Alkam Alkam
JF-Expert Member
- Jan 7, 2018
- 602
- 509
MANARA ANABAKI KUWA SHUJAA ALIYESHINDIKANA KATIKA UTANI WA JADI.
Niliwahi kuandika siku za karibu Yanga wakitaniwa utani unaoakisi ukweli wanakimbilia kumtusi Mo au Manara. Mnajua ni kwa nini? Wanaamini Mo ndio anaiwezesha Simba kuwepo hapo ilipo na ndio maana inakuwa juu yao.
Na wanaamini mtu aliyewashinda kwa uwezo wao wa kuzusha na kulaghai watu ni Manara. Ikumbukwe Manara alilelewa kwao. Hivyo mbinu zao zote anazijua. Hivyo inakuwa rahisi kwake kujua wapi apige waumie. Si anaujua udhaifu wao?
Nimemsikia Bumburi akiporomosha matusi ya nguoni kama kawaida ya wapuuzi wote walivyo. Ni mpuuzi tu ndio anaweza kufika mahali bila kujali chochote akaamua kuporomosha matusi hadharani hakuna jina lingine zuri la kumwita bali ni Mpuuzi.
Eti amekasirishwa kutaniwa baada ya kunusurika kwenye ajali baada ya tairi ya basi lao kupasuka hivyo alihitaji pole na sio kutaniwa. Utani una mipaka? Kilimjaza Bumburi sio hicho. Kilichomjaza na hasira za kutaniwa kusafirisha timu kwa basi bovu lisilofanyiwa ukarabati mpaka Shinyanga huku wakijinadi timu imehama kwenye umaskini na sasa ina hiduma kama wapatazo Simba. Sasa kauli na vitendo ni tofauti. Na kusafiri na basi huwezi kuficha. Hivyo kutaniwa kwenye hili ndiko kuliko mjaza na akakosa majibu. Akaamua kuwa Mpuuzi.
Manara anajua utani na ndio maana mpaka leo hajawahi kuitwa au kushutumiwa popote kuwa anatakiwa kujibu kauli zake. Zaidi tu ya Wanayanga kumchukia na kusema anaisema timu yao vibaya. Hivi mlitaka Manara aisema Yanga vizuri? Au mlitaka Manara asiitaja Yanga? Si Manara tu hata Mimi nikipata nafasi ya kuikejeli Yanga na kuwashusha thamani nitafanya hivyo.
Niwakumbushe baadha ya utani Yanga waliowahi kuwafanyia Simba na hakuna aliyewahi kuwatukana.
1 Miaka ya 1990 waliwahi kuja na shanga pale Uhuru wakaturushia kwa marundo wakidai Simba tunafuga mashoga na hakuna aliyewatukana bali tuliishia kucheka.
2. Jery Muro aliwahi kusema Yanga ya Manji itainunua Simba na kupeleka wachezaji wake wote wakacheze soka la ufukweni. Hakuna aliyewaporomoshea matusi bali tulicheka tu.
3. Yanga hawa hawa kupitia kifo cha Marehemu Mafisango tena kupitia msemaji wao waliwahi kutuambia tumekula fedha za rambi rambi na hatuwezi kuwa mabingwa mpaka turudishe rambi rambi hakuna aliyepaniki na kuwaporomoshea matusi.
4. Hawa hawa tulipopata ajali tukitokea Dodoma na kumpoteza mpendwa wetu bado walitutania kwamba ajali ile ilisababishwa na matunguri tuliyobeba na tumemtoa kafara ili tutwae kombe la Fa. Hakuna aliyewaporomoshea matusi.
Kinachowauma Yanga wote sio ajali ni kutaniwa mambo yanayoakisi ukweli na wanaona kabisa washazidiwa mno na hawana majibu hivyo wanakimbilia kwenye matusi. Ni kawaida ya mtu yeyote dhaifu akiidhiwa hoja hukimbilia kwenye matusi.
Kwa hili Bumbuli amejidhalilisha, ameidhalilisha klabu yake na amedhalilisha mashabiki wote wa soka nchini. Anatakiwa ajitafakari kama kweli ana wazazi na amelelewa katika maadili ya kitanzania. Au ni mtu wa aina fulani ila huwa anafanikiwa kuficha tabia zake halisi na sasa ameoneka Bumburi halisi na sura yake ndio hiyo.
