and keep daring forever
 
Natamani iwe sasa itakuwa ni furaha ilioje Tz. kufanya power transition kwa amani na utulivi bila kuingiliwa na vibendera mfuata upepo. Hayawi hayawi mwisho yatakuwa.
 
WanaJF,

Sasa tuache lawama, ushabiki, matusi, shutuma, umbea, uongo, uzandiki, ukada, udini, ukabila, uonevu na uchochezi. Tuache yote na tujenge nchi yetu. Kama ni lawama, matusi, shutuma, udhaifu, mapungufu nk tumeshayataja! Sasa tuseme tunaenda wapi.

Kwa niaba ya Raisi nachukua maamuzi yafuatayo;

1.Najiuzulu wadhifa wangu wa u-Raisi, ukuu wa majeshi na uenyekiti wa chama!

2.WanaJF waunde serikali kutoka miongoni mwao wanayoiona ina uwezo wa kutatua matatizo ya wananchi. Mawaziri hao watoe mipango kazi yao ya nini kifanyike na kifanyike vipi ili kuokoa taifa.

Mpaka sasa najua matatizo ambayo WanaJF wanayaona na kuyasema sana dhidi ya Serikali yangu, Ufisadi, Rushwa, Elimu, Ajira, Afya, Matumizi mabaya ya ofisi, Umeme, Miundombinu, Mfumuko wa bei, Ujambazi, Unyanyasaji wa kijinsia, Mauaji ya Albino, Mauaji ya Wazee, Malipo ya Wazee wa East Africa, Malipo ya Dowans, Migomo, Matatizo ya Walimu, Madaktari na Wafanyakazi wengine nk! Kwa kweli nakubali ni mengi!

Ni matumaini yangu viongozi wazuri watapatikana kwa mfano, Mzee Mwanakijiji, Waberoya, Mohamed Shossi, Michelle, Birigita, Denyo, Rev Masanilo, Voiceof Reason na wengineo wengi! Kila anayeonekana anafaa atoe mapendekezo ya kina kuhusu wizara yake!

Kelele za kupanda bei ya nishati zibadilike kuwa mapendekezo kuhusu nini kifanyike! Mikataba mibovu yatolewe mapendekezo mikataba hiyo ifanyweje!

WanaJF, forum yenu iwe chimbuko la suluhisho na sio mfereji wa lawama. Sio kwamba msilaumu au msifichue ufisadi bali kama viongozi sasa mtoe solutions kulingana na hali halisi.

Shutuma na lawama zenu zimenisababisha niwarudie niwaombe mnisaidie kuongoza kwani mnaonekana mnao uwezo mkubwa. Nadhani hilo mtaliweza. Semeni bila kuficha nini kifanyike kutatua matatizo hayo mnayoyapigia kelele kila kukicha. Imefika mahali kelele za mlango zinamzuia mwenye nyumba kulala! Sipati usingizi!


Asante kwa kunipa cheo cha uwaziri! umenikumbusha mbali sana!

Haya ndiyo nitaanza nayo kama waziri wa mambo ya ndani au related ministry

1. Kwanza jukumu langu kubwa ni kurudisha uzalendo wa nchi hii, Uzalendo kwa kiasi kikubwa una sababisha kila kitu kunyooka, madaktari, mainjinia, polisi, viongozi,wanafunzi kama wana uzalendo wa kutosha..hata kama nchi itapitia hali ngumu ya ki-uchumi due to external factors still uzalendo utalibeba taifa. Kwangu mimi ili kujenga taifa jipya la TANZANIA basi uzalendo uhamasishwe kwanza kwa
a) kufundisha elimu ya uraia, matamasha, miziki, filamu, seminars, etc
b)kujikumbusha historia ya nchi yetu na ni nini viongozi w mwanzo walifanya na leo tunafaidi
c) kutoa matuzo, kwa innovators, wajasiriamali, watu waliofanya mambo ya kutukuka nchi hii, etc
d)etc...I mean so many techniques ambazo zitarudisha uzalendo wa wananchi kwa taifa lao

pia nitalenga kuhamasisha kujiondoa kwenye tabia mbaya kama...kuchangia harusi sana badala ya elimu.....,

Kuhamasisha vijana, wafanyakazi kujitolea kufundisha mashuleni, kama shule za kata n.k volunteering in many issues this will manifest level of nationalism..


