Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
KWA HILI STANBIC BANK WAOMBE RADHI
Niko Mbali na mjini , Njia yangu rahisi zaidi ya kuchukuwa pesa kutoka kwenye benki ninayohifadhi pesa zangu ni kwa kutumia Kadi za ATM , ambapo inaniruhusu kutumia ATM za benki nyingine kama zao zinakuwa hazina pesa au sehemu hiyo hakuna mashine za ATM zao ndivyo ninavyofanya kazi kila wakati kwa sababu niko nje ya mji - wengine ni kutokana na kazi zao na vitu vingine uharaka na nini wanatumia hizi mashine za ATM kwa ajili ya kuchukuwa pesa zao .
Sasa toka jana saa 6 mchana benki inayohifadhi pesa zangu STANBIC imekuwa na tatizo kwenye utoaji pesa kwenye mashine za ATM mpaka kwenye teller zao ndani ya benki zao karibu zote nchini hata unapotumia ATM kadi hii kwa ajili ya kujichukulie pesa kutumia mashine za benki zingine napo hazifanyi kazi .
Leo imeingia siku ya pili sijapata taarifa yoyote kutoka kwa STANBIC ya kimaandishi au hata ya maneno , wakati najisajili kwenye huduma zao niliwapa Barua pepe zangu 3 zote zinazofanya kazi , nikawapa mpaka namba zangu za simu 2 zote ambazo ziko hewani masaa 24 hata nikiwa nje ya nchi zote huwa zinafanya kazi .
Nakuambia leo ni siku ya pili na sasa ni saa 7 mchana huduma za kibenki kwenye benki ya STANBIC bado hazijarudi kawaida zaidi ya masaa 24 haya , wengi wamepata hasara kwa kupotezewa muda wao na hata kupoteza wateja kama watu hao walikuwa wanataka kutoa pesa kwa ajili ya kuendesha biashara zao mbali mbali .
Namba zetu za simu wanazo wanashindwa kutupa taarifa hata kwa sms tu , kwani sms 1 ni bei gani kumtaarifu tu mteja kwamba kwa sasa kuna tatizo na tutarekebisha baada ya muda fulani ? hiyo inaweza kuwa gharama lakini email zetu wanazo kwanini hata wasitutumie basi email kutupa taarifa badala ya kutumia email hizo kututumia matangazo ya biashara ?
Huu sio uungwana hata kidogo wanatumia amani tuliyokuwa nayo na utulivu kudhubutu kufanya mambo kama haya kama vile hakuna hata mmoja atakayenyoosha kidole kuuliza au kuwafokea , wanafikiri watu wote ni mbumbumbu wameridhika kwahiyo watakaa kimya tu bila kufanya chochote .
Nimepotezewa muda wangu na nimepata hasara sana kwa haya masaa 24 ambapo benki haifanyi kazi nashindwa kufanya shuguli zingine zinazonilazimu kutumia hela yangu ambayo nimehifadhi kwenye benki yao kwa maarifa yangu mwenyewe , leo sipewi taarifa na wala sina haki ya kupata taarifa hizo
Nimeangalia kwenye vyombo vyote vya habari , mpaka kwenye magazeti mpaka kwenye tovuti mbalimbali hata ya benki hiyo hakuna taarifa zozote za tatizo hili zaidi ya masaa 24 sasa .
Nauomba Uongozi wa benki hii utoe taarifa rasmi kwa ummah na kuomba msamaha kwa wateja wao wote ambao wamesumbuliwa na tatizo hili kwa namna moja au nyingine , na wasimamizi wa mabanki haya kama ni benki kuu au taasisi zingine ziwabane waendeshaji wa benki hizi kuhusu viwango vyao vya utoaji huduma na mawasiliano yao mengine waliyokuwa nayo kwa wateja wao .
Niko Mbali na mjini , Njia yangu rahisi zaidi ya kuchukuwa pesa kutoka kwenye benki ninayohifadhi pesa zangu ni kwa kutumia Kadi za ATM , ambapo inaniruhusu kutumia ATM za benki nyingine kama zao zinakuwa hazina pesa au sehemu hiyo hakuna mashine za ATM zao ndivyo ninavyofanya kazi kila wakati kwa sababu niko nje ya mji - wengine ni kutokana na kazi zao na vitu vingine uharaka na nini wanatumia hizi mashine za ATM kwa ajili ya kuchukuwa pesa zao .
Sasa toka jana saa 6 mchana benki inayohifadhi pesa zangu STANBIC imekuwa na tatizo kwenye utoaji pesa kwenye mashine za ATM mpaka kwenye teller zao ndani ya benki zao karibu zote nchini hata unapotumia ATM kadi hii kwa ajili ya kujichukulie pesa kutumia mashine za benki zingine napo hazifanyi kazi .
Leo imeingia siku ya pili sijapata taarifa yoyote kutoka kwa STANBIC ya kimaandishi au hata ya maneno , wakati najisajili kwenye huduma zao niliwapa Barua pepe zangu 3 zote zinazofanya kazi , nikawapa mpaka namba zangu za simu 2 zote ambazo ziko hewani masaa 24 hata nikiwa nje ya nchi zote huwa zinafanya kazi .
Nakuambia leo ni siku ya pili na sasa ni saa 7 mchana huduma za kibenki kwenye benki ya STANBIC bado hazijarudi kawaida zaidi ya masaa 24 haya , wengi wamepata hasara kwa kupotezewa muda wao na hata kupoteza wateja kama watu hao walikuwa wanataka kutoa pesa kwa ajili ya kuendesha biashara zao mbali mbali .
Namba zetu za simu wanazo wanashindwa kutupa taarifa hata kwa sms tu , kwani sms 1 ni bei gani kumtaarifu tu mteja kwamba kwa sasa kuna tatizo na tutarekebisha baada ya muda fulani ? hiyo inaweza kuwa gharama lakini email zetu wanazo kwanini hata wasitutumie basi email kutupa taarifa badala ya kutumia email hizo kututumia matangazo ya biashara ?
Huu sio uungwana hata kidogo wanatumia amani tuliyokuwa nayo na utulivu kudhubutu kufanya mambo kama haya kama vile hakuna hata mmoja atakayenyoosha kidole kuuliza au kuwafokea , wanafikiri watu wote ni mbumbumbu wameridhika kwahiyo watakaa kimya tu bila kufanya chochote .
Nimepotezewa muda wangu na nimepata hasara sana kwa haya masaa 24 ambapo benki haifanyi kazi nashindwa kufanya shuguli zingine zinazonilazimu kutumia hela yangu ambayo nimehifadhi kwenye benki yao kwa maarifa yangu mwenyewe , leo sipewi taarifa na wala sina haki ya kupata taarifa hizo
Nimeangalia kwenye vyombo vyote vya habari , mpaka kwenye magazeti mpaka kwenye tovuti mbalimbali hata ya benki hiyo hakuna taarifa zozote za tatizo hili zaidi ya masaa 24 sasa .
Nauomba Uongozi wa benki hii utoe taarifa rasmi kwa ummah na kuomba msamaha kwa wateja wao wote ambao wamesumbuliwa na tatizo hili kwa namna moja au nyingine , na wasimamizi wa mabanki haya kama ni benki kuu au taasisi zingine ziwabane waendeshaji wa benki hizi kuhusu viwango vyao vya utoaji huduma na mawasiliano yao mengine waliyokuwa nayo kwa wateja wao .