Vyovyote iwavyo na kwa namma yoyote hakuna namna yoyote ya kuhalalisha matusi ila lugha nzuri ya mtukanaji daima ni PUNGUANI NA MPUUZI.
Niliwahi kuandika siku za karibu Yanga wakitaniwa utani unaoakisi ukweli wanakimbilia kumtusi Mo au Manara. Mnajua ni kwa nini? Wanaamini Mo ndio anaiwezesha Simba kuwepo hapo ilipo na ndio maana inakuwa juu yao.
Na wanaamini mtu aliyewashinda kwa uwezo wao wa kuzusha na kulaghai watu ni Manara. Ikumbukwe Manara alilelewa kwao. Hivyo mbinu zao zote anazijua. Hivyo inakuwa rahisi kwake kujua wapi apige waumie. Si anaujua udhaifu wao?
Nimemsikia Bumburi akiporomosha matusi ya nguoni kama kawaida ya wapuuzi wote walivyo. Ni mpuuzi tu ndio anaweza kufika mahali bila kujali chochote akaamua kuporomosha matusi hadharani hakuna jina lingine zuri la kumwita bali ni Mpuuzi.
Eti amekasirishwa kutaniwa baada ya kunusurika kwenye ajali baada ya tairi ya basi lao kupasuka hivyo alihitaji pole na sio kutaniwa. Utani una mipaka? Kilimjaza Bumburi sio hicho. Kilichomjaza na hasira za kutaniwa kusafirisha timu kwa basi bovu lisilofanyiwa ukarabati mpaka Shinyanga huku wakijinadi timu imehama kwenye umaskini na sasa ina hiduma kama wapatazo Simba. Sasa kauli na vitendo ni tofauti. Na kusafiri na basi huwezi kuficha. Hivyo kutaniwa kwenye hili ndiko kuliko mjaza na akakosa majibu. Akaamua kuwa Mpuuzi.
Manara anajua utani na ndio maana mpaka leo hajawahi kuitwa au kushutumiwa popote kuwa anatakiwa kujibu kauli zake. Zaidi tu ya Wanayanga kumchukia na kusema anaisema timu yao vibaya. Hivi mlitaka Manara aisema Yanga vizuri? Au mlitaka Manara asiitaja Yanga? Si Manara tu hata Mimi nikipata nafasi ya kuikejeli Yanga na kuwashusha thamani nitafanya hivyo.
Niwakumbushe baadha ya utani Yanga waliowahi kuwafanyia Simba na hakuna aliyewahi kuwatukana.
1 Miaka ya 1990 waliwahi kuja na shanga pale Uhuru wakaturushia kwa marundo wakidai Simba tunafuga mashoga na hakuna aliyewatukana bali tuliishia kucheka.
2. Jery Muro aliwahi kusema Yanga ya Manji itainunua Simba na kupeleka wachezaji wake wote wakacheze soka la ufukweni. Hakuna aliyewaporomoshea matusi bali tulicheka tu.
3. Yanga hawa hawa kupitia kifo cha Marehemu Mafisango tena kupitia msemaji wao waliwahi kutuambia tumekula fedha za rambi rambi na hatuwezi kuwa mabingwa mpaka turudishe rambi rambi hakuna aliyepaniki na kuwaporomoshea matusi.
4. Hawa hawa tulipopata ajali tukitokea Dodoma na kumpoteza mpendwa wetu bado walitutania kwamba ajali ile ilisababishwa na matunguri tuliyobeba na tumemtoa kafara ili tutwae kombe la Fa. Hakuna aliyewaporomoshea matusi.
Kinachowauma Yanga wote sio ajali ni kutaniwa mambo yanayoakisi ukweli na wanaona kabisa washazidiwa mno na hawana majibu hivyo wanakimbilia kwenye matusi. Ni kawaida ya mtu yeyote dhaifu akiidhiwa hoja hukimbilia kwenye matusi.
Kwa hili Bumbuli amejidhalilisha, ameidhalilisha klabu yake na amedhalilisha mashabiki wote wa soka nchini. Anatakiwa ajitafakari kama kweli ana wazazi na amelelewa katika maadili ya kitanzania. Au ni mtu wa aina fulani ila huwa anafanikiwa kuficha tabia zake halisi na sasa ameoneka Bumburi halisi na sura yake ndio hiyo.
Vyovyote iwavyo na kwa namma yoyote hakuna namna yoyote ya kuhalalisha matusi ila lugha nzuri ya mtukanaji daima ni PUNGUANI NA MPUUZI.