Kwa muundo huu, tunaua CHASO

Kwa muundo huu, tunaua CHASO

mantegi

Member
Joined
Oct 16, 2012
Posts
27
Reaction score
20
Wanajf wa CHADEMA, juzi niliona waraka wa katibu mkuu wa BAVICHA kamanda, Deogratias Munishi unaoelekeza muundo mpya wa CHASO ngazi ya mkoa . Huu waraka unaelekeza kuwa CHASO mkoa utaongozwa na viongozi watatu ambao ni:

(a) Mratibu wa CHASO Mkoa
(b) Mratibu Msaidizi wa CHASO Mkoa
(C) Mratibu wa uhamasishaji wa CHASO Mkoa.

Ikumbukwe kuwa kuanzia mwaka jana WanaCHASO walipewa maagizo ya kuendelea kutumia rasimu ya katiba ya CHASO ambayo bado inafanyiwa kazi ambapo watatumia muda huo kuangalia kama katiba hiyo inatakidhi haja. Katika rasimu ya katiba ya CHASO ngazi ya Mkoa inaongozwa na viongozi watano kitu ambacho mi naona ni sahihi kutokana na sababu nitakazotaja hapa chini. Nafasi zinazopendekezwa kwenye hiyo rasimu ngazi ya mkoa ni:

(a) Mwenyekiti
(b) Katibu
(c) Katibu Msaidizi
(d) Katibu Mwenezi
(e) Mweka Hazina

Binafsi sikubaliani na pendekezo kwenye huu waraka bali nakubaliana na pendekezo la rasimu ya katiba ya CHASO kwa sababu zifuatazo:

(1) CHASO Mkoa inajumuisha vyuo vingi ambavyo kimsingi Almanac zao hutofautiana kwa mfano, kwa mkoa wa Morogoro Almanac ya tawi la chuo kikuu Mzumbe ni tofauti na vyuo vingine hivyo kama viongozi wa mkoa wapo wachache uendeshaji wa shughuli za mkoa utakuwa mgumu kwani kuna uwezekano mkubwa Viongozi wote wakawa likizo au wakawa nje ya Mkoa kwa shughuli za masomo kama field na n.k

(2) Kwakuwa, vyuo ndani ya Mikoa viko mbalimbali na geographical conditions ni tofauti hivyo ni vyema kuwa na kundi kubwa kidogo la viongozi ili wasaidiane katika utendaji wa shughuli zao ikizingatiwa kwamba tofauti na shughuli za CHASO, wanamajukumu ya kusoma ambayo nayo ni muhimu kwa maslai ya taifa, chama na wao wenyewe.

(3) Kwakuwa, kuwa kiongozi wa CHASO wakati mwingine ni kutangaza vita na uongozi wa chuo hivyo wakati wowote chochote kinaweza kutokea kama kufukuzwa chuo hivyo tukiwa na viongozi wachache ngazi ya mkoa, kama kiongozi akifukuzwa kuna hatari ya kubaki bila kiongozi wa mkoa au akabakia kiongozi mmoja.

(4) Kwa mara nyingi utakuta vyuo ndani ya mkoa vinatofautiana katika muda wa kufunga na kufungua vyuo, hivyo viongozi wakiwa wengi kidogo itasaidia kwani wengine wakiwa likizo au field, waliobaki wanaendeleza mapambano na shughuli zingine.

(5) Kwakuwa maamuzi ya Mkoa yanahitaji busara, ni vyema kuwa na watu wengi kidogo watakaounganisha mawazo pamoja na kupata maamuzi sahihi.

(6) Kama ngazi ya mkoa watabuni miradi yao hawatakuwa na Mtunza Hazina kama tutakuwa na viongozi watatu kwa mujibu wa waraka toka makao makuu BAVICHA.

(7) Ile rasimu ya katiba ina maelezo ya ziada kwa viongozi kama vile kufanya mikutano, vikao na majukumu ya kila kiongozi tofauti na waraka huu.

