wakukurupuka1
JF-Expert Member
- Feb 17, 2023
- 525
- 1,187
IT, hili neno linaweza kuwa na maana nyingi lakini hapa nataka kumaanisha IN TRANSIT kwa maana ya zile gari zinazopelekwa nchi za jirani kupitia bandari yetu ya Dar es salaam nk.
Hizi gari zimekuwa moja ya usafiri wa tuliowengi pale tunapopata safari za dharura kwenda makwetu, huwa zinatusaidia sana japo wengi wetu hatujajua hatari yake.
Bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye point kuwa baadhi ya hizi gari au usafiri huu ni moja kati ya vyanzo VIZURI vya ajali za barabarani na hasa nyakati za usiku na askari hawatangazi sana matukio ya ajali za hizo gari kwani zinakuwa zimepita kwenye check points wanazozisimami.
Iko hivi, utakuta dereva au madereva hao baadhi (natumia neno baadhi kwa makusudi ili kuepuka kushambuliwa) huwa wanapata tenda hiyo let say kupeleka hizo gari kwenye exit points kwa maana ya mipakani, sasa ukute madereva wa 3 wamepata tenda ya kupeleka gari kumi au kumi na tano hivi pengine zaidi au pungufu, wanachofanya wanazitoa hizo gari wanazipaki majali hapa hapa tuseme Dar wanachukua mbili au tatu kulingana na idadi yao wanaanza kuzikimbiza kwenda nazo mpakani let say Tunduma Kasumulu Rusumo nk.
Na mara nyingi huwa wanapenda kusafiri nyakati za usiku kukwepa askari na tochi za mchana, na lengo lao kwa mfano wakienda Tunduma wana target wafike asubuhi kunapambazuka halafu waache hizo gari wadandie usafiri mwingine tena wa kurudi Dar waje wachukue gari nyingine tena hivyo mpaka wamalize, ili mradi tu wapate pesa nyingi, lakini ujiulize hivi dereva wa namna hiyo akipata ajali pengine kutokana na uchovu wa safari za mfululizo atasema ajali hazina kinga!?
Kama haitoshi madereva hawa baadhi yao huwa wanapenda sana kutumia vinywaji fulani kama enejaiza au booster wenyewe wanaita ,je kuna usalama kweli hapo, lakini kama haitoshi baadhi ya madereva wa hizo IT ni wale ambao hawana UZOEFU wa kutosha hata kidogo its ok ndo wanaanza kupata UZOEFU lakini ilitakiwa wawe chini ya usimamizi wa wenye uzoefu.
Hizi IT zinasababisha sana ajali lakini polisi au hata niseme serikali kama vile hawalioni wao wanangoja tu kutangaza matokeo, utasikia uzembe wa dereva, MWENDO KASI, KUTAKA KULIPITA GARI LINGINE BILA KUCHUKUA TAHADHARI na mengi ya namna hiyo.
Askari wa usalama barabarani anaweza asione kitu chochote lakini sio gari la IT, hata liwe mbali kiasi gani na liwe na rangi ya aina gani atalitambua tu maana akishaiona tu IT anajua chambichambi tayari.
Wito wangu, tujitahidi kubaini vyanzo vya ajali badala ya kusubiri tutangaze matokeo, kwanini pasiwe na utaratibu kuwa it zote zitengewe siku ya kusafirishwa mfano inaweza kuwa mara mbili au mara tatu kwa wiki na kwa kuripoti kwenye check points maalumu na kwa muda maalum,kwa kifupi lazima ziwe controlled ,ziwe na muda wa kusafiri kutoka point moja hadi nyingine na si vinginevyo, nawaza tu.
Angalizo: Baadhi ya IT
Onyo: Unayetumia IT kama usafiri wa kuaminika hukatazwi lakini kuwa makini
Credit: Thomas Mwamfupe
Hizi gari zimekuwa moja ya usafiri wa tuliowengi pale tunapopata safari za dharura kwenda makwetu, huwa zinatusaidia sana japo wengi wetu hatujajua hatari yake.
Bila kupoteza muda niende moja kwa moja kwenye point kuwa baadhi ya hizi gari au usafiri huu ni moja kati ya vyanzo VIZURI vya ajali za barabarani na hasa nyakati za usiku na askari hawatangazi sana matukio ya ajali za hizo gari kwani zinakuwa zimepita kwenye check points wanazozisimami.
Iko hivi, utakuta dereva au madereva hao baadhi (natumia neno baadhi kwa makusudi ili kuepuka kushambuliwa) huwa wanapata tenda hiyo let say kupeleka hizo gari kwenye exit points kwa maana ya mipakani, sasa ukute madereva wa 3 wamepata tenda ya kupeleka gari kumi au kumi na tano hivi pengine zaidi au pungufu, wanachofanya wanazitoa hizo gari wanazipaki majali hapa hapa tuseme Dar wanachukua mbili au tatu kulingana na idadi yao wanaanza kuzikimbiza kwenda nazo mpakani let say Tunduma Kasumulu Rusumo nk.
Na mara nyingi huwa wanapenda kusafiri nyakati za usiku kukwepa askari na tochi za mchana, na lengo lao kwa mfano wakienda Tunduma wana target wafike asubuhi kunapambazuka halafu waache hizo gari wadandie usafiri mwingine tena wa kurudi Dar waje wachukue gari nyingine tena hivyo mpaka wamalize, ili mradi tu wapate pesa nyingi, lakini ujiulize hivi dereva wa namna hiyo akipata ajali pengine kutokana na uchovu wa safari za mfululizo atasema ajali hazina kinga!?
Kama haitoshi madereva hawa baadhi yao huwa wanapenda sana kutumia vinywaji fulani kama enejaiza au booster wenyewe wanaita ,je kuna usalama kweli hapo, lakini kama haitoshi baadhi ya madereva wa hizo IT ni wale ambao hawana UZOEFU wa kutosha hata kidogo its ok ndo wanaanza kupata UZOEFU lakini ilitakiwa wawe chini ya usimamizi wa wenye uzoefu.
Hizi IT zinasababisha sana ajali lakini polisi au hata niseme serikali kama vile hawalioni wao wanangoja tu kutangaza matokeo, utasikia uzembe wa dereva, MWENDO KASI, KUTAKA KULIPITA GARI LINGINE BILA KUCHUKUA TAHADHARI na mengi ya namna hiyo.
Askari wa usalama barabarani anaweza asione kitu chochote lakini sio gari la IT, hata liwe mbali kiasi gani na liwe na rangi ya aina gani atalitambua tu maana akishaiona tu IT anajua chambichambi tayari.
Wito wangu, tujitahidi kubaini vyanzo vya ajali badala ya kusubiri tutangaze matokeo, kwanini pasiwe na utaratibu kuwa it zote zitengewe siku ya kusafirishwa mfano inaweza kuwa mara mbili au mara tatu kwa wiki na kwa kuripoti kwenye check points maalumu na kwa muda maalum,kwa kifupi lazima ziwe controlled ,ziwe na muda wa kusafiri kutoka point moja hadi nyingine na si vinginevyo, nawaza tu.
Angalizo: Baadhi ya IT
Onyo: Unayetumia IT kama usafiri wa kuaminika hukatazwi lakini kuwa makini
Credit: Thomas Mwamfupe