Kwa hili makampuni ya simu hayawezi kukwepa hizi lawama

FROWIN

JF-Expert Member
Jul 25, 2012
213
84
Habari za mida hii wadau wa Jf ,Leo nimepatwa na tatizo naomba msada wa ufumbuzi kidogo,swala lipo kama hivi,mnano tarehe 21/07/2018 nilifanya biashara na jamaa mmoja ambaye niliwasiliana naye kupitia simu. Baada ya makubaliano ya biashara yetu ,then akanitumia pesa na Mimi nikamtumia mzigo kumbe wakati huohuo mwenzangu hakuwa na lengo nzuri kibashara ,Leo tarehe 24/07/2018 nimepokea ujumbe kutoka Airtel kwamba pesa iliyotumwa kimakosa kutoka namba X imerejesha (kurudishwa) kwa aliyeituma kimakosa .Baada ya kufanya mawasiliano na airtel wakaniambia niwapigie voda kwa sababu mteja aliyetuma pesa ndiye aliyeomba pesa irudishwa kwamba imetuma kwangu kimakosa,kila nikipiga simu voda wananiambia wapigie airtel ndio walioruhusu pesa irudishwe.Sasa swali langu ni kwamba haya makampuni ya simu yanawezaje kurudishwa muhamala uliofanyika bila hata kunipigia simu? Pia haki ya mteja kama Mimi inatuzwaje kama mtu anaweza tu kupiga simu ya kusitisha muhamala na makampuni yakafanya hivyo?
 
Nadhani makampuni yote ya simu huwa yanatoa namba maalumu kama unataka kuwa unafanyia biashara, ukiwa na hiyo namba kamwe pesa hairudishwi kiboya. Japo kuna mtandao kama tigo huwa kabla ya kurudisha wanakupigia siku kwanza na kama kuna utata wanawakutanisha wote wawili. Kama namba siya biashara then mtu aliyetuma hiyo pesa nduye mwenye mamlaka na siyo wewe iliyeingia kwako
 
Nadhani makampuni yote ya simu huwa yanatoa namba maalumu kama unataka kuwa unafanyia biashara, ukiwa na hiyo namba kamwe pesa hairudishwi kiboya. Japo kuna mtandao kama tigo huwa kabla ya kurudisha wanakupigia siku kwanza na kama kuna utata wanawakutanisha wote wawili. Kama namba siya biashara then mtu aliyetuma hiyo pesa nduye mwenye mamlaka na siyo wewe iliyeingia kwako
Kimsingi ilitakiwa Mimi binafsi nipigiwe simu sasa hii haijafanyika,na inatakiwa wafanye hivyo kwa ajili ya kulinda haki ya mpokea pesa pia .
 
Kuna mshkaji alitaka kumtafuna demu! Demu akaomba nauli! Mshkaji akatuma nauli. Demu akapokea pesa na kisha akazima CMU. Jamaa akawapigia mtandao wa CMU. Akawambia nimetuma pesa kimakosa! Kampuni ya CMU wakamjibu ACHA UNDEZI, YULE NI DEMU WK
 
1.Ni vizuri kuchukua hatua mapema pale unapotumiwa pesa ujiridhishe umetoa unayo mkononi kisha ndipo utume mzigo hilo ni la kuzingatia kwa mnaofanya biashara.

2.Pesa za kutoka mitandao mingine (voda-airtel) huwa maamuzi yapo zaidi kwa wale wahudumu maana yeye alipaswa awasiliane na voda kuifatilia hiyo pesa ndipo akipatiwa majibu aweze kuirejesha.

3.Kwawewe mfanya biashara kuwa na line iliyo na usajili sahihi na ndipo uitumie kwa biashara yaani unapotumiwa pesa unaitoa au kama si kutoa unahamisha kwenda line yako ya mawasiliano hapo mtandao wowote hauwezi irudisha sababu pesa inarudi ikiwa imetumwa kwenda kwa mtu mmoja (P2P) ila akiongezeka mwingine wa tatu haiwezi rudi.
 
Haya makampununi ya simu ni hatari siku hizi, binafsi vodacom siwaelewi hata mimi. Pia mabank nayo siku hizi ovyo kabisa. Juzi nimepata ujumbe kuwa pesa yangu imekatwa kutoka akaunti yangu ya bank kwa madai kuwa walipigiwa simu na vodacom kuwa kuna muamala ulifanyika mwaka jana kutoka katika simu yangu kwenda bank kimakosa. Nnilipowapigia voda wadai wao hawahusiki na pesa hiyo nifuatilie bank. Bank waninipa maelezo ambayo sikuyaelewa baada ya kuwabana kuwa waniambie ni nani aliyewapa ruhusa ya kuingilia akaunti yangu na kutoa pesa bila idhini yangu? Hivyo hawa watu wanashirikiana kupiga pesa za watu.
 