Hizo ndio sababu zinazonifanya nipendekeze viongozi watano badala ya watatu. Nilikuwa na mpango wa kuandika barua kwenda makao makuu BAVICHA kuelezea haya mawazo yangu lakini kwa kuwa mimi bado mchanga katika siasa na taratibu za chama, nikaona ni vyema nilete hili wazo humu jf ili mnishauri juu ya mawazo hayo na kama kufanya hivyo ni kuhoji mamlaka ya juu au la. Vilevile mnishauri kama kufanya hivyo sitakiuka kanuni na taratibu za chama. Nawasilisha hoja.

NB: Ni kwa ajili ya wanachama wa CHADEMA na wapenda mabadiliko tu, tafadhali.

 
Ni wazo zuri sana kwenye ujenzi wa chama imara kwaajili ya kukamata dola 2015, ila pia ningependekeza wazo hili ulitengeneze vizuri kwenye mfumo wa barua kisha uiwasilishe kwenye uongozi wa chama kama mwanachama mpenda maendeleo ya Chama. Ukombozi unapatikana through michango ya wazalendo mbalimbali wenye mapenzi mema na nchi. PAMOJA TUTAFANIKISHA
 
. Nilikuwa na mpango wa kuandika barua kwenda makao makuu BAVICHA kuelezea haya mawazo yangu lakini kwa kuwa mimi bado mchanga katika siasa na taratibu za chama, nikaona ni vyema nilete hili wazo humu jf ili mnishauri juu ya mawazo hayo na kama kufanya hivyo ni kuhoji mamlaka ya juu au la. Vilevile mnishauri kama kufanya hivyo sitakiuka kanuni na taratibu za chama. Nawasilisha hoja.
NB: Ni kwa ajili ya wanachama wa CHADEMA na wapenda mabadiliko tu, tafadhali.

Nadhani utakisaidia sana chamas chako iwapo mawazo yako haya utayawasilisha huko kwenye chama ili yaweze kufanyiwa kazi kikamilifu. Usiogope uchanga, mawazo kama haya, na ukiweza kuyatetea ndiyo yatakukuza katika siasa. hata hao unaowaona kuwa wamekomaa walianza hivi hivi
 
Msomi wa ngazi ya chuo kikuu lakini bado unaugua ule ugonjwa maarufu kwa watanzania - uoga!

Wazo zuri, ondoa uoga ulifikishe kunakohusika, naamini watalifanyia kazi haraka.
 
Msomi wa ngazi ya chuo kikuu lakini bado unaugua ule ugonjwa maarufu kwa watanzania - uoga!

Wazo zuri, ondoa uoga ulifikishe kunakohusika, naamini watalifanyia kazi haraka.

Wakiwa na ujasiri wa kuhoji si mnawaundia mizengwe na kuwafukuza?! Kwanini wasiwe waoga?!

Mwanachama anakiri mwenyewe kwamba anaogopa kuihoji mamlaka ya juu.

Inasikitisha sana.
 
Hoja nzuri sana kwa maslahi ya Chadema.Bavicha wafanyie kazi.
 
Wakiwa na ujasiri wa kuhoji si mnawaundia mizengwe na kuwafukuza?! Kwanini wasiwe waoga?!

Mwanachama anakiri mwenyewe kwamba anaogopa kuihoji mamlaka ya juu.

Inasikitisha sana.

Sumu unayojaribu kusambaza hapa JF haina madhara hata kwa mmbu au kiroboto!
 
Wazo zuri sana. Sitegemei kuona BAVICHA wanaendeleza uzembe katika kushughulikia maoni hayo ya mdau kuhusu CHASO.
 
Kwa mujibu wa Waraka Na 1 wa Bavicha 2013,utaratibu wa kuunda CHASO ngazi ya Mkoa utakuwa kama ifuatavyo:-
1.>Kila chuo kitakuwa na tawi kama kawaida na kitakuwa na viongozi wake kwa mfumo ambao uko mpaka hivi sasa.
2.>Kila mwenyekiti na katibu wa kila tawi kwenye mkoa husika wataunda kamati ya uratibu ya CHASO ngazi ya mkoa.
3.>Ngazi ya mkoa ya CHASO itaongozwa na viongozi wafuatao.

a.Mratibu wa CHASO Mkoa.
b.Mratibu msaidizi wa CHASO Mkoa.
c.Mratibu wa uhamasishaji wa CHASO Mkoa.

