Kwa hili simuungi mkono Rais Magufuli

Kwa hili simuungi mkono Rais Magufuli

Unamwuunga au humwuungi ni juu yako. Haitatokea akaungwa mkono kwa jambo lolote na watu wote. Mi binafsi namwuunga mkono. Pamoja na kuwa rais bado ana uchungu na miundombinu. Inaonyesha ana uchungu na barabara zetu na bila shaka mtu huyu pesa ikikaa vizuri atatandika mikeka nchi nzima. Si mwizi ila uchungu wa miundombinu mibovu humtia hasira. Pia anaakisi jina tingatinga. JK hakukosea.

Mimi namuunga mkono kuhusu barabara. Na simuungi mkono jinsi alivyo iwasilisha taarifa pale sio mahala pake. YEYE ange rudi ofisini kwake na angetoa taarifa. Ila tu angepigiwaje makofi, hapo ndio naona nivizuri ametolea taarifa pale ili apate walau kongole.
 
Hapa kuna tatizo kubwa. Ni muhimu kutofautisha nyumba za ibada na majukwaa ya kisiasa. Hakuna ulazima wa kuwatangazia wananchi mahudhurio ya viongozi kwenye shughuli za kidini, labda kuwe na mwaliko rasmi kiserikali.
 
Katiba yetu imeweka bayana kwamba serikali haina Dini, japo viongozi wa serikali wana Dini zao!

Rais Magufuli anafahamika kwamba yeye ni m-Kristo m-Katoliki! Kwamba kwa utashi wake anaamua kwenda kusali kwenye makanisa ya madhehebu mengine, ni swala lake binafsi!

Simuungi mkono anapokwenda kwenye makanisa hayo na waandishi wa habari/kamera na anapopewa nafasi ya kutoa salamu badala ya kuzungumza tu kama muumini, anazungumza kama Rais na anazungumzia mambo yenye mwangwi wa kisiasa!

Kipekee zaidi simuungi mkono kwa kwenda kuzungumzia swala la barabara ya Ubungo - Kibangu Kanisani kwa mzee wa upako!

Hata kama kweli aliguswa na mzee wa upako kwa vile anampenda, angaliweza kufanya ziara hata ya kushtukiza kwa wananchi wa eneo husika na kuwaahidi hilo!

Tena hili lingemletea heshima kubwa kwa jamii na hata kumjenga kisiasa!


Mzee wa upako TRANSFORMER ni mtumishi makini wa neno la Mungu.

Amewasaidia watu wengi sana kwa mambo mengi na ushauri wa kiroho.

Mh.Rais alienda kusali kama ambavyo mtu yeyote anayekwenda kusali either
msikitini au kanisani.(imani haina mipaka).

Ni vema tukawaunga mkono watumishi wa Mungu na haijirishi ni dhehebu gani au dini gani.

Kwa ufupi Mh.Rais alipata upako/roho wa bwana alimuingia na kusema aliyoyasema ambayo
ni mazuri na wala si dhambi.
 
Mzee wa upako TRANSFORMER ni mtumishi makini wa neno la Mungu.

Amewasaidia watu wengi sana kwa mambo mengi na ushauri wa kiroho.

Mh.Rais alienda kusali kama ambavyo mtu yeyote anayekwenda kusali either
msikitini au kanisani.(imani haina mipaka).

Ni vema tukawaunga mkono watumishi wa Mungu na haijirishi ni dhehebu gani au dini gani.

Kwa ufupi Mh.Rais alipata upako/roho wa bwana alimuingia na kusema aliyoyasema ambayo
ni mazuri na wala si dhambi.

Kama ni kweli alipata huo upako angejipiga mfukoni kwake binafsi atoe sadaka ya kuwezesha huduma za kijamii zinazosimamiwa na kanisa la mzee wa upako, lakini sio kutumia kodi za wananchi wote kumfurahisha mzee wa upako eti kwa vile anampenda! Barabara angeagiza akiwa ofisini ingetengenezwa tu japo angeyakosa makofi na vigele gele alivyopigiwa jana!
 
Ya wezekana usimuelewe maana alituma timu kuangalia ile barabara pamoja na kufanya evaluasheni na baadaye kachukua ripoti akaipeleka kanisani why?

Na hapo ndipo ilipo hoja yangu - kwa nini aipeleke hoja ya ujenzi wa barabara kanisani kwa mzee wa upako na sio kwa jamii ya eneo husika?
 
Katiba yetu imeweka bayana kwamba serikali haina Dini, japo viongozi wa serikali wana Dini zao! Rais Magufuli anafahamika kwamba yeye ni m-Kristo m-Katoliki! Kwamba kwa utashi wake anaamua kwenda kusali kwenye makanisa ya madhehebu mengine, ni swala lake binafsi!

Simuungi mkono anapokwenda kwenye makanisa hayo na waandishi wa habari/kamera na anapopewa nafasi ya kutoa salamu badala ya kuzungumza tu kama muumini, anazungumza kama Rais na anazungumzia mambo yenye mwangwi wa kisiasa! Kipekee zaidi simuungi mkono kwa kwenda kuzungumzia swala la barabara ya Ubungo - Kibangu Kanisani kwa mzee wa upako!

Hata kama kweli aliguswa na mzee wa upako kwa vile anampenda, angaliweza kufanya ziara hata ya kushtukiza kwa wananchi wa eneo husika na kuwaahidi hilo!
Tena hili lingemletea heshima kubwa kwa jamii na hata kumjenga kisiasa!

Mkuu uliambiwa humhum jf,tegemea sarakas na maigizo ya kutosha chin ya awamu hii,mengine yameshaanza kuzimika.Walikuwepo mawazir wanakagua sign book asubuh na makamera wako wap!Mkuu mwenyewe ameshachuja faster.
 
Back
Top Bottom