Kwa hili TENGA SIKUUNGI MKONO

ligendayika

JF-Expert Member
Aug 31, 2012
1,183
198
Jana katika michezo ya ITV niliwasikia viongozi wa African Lyon wakilalamikia maamuzi ya TFF ya kuzuia udhamini wao na ZANTEL kampuni mojawapo ya simu nchini. Kwa hili tenha hajautendea haki mpira wa Tanzania yeye kama kiongozi alitakiwa kuwaka mipango mizuri ya maendeleo ya soka ikiwemo kuzuia mikataba ambayo haina lengo la kuendeleza Soka nchini kama huu wa Vodacom. Nakushauri Tenga pitia ligi za duniani na afrika utaona kampuni zinazofanan zinadhamini ligi moja mfano Congo DRC vodacom wapo na tigo,England Baclays na Standard chartered bank. Je Tenga ana maslahi mengine ndani ya Vodacom tofauti na maendeleo ya soka tunataka ushindani ktk udhamini wa soka Tanzania ili kupandisha kiwango cha soka nchini. Naomba kuwasilisha tuchangie.
 
Ni kweli uyasemayo ina wezekana tenga ana maslahi zaidi na voda achilia mbali udhamini badala kusaidia klabu yeye anakandamiza ajiulize huo udhamini wa voda unatosheleza vilabu
 
Mkuu mimi nimshabiki sana sana wa Mnyama kifupi soka la tanganyika lakini soka letu linapelekwa pelwkwa tu kihuni huni imradi liende na watu wamejaa unazi wa kijinga hata kwenye mambo ambaayo haya hitaji unazi wa kisenge, Tenga amalize mda wake awapishe wengine nao wajaribu angalia swala na Michael wambura kuzuiliwa asigombe, angalia swala la usali wa wachezaji utaona utumbo mwanzo mwisho...huko mikoani ndiyo usiseme....
 
Tatizo letu wabonngo ni kusaini mikataba mbalimbali bila ya kuisoma vizuri.yawezekana kabisa mkataba wa voda ulikua hautoi mwanya kwa tim kuingia mkataba na kampuni nyingine kakini kutokana na njaa ilivyoibana vilabu vyetu hujikuta wanasain bila umakini. Sii michezo tu hata mikataba ya mikopo nk hua na mitego ambayo watu huiingia bila kujijua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom