ligendayika
JF-Expert Member
- Aug 31, 2012
- 1,183
- 198
Jana katika michezo ya ITV niliwasikia viongozi wa African Lyon wakilalamikia maamuzi ya TFF ya kuzuia udhamini wao na ZANTEL kampuni mojawapo ya simu nchini. Kwa hili tenha hajautendea haki mpira wa Tanzania yeye kama kiongozi alitakiwa kuwaka mipango mizuri ya maendeleo ya soka ikiwemo kuzuia mikataba ambayo haina lengo la kuendeleza Soka nchini kama huu wa Vodacom. Nakushauri Tenga pitia ligi za duniani na afrika utaona kampuni zinazofanan zinadhamini ligi moja mfano Congo DRC vodacom wapo na tigo,England Baclays na Standard chartered bank. Je Tenga ana maslahi mengine ndani ya Vodacom tofauti na maendeleo ya soka tunataka ushindani ktk udhamini wa soka Tanzania ili kupandisha kiwango cha soka nchini. Naomba kuwasilisha tuchangie.