Kwa hili; CHADEMA hawakutenda Vyema, Walikosea!

Kwa hili; CHADEMA hawakutenda Vyema, Walikosea!

Filipo Lubua

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2011
Posts
339
Reaction score
578
Wenzangu WanaJF,

Nikiwa mnazi mkubwa wa mabadiliko yasiyoogopa gharama yoyote, naomba niwe kinyume na hili walilolifanya viongozi wa Chadema katika maandamano ya juzi kwa kile walichokiita kumshinikiza Anna Makinda Angoke kwenye kiti.

Kwa ujumla kila kitu kilifanyika vyema kabisa, hata kutoa namba za Anna Makinda kwa wananchi na dunia nzima bado ilikuwa sahihi. Viongozi wa Chadema, Zitto na Lema, walizisoma namba za Makinda waziwazi bila hata kificho. Hilo bado sioni kama lilikuwa tatizo.

Tatizo kubwa nilionalo ni kwamba, viongozi hawa hawakuwapa elimu wananchi kama namba zile zilikuwa zina umuhimu gani hasa. Wananchi hawakuelimishwa kuwa namba zile zilikuwa za kutuma maoni kwa Anna Makinda, maoni ya busara na yasiyo na matusi.

Katika hali ya namna ile, wananchi wataanza kumtukana Spika Makinda, bila hata kujua kama ni kiongozi mkubwa wa nchi. Wananchi wangetakiwa waelimishwe umuhimu wa kumhitaji Anna Makinda ajiuzulu lakini kwa lugha yenye staha na maneno ya hoja.

Ni wazi kuwa, kwa mfumo wa mawasiliano wa nchi yetu, bado wengi waliweza kutumia kadi za simu zisizosajiliwa na kumvurumishia Spika matusi (kama gazeti moja lilivyokwisha kuripoti).

Yawezekana bado hajatukanwa, ila yawezekana akatukanwa pia. Sharti tukubaliane kuwa watu hawakuelimishwa kuwa kuna madhara (repercussions) iwapo watamtumia jumbe za matusi. Ikiwa jumbe alizokwisha kutumiwa (au atakazotumiwa) zitakuwa zina matusi, hili litahafifisha hoja ya msingi ya Chadema kutaka kumng'oa Makinda (jambo ambalo mimi binafsi nisingependa litokee).

Kwa Chadema kutowaelimisha wananchi namna bora ya kumwandikia Makinda/Ndugai ujumbe, hili ni kosa; na matusi yote atakayotukanwa Makinda (maana kweli watu wamemchukia) itakuwa ni lawama kwa Chadema. Kwa kweli, bila ushabiki, kwa hili Chadema walikosea.

PEOPLES POWER!!
 
Wewe ni nani kakuambia katukanwa? Umethibitisha? Unaweza kuonyesha moja ya sms?

Achana na propaganda za Habari Leo
 
Teh teh teh!
wewe unajuaje kama kweli aliyotumiwa yalikuwa matusi?
Kumbuka kwa kuwa ukweli huwa unauma,wakati mwingine utafsiriwa kama matusi!
 
Uzushi mtupu,mbona ****** hajatukanwa?
 
Wewe ni nani kakuambia katukanwa? Umethibitisha? Unaweza kuonyesha moja ya sms?

Achana na propaganda za Habari Leo

Yawezekana hajatukanwa, ila yawezekana akatukanwa pia. Lazima tujifunze kukubaliana na hoja za msingi ambazo hata haziathiri mitazamo yetu ya kisasa na kivyama. Mimi pia nimeshamwandikia ujumbe Anna Makinda, na nashukuru viongozi wa Chadema kutoa namba, lakini sharti tukubaliane kuwa watu hawakuelimishwa kuwa kuna repercussions iwapo watamtumia jumbe za matusi. Ikiwa jumbe alizokwisha kutumiwa (au atakazotumiwa) zitakuwa zina matusi, hili litahafifisha hoja ya msingi ya Chadema kutaka kumng'oa Makinda (jambo ambalo mimi binafsi nisingependa litokee).
 