Ili kwangu mimi kwa Tanzania ya sasa naona nibora kuliko kingine, maana uzalendo HAMNA.....uzalendo ni motivation ya kila kitu kwa taifa!!

2. Kusimamia mabadiliko ya katiba mpya yenye kujenga taifa jipya..... katiba ni chachu na ni engine ya taifa lolote lile najua hili la wizara ya sheria lakini...

3. Nitahakikisha idara za magereza zinawatumia vizuri wafungwa kwa manufaa ya taifa na kuwafundisha elimu za ufundi na kuwawezesha pindi watokapo. Assume kunakuwa na shamba kubwa la kisasa, ambalo wafungwa wanazalisha mali, is far batter kuliko kuwajaza DAR na kufagia nyumba za askari magereza


4. Nitahakikisha kushirikiana na point number moja, uzalendo wa askari unakuwa maradufu, sheria zikisimamiwa kila kitu kitanyooka, rushwa ndogo ndogo zikiondoka kubwa zitatoka wapi, askari watapewa hadhi kama LAPD..au NYPD kazi ya polisi itahitaji vichwa na IT expertise ili wezi wote wa mabenki kupitia IT wanakamatwa, na in short we need best askaris to trouble shoot all problems caused by smarter thieves! Polisi wakiacha rushwa, kila mmoja akafuata sheria kila kitu kitanyooka

5. Kudumisha amani kwa vitendo, kuzuia kwa nguvu mauaji ya albino, vikongwe, kuzuia mauaji ya koo kwa koo uko mara, kabila kwa kabila hasa kwa wafugaji maeneo mengi nchini.

6. KUHAKIKISHA na kuruhusu maandamno yoyote yale kwa watu wa aina yoyote ili mardi hawavunji sheria ya nchi, nitatoa uhuru wa kujieleza na askari wa wizara yangu watatoa support na kulinda maandamano na kuhakikisha yanafikia tamati na kmalizika vyema. uhuru wa kutoa maoni unaleta uwajibikaji wa viongozi!!

7. kuhakikisha wahamiaji haramu wanasakwa na Tz sio shamba la bibi kwa baadhi ya wahamiaji, utoaji wa vibali vya kazi kwa wageni utazingatia uhitaji wa mtu husika, ili kuboresha uzalendo wizara yangu iko tayari kuwaita wataalamu waliko nje kuja kusaidia ujengwaji watanzania mpya!!!

8. Kwa kuwa askari wa wizara yangu wanateseka sana kukaa barabarani due to high traffic, nitahakikisha natoa ushauri wangu wa kitaalamu kwanza kama engineer, pili kama waziri kwa waziri husika wa ujenzi/miundombinu.kuwa DAR esa salaam inahitaji vitu vifuatavyo kupunguza foleni

a) kuboresha huduma za daladala ziweze ku-aacomodate watu wa hadi tofauti, ili kupunguza magari ya watu binafsi

b) kupunguza kodi kwa daladala, kupunguza gharama za mafuta kwa daladala na gharama kuwa juu kwa magari binafsi..ku-discourage matumizi ya magari binafsi

c) kupiga marufuku magari ya watu binafsi kuingia city centre... zijengwe parking kubwa maeneo ya kawe, kimara, aiport, kurasini, etc magari ya watu binafsi yanaishia hapo, kutoka hapo kunakuwa na shuttle za kwapeleka watu cicty centre..( hii ni solution kwa Dsm ya sasa)

d) kuboresha feeder roads zote na kuziwekea traffic lights kwenye junctions,


e) ultimate solution itakuwa kujenga subway najua rais aliyepita Kikwete alisema anataka flyovers, kitaalamu subway zinafaida zaidi kuliko flyovers kwasababu zifuatazo; unaweza kusafirisha sewage/maji machafu, service lines kama umeme, fiber optics etc , gharama za matunzo za subway ni nafuu ukilinganisha na gharama za matunzo za flyovers, pia mji unakuwa hauko polluted sana au kuwa busy unnecessarily!



Kwa sasa ni haya mhesimiwa PM, najua mawaziri wenzangu wana meeengi sana
 
Back
Top Bottom