Kwa kuchezea demokrasia, tutegemee mbinyo, safari hii hata leso zitafuliwa

Nkobe

JF-Expert Member
Feb 17, 2013
2,162
3,162
Wako Watanzania wasiojua uhalisia

Tanzania kama nchi inaelekea kuwa na watu milioni 50. Kati ya hao, walipa kodi hawafiki hata milioni tatu, yaani kundi la watu milioni tatu ndilo linaendesha maisha ya watu milioni 50 kwa afya, miundombinu, maji nk. Maana Watanzania wengi ni walima mihogo na mahindi ya kujikimu, hawana pa kuwakamata ili walipe kodi. Kundi lingine ni vijana jobless waliomaliza vyuo vikuu, sekondari na Shule za msingi, hawalipi kodi zaidi ya kuwapiga vibomu ndugu zao wawape hata nauli.

Kwa misingi hiyo, ni ujinga kusema eti msaada wa mzungu hauhitajiki, unahitajika sana, ndio tuko na maliasili, utalii, lakini vyote hivi vime prove kuwa bado havijafika level ya ku support budget kwa 100%. Kwa kifupi, kujitegenea bila viwanda tunajidanganya.

Kwa kusema hayo, kigezo kikuu cha mzungu kutoa msaada ni demokrasia, ndio hivyo sasa kuanzia mwenyekiti wa kitongoji hadi wabunge, kwa fitina za kila namna wamehakikisha ni ccm wote. Hivyo, Inaelekea Wapinzani watawaandikia umoja wa Ulaya, Marekani kuhusu hali ya kidemokrasia nchini.

Tena wataandika huku wakiweka vielelezo vya mabox fake ya kura, damu za watu nk.

Hivyo, hali itakuwa mbaya kwa wafanyabiashara, wafanyakazi maana mzunguko wa pesa hautakuwepo. Tutegemee mbinyo ambao haukuwahi kutokea, Tutegemee anguko la thamani ya pesa nk.
 
Wabongo bhana, yaani mnaamini kabisa Muzungu anajali kama kuna demokrasia TZ au hakuna? Inaelekea mnaamini kabisa Muzungu anakosa usingizi sababu ya Zito Kabwe au tundu?

Low IQ!
 
wameamua ƙuchoma ƙitanɗa wanacho lalia ili ƙuua kunguni itawacost
Bro this time nilijiandaa kisaikolojia hasa baada ya siku ya kwanza kuona mabox yanakamatwa...sijajisumbua kufuatilia matokeo.
Niwahakikishie majambazi wa ccm wote humu na nje ya humu kuwa wamejiletea mikosi.
Wananchi wametimiza majukumu yao ya kupiga kura wao wamepindua meza.
Hakila laana i juu yao sisi tutapeta tu waliwake jua au inyeshe mambo yataenda.
Hata mbinyo utokee sitaogopa nitatoboa bila hofu.

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Wabongo bhana, yaani mnaamini kabisa Muzungu anajali kama kuna demokrasia TZ au hakuna? Inaelekea mnaamini kabisa Muzungu anakosa usingizi sababu ya Zito Kabwe au tundu?

Low IQ!
Hivi ndugu mwenye IQ kubwa, TRA, TASAF, NSSF kwa kutaja kwa uchache, vilianzishwa kwa mawazo ya wabongo, au maelekezo kutoka kwa wafadhili?
 
Wako Watanzania wasiojua uhalisia

Tanzania kama nchi inaelekea kuwa na watu milioni 50. Kati ya hao, walipa kodi hawafiki hata milioni tatu, yaani kundi la watu milioni tatu ndilo linaendesha maisha ya watu milioni 50 kwa afya, miundombinu, maji nk. Maana Watanzania wengi ni walima mihogo na mahindi ya kujikimu, hawana pa kuwakamata ili walipe kodi. Kundi lingine ni vijana jobless waliomaliza vyuo vikuu, sekondari na Shule za msingi, hawalipi kodi zaidi ya kuwapiga vibomu ndugu zao wawape hata nauli.

Kwa misingi hiyo, ni ujinga kusema eti msaada wa mzungu hauhitajiki, unahitajika sana, ndio tuko na maliasili, utalii, lakini vyote hivi vime prove kuwa bado havijafika level ya ku support budget kwa 100%. Kwa kifupi, kujitegenea bila viwanda tunajidanganya.

Kwa kusema hayo, kigezo kikuu cha mzungu kutoa msaada ni demokrasia, ndio hivyo sasa kuanzia mwenyekiti wa kitongoji hadi wabunge, kwa fitina za kila namna wamehakikisha ni ccm wote. Hivyo, Inaelekea Wapinzani watawaandikia umoja wa Ulaya, Marekani kuhusu hali ya kidemokrasia nchini.

Tena wataandika huku wakiweka vielelezo vya mabox fake ya kura, damu za watu nk.

Hivyo, hali itakuwa mbaya kwa wafanyabiashara, wafanyakazi maana mzunguko wa pesa hautakuwepo. Tutegemee mbinyo ambao haukuwahi kutokea, Tutegemee anguko la thamani ya pesa nk.
Tunarlekea milioni 60 Chief! Sio 50
 
Wabongo bhana, yaani mnaamini kabisa Muzungu anajali kama kuna demokrasia TZ au hakuna? Inaelekea mnaamini kabisa Muzungu anakosa usingizi sababu ya Zito Kabwe au tundu?

Low IQ!hu

Wabongo bhana, yaani mnaamini kabisa Muzungu anajali kama kuna demokrasia TZ au hakuna? Inaelekea mnaamini kabisa Muzungu anakosa usingizi sababu ya Zito Kabwe au tundu?

Low IQ!
Sawa kabisa, muda utasema
 
Back
Top Bottom