Hata wangepewa mistari ya kuandika ua topic za kuandika bado mtu anaweza kuandika anachojisikia kuandika. Hii ni expression ya uchungu wa dhuluma wanazofanyiwa watnzania kupitia bunge na serikali na hawana pa kuzipeleka. Kumbuka mtu mwenye hasira anaweza kufanya lolote bila kujali. Kama huamini nenda kajaribu kumshika rafiki yako wakati wa ugomvi,anaweza kukugeuka na kukudhuru..
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Wakati Lema akitoa hizo namba aliwasihi wananchi wasitukane lkn huwezi kumpangia mtu namna ya kuandika anavyotaka.
 
Huyo bi mkubwa hajatukanwa, anachofanya ni kutaka huruma ya watanzania, hana lolote.
 
Ndugu hata bungeni penyewe hao maspika na serkali yao kuambiwa ukweli kwao ni matusi jua ilo na imesababisha mda mwingine hata wabunge wa upinzani hama kutoka au kutolewa nje ya bunge. Pia watanzania ndio wenye uchungu na rasilimali zao basi kama ngivu ya umma imepata nafasi ya kuwaambia ukweli na waseme. Nawapongeza sana waliotoa hizo namba kama vipi ziwe zinatolea hata za mafisadi wengine tuwapashe ukweli tumechoka. Mwisho ndungu vuguvugu za kudai haki kwa viongozi kama hao si za negosition and constitution rather than struggling by any means! We kama vp ngoja haki yako kwa njia hiyo kama itakuja!
 
Wenzangu WanaJF,

Nikiwa mnazi mkubwa wa mabadiliko yasiyoogopa gharama yoyote, naomba niwe kinyume na hili walilolifanya viongozi wa Chadema katika maandamano ya juzi kwa kile walichokiita kumshinikiza Anna Makinda Angoke kwenye kiti.

Kwa ujumla kila kitu kilifanyika vyema kabisa, hata kutoa namba za Anna Makinda kwa wananchi na dunia nzima bado ilikuwa sahihi. Viongozi wa Chadema, Zitto na Lema, walizisoma namba za Makinda waziwazi bila hata kificho. Hilo bado sioni kama lilikuwa tatizo.

Tatizo kubwa nilionalo ni kwamba, viongozi hawa hawakuwapa elimu wananchi kama namba zile zilikuwa zina umuhimu gani hasa. Wananchi hawakuelimishwa kuwa namba zile zilikuwa za kutuma maoni kwa Anna Makinda, maoni ya busara na yasiyo na matusi.

Katika hali ya namna ile, wananchi wataanza kumtukana Spika Makinda, bila hata kujua kama ni kiongozi mkubwa wa nchi. Wananchi wangetakiwa waelimishwe umuhimu wa kumhitaji Anna Makinda ajiuzulu lakini kwa lugha yenye staha na maneno ya hoja.

Ni wazi kuwa, kwa mfumo wa mawasiliano wa nchi yetu, bado wengi waliweza kutumia kadi za simu zisizosajiliwa na kumvurumishia Spika matusi (kama gazeti moja lilivyokwisha kuripoti).

Yawezekana bado hajatukanwa, ila yawezekana akatukanwa pia. Sharti tukubaliane kuwa watu hawakuelimishwa kuwa kuna madhara (repercussions) iwapo watamtumia jumbe za matusi. Ikiwa jumbe alizokwisha kutumiwa (au atakazotumiwa) zitakuwa zina matusi, hili litahafifisha hoja ya msingi ya Chadema kutaka kumng'oa Makinda (jambo ambalo mimi binafsi nisingependa litokee).

Kwa Chadema kutowaelimisha wananchi namna bora ya kumwandikia Makinda/Ndugai ujumbe, hili ni kosa; na matusi yote atakayotukanwa Makinda (maana kweli watu wamemchukia) itakuwa ni lawama kwa Chadema. Kwa kweli, bila ushabiki, kwa hili Chadema walikosea.

PEOPLES POWER!!

Mbona iyo ni intro tu, tunaomba na huku kwetu mikoani watupe izo namba tumuonyeshe kazi huyu bibi
 
Wenzangu WanaJF,

Nikiwa mnazi mkubwa wa mabadiliko yasiyoogopa gharama yoyote, naomba niwe kinyume na hili walilolifanya viongozi wa Chadema katika maandamano ya juzi kwa kile walichokiita kumshinikiza Anna Makinda Angoke kwenye kiti.

