Kwa malezi haya, ndoa nyingi zitaendelea kuvunjika!

Nyalotsi

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
6,978
5,025
Kuna ndugu yangu wa kike 18 miaka, anasoma chuo karibu na ninapoishi. Yeye anaishi kwa mama yake mdogo mbali na chuo. Nilimkaribisha awe anakuja mchana anapika na kula kwangu ili kupunguza gharama za kununua chakula na ufunguo nikampatia. Chakula chote nanua naweka ndani ikijumuishwa na mboga huwa naipika na kuhifadhi kwenye kafriji kangu. Tatizo sasa, atakuja atapika na kula na vyombo anaviacha vichafu. Nikirudi kutoka kazini naviosha. Kuna siku nilisafiri na niliporudi nikaona vyombo vyote vichafu na nikaviosha. Siku moja nikamueleza kistaarabu awe anaosha vyombo anavyovitumia. Kuanzia siku hiyo hajakanyaga tena kwangu. Ninajiuliza, kumsisitiza usafi ni kosa? Hili mara nyingi linajitokeza hata kwenye ndoa kutokana na watu kushindwa kufanya vitu vidogo kama kuosha vyombo, kupika, kutandika kitanda, kupiga deki nk na kupelekea ndoa kuwa na migogoro. Wito wangu kwenu wazazi: wafundisheni watoto wenu wazijue kazi ndogo ndogo hata kama wanasoma boarding! Wakirudi likizo wajifunze hata kuosha vyombo na kufua.
 
Kweli kabisa ulichosema watoto wa sikuhizi kazi hawafanyi wanasema Ni digitali
 
Kuna family moja naijua mwanaume ana maweee wife ni kimeo nyumba yao nzuri wife kaishaifanya km banda la kuku,haelewekii,alikuwa mvivu tangu alipokuwa binti ,walijua ataacha
 
Back
Top Bottom