MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,252
- 8,003
Yaani mikutano ya Chama inafanyikia ikulu watu wako kimya?? Hakuna anayehoji kitu hata mmoja??hakuna hata kunyoosha kidole au kukemea? Huu uoga umeanza lini? Hiki kitu kinashangaza sana na kinaumiza mno!!! Tena katika mfumo ambao kila chama kina haki ya kwenda ikulu endapo kikapewa ridhaa na wanamchi.
Kwa uelewa Wangu mimi wa elimu ya hapa na pale katika sharia ni kwamba Ikulu ni kama nyumba taifa! Ikulu haijawa nyumba ya kufanyia shughuli za kichama!! Huu ni mwiko! Kwanini miiko ya kitaifa inavunjwa kiasi hiki?
Kama watu wanatumia Ikulu kufanyia shughuli za chama watashindwaje kuchota pesa benki kuu kwa matumizi ya shughuli za chama? Kunatofauti gani kutumia Ikulu kwa shughuli za Chama na kutumia pesa za walipa kodi zilizopo benki kuu kendesha shughuli za chama?
Kwahiyo CHADEMA, CUF,NCCR,ACT,TLP na vyama vingine navyo vinanavyo wajibu wa kutumia Ikulu kwa shughuli za vyama vyao endapo wakihitaji? Hili ndio mara ya kwanza linatokea Tanzania tu! Sidhani kama hayati Baba wa taifa angalikua hai angekubaliana na vitendo hivi.
Hivi itokee Mwenyekiti Wangu wa wataa wa hapa Sanaware akaita wanachama wenzake kama walikua na mkutano wa kichama wafanyie kwenye ofisi ya serikali tena wakavaa na sare zao hali itakuaje? Wananchi walichukuliaje hilo tukio ikiwa ni ngazi ya mtaa tu? Siasa za mtaa huu zitatafsiriwa vipi?
Kwa hili ninawashangaa wapinzani wa nchi hii kikaa kimya, inamaana wao wanaona sawa? Wapinzani Mara nyingi hubeba sauti za wananchi lakini kwa ukimya huu wanakatisha tamaa wanamchi.
Kwa uelewa Wangu mimi wa elimu ya hapa na pale katika sharia ni kwamba Ikulu ni kama nyumba taifa! Ikulu haijawa nyumba ya kufanyia shughuli za kichama!! Huu ni mwiko! Kwanini miiko ya kitaifa inavunjwa kiasi hiki?
Kama watu wanatumia Ikulu kufanyia shughuli za chama watashindwaje kuchota pesa benki kuu kwa matumizi ya shughuli za chama? Kunatofauti gani kutumia Ikulu kwa shughuli za Chama na kutumia pesa za walipa kodi zilizopo benki kuu kendesha shughuli za chama?
Kwahiyo CHADEMA, CUF,NCCR,ACT,TLP na vyama vingine navyo vinanavyo wajibu wa kutumia Ikulu kwa shughuli za vyama vyao endapo wakihitaji? Hili ndio mara ya kwanza linatokea Tanzania tu! Sidhani kama hayati Baba wa taifa angalikua hai angekubaliana na vitendo hivi.
Hivi itokee Mwenyekiti Wangu wa wataa wa hapa Sanaware akaita wanachama wenzake kama walikua na mkutano wa kichama wafanyie kwenye ofisi ya serikali tena wakavaa na sare zao hali itakuaje? Wananchi walichukuliaje hilo tukio ikiwa ni ngazi ya mtaa tu? Siasa za mtaa huu zitatafsiriwa vipi?
Kwa hili ninawashangaa wapinzani wa nchi hii kikaa kimya, inamaana wao wanaona sawa? Wapinzani Mara nyingi hubeba sauti za wananchi lakini kwa ukimya huu wanakatisha tamaa wanamchi.