Hivyo kwa mkoa wa Morogoro ambao mleta hoja ameutolea mfano, una matawi 6 ya CHASO,kwa kutumia kipengele na 2 hapo juu kutakuwa na idadi ya waratibu 15 kwa ngazi ya mkoa wa Morogoro ikiwa ni pamoja na wale wa kipengele na 3.

Namuomba mleta hoja ajielekeze vizuri kwenye waraka husika.
 
Hoja nzuri sana kwa maslahi ya Chadema.Bavicha wafanyie kazi.

Kumbe uPo?Najua kiti cha moto.Bado ww kukamatwa kwenye sagga ya Ugaidi.
Najua unaweza kuisaidia polisi Vizuri sana.Pole sana Mkuu kwa kukosa pa kujishikilia.
Naona jina lile linakuja "CHAMA CHA MAUA...."
MOLEMO kwisha habari yenu.Haiwezekani mkawa mnawinda roho za watanzania wenzenu na kukimbilia kwenye media kusema ni jeshi la polisi.
Mungu kawaumbua.Na bado mtatajana wote..Msalimie Msafiri Mtemelwa.
 
Sumu unayojaribu kusambaza hapa JF haina madhara hata kwa mmbu au kiroboto!

Bado wewe kukamatwa.Mmegeuza chama msitu wa kusaka nafsi za waaandishi habari.
NAKUONEA HURUMA SANA,UNAONEKANA KWENYE POST MOJA MOJA KAMA HIVI.
KWISHA HABARI YAKO MWITA MARANYA!
GAIDI
 
Wazo zuri sana. Sitegemei kuona BAVICHA wanaendeleza uzembe katika kushughulikia maoni hayo ya mdau kuhusu CHASO.

Molemo.Mwita maranya.Nicas mtei na Ben Saanane.Kitengo maalumu cha chadema mnao mkana Ludovick wakati mlikuwa manasaidiana kufanya michezo yenu.
Nicas pole sana.
BAVICHA imeshakwisha,Watanzania hawataki tena kusikia chadomo.
Bado ww na Binamu yako kukamatwa
 
Kumbe uPo?Najua kiti cha moto.Bado ww kukamatwa kwenye sagga ya Ugaidi.
Najua unaweza kuisaidia polisi Vizuri sana.Pole sana Mkuu kwa kukosa pa kujishikilia.
Naona jina lile linakuja "CHAMA CHA MAUA...."
MOLEMO kwisha habari yenu.Haiwezekani mkawa mnawinda roho za watanzania wenzenu na kukimbilia kwenye media kusema ni jeshi la polisi.
Mungu kawaumbua.Na bado mtatajana wote..Msalimie Msafiri Mtemelwa.

Sasa mbona mapovu mengi mkuu kwani wewe ndio nani vile hata utoe hakumu si mlisema kama issue iko Mahakamani haina haja ya kuitolea hukumu si mnasema mnafuata utawala bora sasa hii ya kuhukumu Chadema ati ni magaidi imetoka wapi japokuwa huipendi Chadema lakini hebu jaribu kuwa mvumilivu kwani kama utakumbuka mlitoa hukumu kule Arusha lakini ukweli ukajulikana na mkatambaa sasa badala ya kuropoka wakati hata kesi haijasomwa ni bora ulete hoja nyingine nzuri kama za nini kifanyiki ili tupate maji kila kona ya nchi,Elimu bora,Matibabu bora japokuwa wewe utaenda tabiwa India any way hongera kwa hilo.So na jamaa zako marafiki zako,jirani,uliosoma nao je wanapata nini?So mkuu nakupa akiba ya maneno sina kinyongo nawe lakini nasema hivi kama unaona issue imeletwa hapa na hauna mod nayo ipotezee tu tujali muda kaka leta kitu cha maendeleo ya Taifa zima achana na mambo ya kesi ambazo ziko mahakamani ahsante
 
Back
Top Bottom