1.Ni vizuri kuchukua hatua mapema pale unapotumiwa pesa ujiridhishe umetoa unayo mkononi kisha ndipo utume mzigo hilo ni la kuzingatia kwa mnaofanya biashara.

2.Pesa za kutoka mitandao mingine (voda-airtel) huwa maamuzi yapo zaidi kwa wale wahudumu maana yeye alipaswa awasiliane na voda kuifatilia hiyo pesa ndipo akipatiwa majibu aweze kuirejesha.

3.Kwawewe mfanya biashara kuwa na line iliyo na usajili sahihi na ndipo uitumie kwa biashara yaani unapotumiwa pesa unaitoa au kama si kutoa unahamisha kwenda line yako ya mawasiliano hapo mtandao wowote hauwezi irudisha sababu pesa inarudi ikiwa imetumwa kwenda kwa mtu mmoja (P2P) ila akiongezeka mwingine wa tatu haiwezi rudi.
Hata inatakiwa makampuni ya simu yafanye vinginevyo ili kulinda maslahi ya pande zote mbili huwezi kurudisha pesa kwa sababu tu aliyeituma karipot imetumwa kimakosa ,ilitakiwa wafanye mawasiliano pande zote mbili na kama kuna utata kesi iende kwenye vyombo vya sheria ,sio kuirudisha immediately mtu anapolipoti
 
We nae ukitumiwa pesa hamisha fastaa kwenda katika namba yako nyingine ....sikuhizi kila MTU na akili yake ....na wahudumu wa mitandao ndiyo vizibo kabisaaa hawajielewi utakua unakula hasara kila mara
 
Kama una Fanya biashara basi ni vema uka sajili line ya Lipa kwa M pesa (LiPa Namba) iyo ni special kwa wanaolipana kwa njia ya Simu ila hii P2P utalizwa sana maana watu hawana ustaarabu unampa mtu bidhaa ana piga simu kua ametuma pesa kimakosa naomba irudishwe!??
 
Akili kumkichwa hizi kesi ni nyingi sana "alie tumiwa pesa kimakosa akaitoa yote =alie tuma pesa akaomba pesa irudishwe ametuma kima kosa"
 
Kuna mshkaji alitaka kumtafuna demu! Demu akaomba nauli! Mshkaji akatuma nauli. Demu akapokea pesa na kisha akazima CMU. Jamaa akawapigia mtandao wa CMU. Akawambia nimetuma pesa kimakosa! Kampuni ya CMU wakamjibu ACHA UNDEZI, YULE NI DEMU WK
Hii chai
 
Habari za mida hii wadau wa Jf ,Leo nimepatwa na tatizo naomba msada wa ufumbuzi kidogo,swala lipo kama hivi,mnano tarehe 21/07/2018 nilifanya biashara na jamaa mmoja ambaye niliwasiliana naye kupitia simu. Baada ya makubaliano ya biashara yetu ,then akanitumia pesa na Mimi nikamtumia mzigo kumbe wakati huohuo mwenzangu hakuwa na lengo nzuri kibashara ,Leo tarehe 24/07/2018 nimepokea ujumbe kutoka Airtel kwamba pesa iliyotumwa kimakosa kutoka namba X imerejesha (kurudishwa) kwa aliyeituma kimakosa .Baada ya kufanya mawasiliano na airtel wakaniambia niwapigie voda kwa sababu mteja aliyetuma pesa ndiye aliyeomba pesa irudishwa kwamba imetuma kwangu kimakosa,kila nikipiga simu voda wananiambia wapigie airtel ndio walioruhusu pesa irudishwe.Sasa swali langu ni kwamba haya makampuni ya simu yanawezaje kurudishwa muhamala uliofanyika bila hata kunipigia simu? Pia haki ya mteja kama Mimi inatuzwaje kama mtu anaweza tu kupiga simu ya kusitisha muhamala na makampuni yakafanya hivyo?
Hapo HAKUNA LAWAMA YOYOTE kwa makampuni ya simu na ndio malipo ya dhambi ya kujaribu kukwepa kodi. Kama ni mfanyabiashara na umeona umuhimu wa matumizi ya malipo kwa njia ya simu zipo huduma maalumu za malipo unasubscribe ambazo mlipaji hawezi kutoa pesa alizolipa kwa huduma/bidhaa alizonunua. Kwenye miamala ya kawaida mtumaji ana haki ya kuomba pesa yake irejeshwe anytime anapoona kakosea na halina mjadala mno maana kampuni ya simu haifahamu consideration ya utumwaji wa fedha husika eti hadi impigie mtumiwaji kumuomba ridhaa.
 
Back
Top Bottom