Kwa hili, Hongera Mh. Rais Dr Jakaya Kikwete!

Ng`wanakidiku

JF-Expert Member
Apr 18, 2009
1,195
232
Great Thinkers,
Pamoja na ugumu wa maisha kwa watanzania, lakini hatuna budi kumpongeza Mh. Rais kwani kalitumikia taifa ktk mwaka 2011 kwa juhudi zake zote ktk kuhakikisha uchumi unaimarika na pia kudumisha amani. Japokuwa naamini kuna mengi alipaswa kuyafanya, nadhani tumtie moyo na kushirikiana naye ktk kujenga uchumi wetu, kwani yeye peke yake bila sisi wananchi kushirikiana ktk nyanja zote nchi haiwezi kuondokana na mambo yote ambayo tunahisi ni kikwazo ktk kufikia maisha yaliyo bora kwa kila mtanzania. Wewe kama kijana, mzee, mama, dada, au uwe ktk uongozi wa kifamilia (baba au mama au kaka) au uongozi wa kampuni, nadhani tunapenda japo kupongezwa hata kama hatujaweza kufikia lengo tulilojiwekea. Naomba tuungane ktk hili!
Mungu ibariki JF!
Mungu wabariki wana JF!
Great Thinkers daima mtadumu!!
Wenu Ng'wanakidiku!
30.12.2011
00:30 am
 
Natamani sana nikuunge mkono mkuu ila nafsi yangu inanisuta. Tokea JK awe raisi maisha yamezidi kuwa magumu na wakati huo marafiki zake wanazidi kuikwapua nchi mchana mchana. Ah mi utanisamehe, sioni la kumpongeza JK kama mwanadamu au kama Raisi (maana uraisi ni taasisi) ila namtakia mwaka mpya mwema
 
mi nina wasiwasi utakuwa ndo wewe JK umeiandika hii thread kwa sababu mtanzania wa kawaida haoni faida yoyote wala hakuna alichokipata tangu JK ameingia madarakani yaani kila kitu ovyo ovyo, Tanzania ya leo imekuwa kama changudoa kila mwanaume analala nayo
 
Great Thinkers,
Pamoja na ugumu wa maisha kwa watanzania, lakini hatuna budi kumpongeza Mh. Rais kwani kalitumikia taifa ktk mwaka 2011 kwa juhudi zake zote ktk kuhakikisha uchumi unaimarika na pia kudumisha amani. Japokuwa naamini kuna mengi alipaswa kuyafanya, nadhani tumtie moyo na kushirikiana naye ktk kujenga uchumi wetu, kwani yeye peke yake bila sisi wananchi kushirikiana ktk nyanja zote nchi haiwezi kuondokana na mambo yote ambayo tunahisi ni kikwazo ktk kufikia maisha yaliyo bora kwa kila mtanzania. Wewe kama kijana, mzee, mama, dada, au uwe ktk uongozi wa kifamilia (baba au mama au kaka) au uongozi wa kampuni, nadhani tunapenda japo kupongezwa hata kama hatujaweza kufikia lengo tulilojiwekea. Naomba tuungane ktk hili!
Mungu ibariki JF!
Mungu wabariki wana JF!
Great Thinkers daima mtadumu!!
Wenu Ng'wanakidiku!
30.12.2011
00:30 am

Kwanza, suala la rais kutumikia taifa ndiyo wajibu wake wa kwanza, hivyo hajafanya cha ziada ingawa amelitumikia chini ya kiwango. Pili,hapo kwenye kuimarisha uchumi umetudanganya kabisa.
 
kweli kabisa tumpongeze na kumpa ushirikiano haSa kwa kutoa uhuru wa kuongea,kutoa maoni japo kuna baadhi wanatumia uhuru huo kuropoka
 
kikwete ameSemwa sana ametukanwa sana lakini ameendelea kuwatumikia watanzania kwa moyo wake wote.big up sana jk
 
Ni kweli kabisa Rais anastahili pongezi maana kwa kipindi kifupi cha mwaka 2011 pekee amefanikiwa KUINUA maisha ya mtanzania wa kawaida kwa kupandisha kidogo tu bei ya mafuta ya taa, bei ya sukari nayo iko vizuri angalau kila mtanzania anaimudu, Sarafu yetu ndo imezidi kuimarika dhidi ya dola ya kimarekani, amefanikiwa kufanya mgao wa umeme kuwa historia kama alivyoahidi, na bei ya umeme bado iko chini sana, ingawa itapanda kidogo mwaka 2012 basi haitazidi 185% tu. Kwa kweli amefanya mengi ila haya ni machache tu.
 
mi nawapongeza polisi wake... Hasa kitengo cha utengenezaji maji ya kuwasha na tear gas!!
 
kikwete ameSemwa sana ametukanwa sana lakini ameendelea kuwatumikia watanzania kwa moyo wake wote.big up sana jk
Absurd!!!! Ama kweli binadamu sio sawa mkuu hebu naomba unilkumbushe JK kawatumikia wananchi kwa kufanya kitu gani amvacho mwenzetu umefaidika nacho???, au ndio unachafua hali ya hewa tu gerat thinker!?
 
