Kwa mchezo huu, wizi hauishi Tanzania

Mdakuzi mkuu

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
212
720
Katika zoezi la kupiga picha za vitambulisho vya shule, mpiga picha alimwambia mwalimu mkuu kwamba picha moja ni 500 kwa kila mwanafunzi.

Mwalimu Mkuu akawaambia walimu wa darasa kuwa wawaambie wanafunzi walete 1000 kila mmoja wao kwa ajili ya picha. Walimu wa madarasa wakawatangazia wanafunzi kuwa kila mmoja alete 1500 kwa ajili ya picha.

Watoto wakasema kwa mama zao wao kuwa kuna kupiga picha na gharama ni 2000. Mama sasa kwa baba wa familia, "Baby hizi shule za siku hizi kwa kupenda pesa, kuna mchango wa picha 5000 mpenzi wangu mtolee mwanao apate kitambulisho"

Asa namna hii wizi utaisha Tanzania ?
 
Back
Top Bottom