Kwa ujumla kila kitu kilifanyika vyema kabisa, hata kutoa namba za Anna Makinda kwa wananchi na dunia nzima bado ilikuwa sahihi. Viongozi wa Chadema, Zitto na Lema, walizisoma namba za Makinda waziwazi bila hata kificho. Hilo bado sioni kama lilikuwa tatizo.

Tatizo kubwa nilionalo ni kwamba, viongozi hawa hawakuwapa elimu wananchi kama namba zile zilikuwa zina umuhimu gani hasa. Wananchi hawakuelimishwa kuwa namba zile zilikuwa za kutuma maoni kwa Anna Makinda, maoni ya busara na yasiyo na matusi.

Katika hali ya namna ile, wananchi wataanza kumtukana Spika Makinda, bila hata kujua kama ni kiongozi mkubwa wa nchi. Wananchi wangetakiwa waelimishwe umuhimu wa kumhitaji Anna Makinda ajiuzulu lakini kwa lugha yenye staha na maneno ya hoja.

Ni wazi kuwa, kwa mfumo wa mawasiliano wa nchi yetu, bado wengi waliweza kutumia kadi za simu zisizosajiliwa na kumvurumishia Spika matusi (kama gazeti moja lilivyokwisha kuripoti).

Yawezekana bado hajatukanwa, ila yawezekana akatukanwa pia. Sharti tukubaliane kuwa watu hawakuelimishwa kuwa kuna madhara (repercussions) iwapo watamtumia jumbe za matusi. Ikiwa jumbe alizokwisha kutumiwa (au atakazotumiwa) zitakuwa zina matusi, hili litahafifisha hoja ya msingi ya Chadema kutaka kumng'oa Makinda (jambo ambalo mimi binafsi nisingependa litokee).

Kwa Chadema kutowaelimisha wananchi namna bora ya kumwandikia Makinda/Ndugai ujumbe, hili ni kosa; na matusi yote atakayotukanwa Makinda (maana kweli watu wamemchukia) itakuwa ni lawama kwa Chadema. Kwa kweli, bila ushabiki, kwa hili Chadema walikosea.

PEOPLES POWER!!
Siyo hilo tu, viongozi wakuu wa CHADEMA hawawezi kukwepa lawama ya kushiriki moja kwa moja kumtusi Madame Spika.
Staha ya majadiliano hakuna na mimi sishangai sana uelewa wa viongozi wengi wa CDM, hawana tofauti sana wa wan JF, ambao hurusha matusi ya nguoni wanapojikuta wamebanwa.
 
Wenzangu WanaJF,

Nikiwa mnazi mkubwa wa mabadiliko yasiyoogopa gharama yoyote, naomba niwe kinyume na hili walilolifanya viongozi wa Chadema katika maandamano ya juzi kwa kile walichokiita kumshinikiza Anna Makinda Angoke kwenye kiti.

Kwa ujumla kila kitu kilifanyika vyema kabisa, hata kutoa namba za Anna Makinda kwa wananchi na dunia nzima bado ilikuwa sahihi. Viongozi wa Chadema, Zitto na Lema, walizisoma namba za Makinda waziwazi bila hata kificho. Hilo bado sioni kama lilikuwa tatizo.

Tatizo kubwa nilionalo ni kwamba, viongozi hawa hawakuwapa elimu wananchi kama namba zile zilikuwa zina umuhimu gani hasa. Wananchi hawakuelimishwa kuwa namba zile zilikuwa za kutuma maoni kwa Anna Makinda, maoni ya busara na yasiyo na matusi.

Katika hali ya namna ile, wananchi wataanza kumtukana Spika Makinda, bila hata kujua kama ni kiongozi mkubwa wa nchi. Wananchi wangetakiwa waelimishwe umuhimu wa kumhitaji Anna Makinda ajiuzulu lakini kwa lugha yenye staha na maneno ya hoja.