Jk nakupongeza kwa kutoifungia jamiiforums kama ilivyo kwa nchi nyingine zinazobana uhuru wa kujieleza na kukosoa wa wananchi wake. utakumbukwa kwa hili
 
Aaah Mtoto wa Masika taratibu tafadhali, usitukosee heshima wanajamvi aisee, ntakupiga ban bwana. Unachoandika na dhamira yako haviendani mkuu...
Great Thinkers,
Pamoja na ugumu wa maisha kwa watanzania, lakini hatuna budi kumpongeza Mh. Rais kwani kalitumikia taifa ktk mwaka 2011 kwa juhudi zake zote ktk kuhakikisha uchumi unaimarika na pia kudumisha amani. Japokuwa naamini kuna mengi alipaswa kuyafanya, nadhani tumtie moyo na kushirikiana naye ktk kujenga uchumi wetu, kwani yeye peke yake bila sisi wananchi kushirikiana ktk nyanja zote nchi haiwezi kuondokana na mambo yote ambayo tunahisi ni kikwazo ktk kufikia maisha yaliyo bora kwa kila mtanzania. Wewe kama kijana, mzee, mama, dada, au uwe ktk uongozi wa kifamilia (baba au mama au kaka) au uongozi wa kampuni, nadhani tunapenda japo kupongezwa hata kama hatujaweza kufikia lengo tulilojiwekea. Naomba tuungane ktk hili!
Mungu ibariki JF!
Mungu wabariki wana JF!
Great Thinkers daima mtadumu!!
Wenu Ng'wanakidiku!
30.12.2011
00:30 am
 
Absurd!!!! Ama kweli binadamu sio sawa mkuu hebu naomba unilkumbushe JK kawatumikia wananchi kwa kufanya kitu gani amvacho mwenzetu umefaidika nacho???, au ndio unachafua hali ya hewa tu gerat thinker!?

chuo cha dodoma nimefaidika nacho nikiwa mmoja wa wahitimu wa hapo.

Panton la MV magogoni kigamboni na matengenezo ya panton la Mv kigamboni kwa kuweka engine mpya.

shule za sekondari za kata. mapungufu yake yakiboresha ni moja ya agenda bora kwa elimu kwa watanzania.

Umerudisha mahakama ya kadhi kwa waislamu wenyewe hata Mkapa ilimshinda. Sasa itaundwa na taasisi zake si serikali.

umetangaza kwa mara ya kwanza waasisi 17 wa kudai uhuru wa Tanganyika. Ni historia ilivyokuwa imefichwa.
 
kikwete ameSemwa sana ametukanwa sana lakini ameendelea kuwatumikia watanzania kwa moyo wake wote.big up sana jk

This is non sense! Asememwa kwa maouvu yake, hakuna uongo ..yaliyosemwa ju yake. yaliyosemwa ndiyo aliotenda! ametukanwa kwa lini? Hiv mtu akikuita mwizi na kweli umeiba hilo ni tusi hilo??..tuache unafiki hapa. zaid zaid yeye ndiye amekuwa akiwatukana wananchi wake kwa kuwaita... "mbayuwayu",wanafunzi wanaopata mimba,kuwaita.."wazembe".Wanaoshi mabondeni,kuwaita .."hawana akili timamu" ,wapinzani kuwapakazia.."udini na ukabila", n.k.

Anawtumikia watz?? acha upuuzi anawatumikia watz gani? mbona mafuta hamna na wafanyabiashara wameiweka serikali mfukonI..kakaa kimya?, mbona bei za bidhaa muhimu zinapanda kakaa kimya? mbona nchi inauzwa kwa mikataba mibovu,kila siku wageni wanazid kuja kuchimba madin yetu bila sisi kufaidi.. yeye anacheka cheka tuu? mbona hatuna umeme wala maji ya uhakika..anaweka smile tu? mbona dowans/al adawi aliyesema hamjui alipokuja ..alikimbia nje nakuacha mapesa yaithinishwe kumlipa? mbona wahanga wa mabomu na sasa mafuriko wanalia kutofikishiwa misaada yao..yeye anaziba masikio? mbona anahongwa suti kuuza ardi yetu? mbona elimu inazidi kushuka na kufaili kunazidi..yeye anazidi kuweka watendaji wabovu wizarini? mbona raia wasio na hatia wanuwawa tena na polisi waliopewa dhaman ya kuwalinda ..yeye ana anamrisha kutumia mabauvu?mbona amesaini muswada wa katiba mbovu, wakiwa anajua ni mbovu..kwa kuwogopa kuwakwaza wenzake kwenye chama tu? ....ameona ni bora kuwaridhisha mafisadi wenzake wachache kwenye chama kwa kuwaumiz mamili ya watz.
mbona...mbona ..zipo nyingi sana vichwani mwa watz!
labda wewe unayenufaika na huu utawala mmbovu ndio utasema amewatumikia..wewe na mafisadi wenzako, kama yeye alivyo fisadi , SHIT!!!. Anatakiwa..AJUIZULU..HATUFAI.
 
Back
Top Bottom