Kwa mlio kwenye ndoa na wengine karibuni

Kwa mlio kwenye ndoa na wengine karibuni

ustadhijuma

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2015
Posts
3,133
Reaction score
2,117
Wangapi na wangapi wamejenga majumba lkn hawakuyakalia wamekusanya mali lakini hawakuzila na wengine wamezila lakini hawakushiba.

Ulizaliwa na mama yako ewe mwanaadamu huku unalia na watu pembeni yako wakifurahia tendea wema nafsi yako ili utapokufa wewe uwe unafurahi na watu wawe wanakulilia.

Sio umekufa we unalia kwa adhabu na watu,wanakulilia hivi kwa ni lini utaacha mchepuko wako na kurudi kwa mkeo? Je ni wangapi mnahudumia michepuko mnaacha familia zikitaabika? Je mtajibu nini kwa Mola wenu?

Kuanzia sasa uache mchepuko wako rudi kwa mkeo/mmeo.

Tutendeane mema jamani kwenye ndoa uadui haufai
 
hivi kweny michepuko kuna nini mnanitamanisha ebu mtujuze wengine
 
Kazi nzuri sana ndugu,
hongera kwa darasa, tatizo kubwa la wanandoa ni kukosa hofu ya MUNGU tamaa za ibilisi ndio zinazotenda kazi ndani ya wanadamu,

hakika hofu ya MUNGU ikiwa ndani ya mtu basi hata matendo yake yatakua na unyofu kwa ukamilifu,
 
Ameen.......... Eli79 pita huku kuna ujumbe unatuhusu.
 
Last edited by a moderator:
Kazi nzuri sana ndugu,
hongera kwa darasa, tatizo kubwa la wanandoa ni kukosa hofu ya MUNGU tamaa za ibilisi ndio zinazotenda kazi ndani ya wanadamu,

hakika hofu ya MUNGU ikiwa ndani ya mtu basi hata matendo yake yatakua na unyofu kwa ukamilifu,

..tena usiombe kutana na IBIRISI chambia msumeno ndo kabisaa atakuvuruga,....
 
Back
Top Bottom