Ni wazi kuwa, kwa mfumo wa mawasiliano wa nchi yetu, bado wengi waliweza kutumia kadi za simu zisizosajiliwa na kumvurumishia Spika matusi (kama gazeti moja lilivyokwisha kuripoti).

Yawezekana bado hajatukanwa, ila yawezekana akatukanwa pia. Sharti tukubaliane kuwa watu hawakuelimishwa kuwa kuna madhara (repercussions) iwapo watamtumia jumbe za matusi. Ikiwa jumbe alizokwisha kutumiwa (au atakazotumiwa) zitakuwa zina matusi, hili litahafifisha hoja ya msingi ya Chadema kutaka kumng'oa Makinda (jambo ambalo mimi binafsi nisingependa litokee).

Kwa Chadema kutowaelimisha wananchi namna bora ya kumwandikia Makinda/Ndugai ujumbe, hili ni kosa; na matusi yote atakayotukanwa Makinda (maana kweli watu wamemchukia) itakuwa ni lawama kwa Chadema. Kwa kweli, bila ushabiki, kwa hili Chadema walikosea.

PEOPLES POWER!!

Wewe umeliona tu la wananchi kukosa busara,lakini la spika kuzuia hoja(matatizo ya wananchi)zisijadiliwe hilo kwako hukuliona.Sinza maji hamna ni shida sana,watu tunaoga na maji kisado ulitarajia wananchi tumkenulie Spika Makinda?Inawezekana mwenzetu geti kali hakuna tatizo kbs,hebu tulia wenye nchi tuzungumze nnaona wewe huna la maana la kuzunguzia.
 
Wewe umeliona tu la wananchi kukosa busara,lakini la spika kuzuia hoja(matatizo ya wananchi)zisijadiliwe hilo kwako hukuliona.Sinza maji hamna ni shida sana,watu tunaoga na maji kisado ulitarajia wananchi tumkenulie Spika Makinda?Inawezekana mwenzetu geti kali hakuna tatizo kbs,hebu tulia wenye nchi tuzungumze nnaona wewe huna la maana la kuzunguzia.

Ni wazi Anna Makinda ametuonea Watanzania, lakini kamwe hatuwezi kumkataa kwa kumtukana. Ni sharti tujue kuwa siasa za matusi hazitakiwi. Tumng'oe kwa hoja na nguvu ya umma, si umma kumtukana
 
Ni wazi Anna Makinda ametuonea Watanzania, lakini kamwe hatuwezi kumkataa kwa kumtukana. Ni sharti tujue kuwa siasa za matusi hazitakiwi. Tumng'oe kwa hoja na nguvu ya umma, si umma kumtukana

Mshahara wa dhambi ni mauti" mshahara wa kununuliwa na mafisadi ni kudharauliwa na watanzania"
so yanayomkuta mama Makinda either ametukanwa au la ni mshahara anavuna wa kukubali kuwatumikia
mafisadi na kutuumiza watanzania"
 
Tusitumie hizo simu kutukana viongozi wa kitaifa, bali tutumie simu kumwonyesha Anna Makinda na Job ndugai kwamba kiti walichokikalia sio mali ya ccm bali ni mali ya umma wa watanzania bila kujali vyama vya siasa.wanachofanya makinda na Ndugai ni kudhoofisha nguvu ya chadema
 
huyu mama spika na naibu wake walikataa kabisa mgomo wa madaktari na walimu kujadiliwa bungeni kwa faida ya serikali huku wakijifanya wanasimamia kanuni,hawa ni nani hadi wadiriki ku-sacrifice 44 milions tanzanians?wajiulize mbona enzi ya samuel sitta watu hawakuandamana kumpinga?hawana tofauti na wauaji.Kwa sababu ya cheo tu? wameingia kwenye historia ya tz,worst leaders of parliament ever to exist in the history of our nation.
 
Hako ka mama sasa kanataka kuhamisha mawazo ya watanzania kutoka kwenye hoja ya msingi ya uendeshaji ovyo wa bunge na badala yake wakaonee huruma??Acha avune upumbavu wake
 
Kufuata taratibu, kanuni na sheria ndo vimetufisha hapa.
 
Back
Top Bottom