Uchaguzi 2020 Kwa hali hii, CHADEMA wanajiandaa kuvunja Muungano

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,603
29,747
Lissu yupo Zanzibar kusaka kura za urais wa Jamhuri.

Nimeanza na dibaji hiyo kwa minajili ya kusema yafuatayo:

1. Katika kunadi sera zake na ahadi za mgombea wa Urais hajawahi kuzungumzia namna atakavyolinda na kuuenzi Muungano ulioasisiwa na mababa wa mataifa ya Tanganyika na Zanzibar.

2. Akiwa Bungeni, Mhe. Lissu aliwahi kuzungumzia Muungano akionyesha kutoukubali na utayari wa kuuvunja.

3. CHADEMA katika harakati zake inakwepa kujadili Muungano wetu.

4. Hawajaweka mgombea wa urais wa Zanzibar na wametangaza kumuunga mkono Maalim Seif ambaye siku zote amekuwa akidai Muungano hauna manufaa na akiupata urais wa Zanzibar atavunja Muingano huo.

Hivyo, endapo Lissu atashinda Bara na Maalim akashinda visiwani basi meza ya muungano itapinduliwa kirahisi kifuta historia tukuka ya Muungano na mshikamano wa kitaifa.

5. CHADEMA haikutangaza awali kumuunga mkono Maalim Seif hapo awali lakini baada ya Seif kuhamasisha wafuasi wake kubeba majambia, mashoka na mundu ili kuleta machafuko, hatua hiyo imeipelekea CHADEMA kuona wamepata mshirika anayeendana na malengo yao.

Ikumbukwe CHADEMA ilipozindua kampeni zake pale Zakhiem ilitangaza maandamano ya nchi mzima kipindi hiki kwa minajili ya kushinikiza hoja zao na kuleta machafuko nchini.

Kwa sababu hii na nyinginezo inapelekea allegations za CHADEMA kujiandaa kuvunja Muungano wetu tukuka.

Hivyo, sisi wapigakura tunajua nini cha kufanya hapo Oktoba 28 ili kuulinda na kuuenzi Muungano wetu.

Msanii JF
 
Huo Muungano hauna ridhaa ya wananchi, bali ni muungano wa shuruti wa viongozi wa ccm. Huo muungano hauna maana yoyote, bali una dalili zote kuwa upo kishirikina zaidi.

Leo hii zikipigwa kura za maoni huru za kuvunja muungano, saa 2 na nusu asubuhi, huo muungano wa maagano ya kishirikina utakuwa umevunjika rasmi.
 
Huo muungano hauna ridhaa ya wananchi, bali ni muungano wa shuruti wa viongozi wa ccm. Huo muungano hauna maana yoyote, bali una dalili zote kuwa upo kishirikina zaidi.

Leo hii zikipigwa kura za maoni huru za kuvunja muungano, saa 2 na nusu asubuhi, huo muungano wa maagano ya kishirikina utakuwa umevunjika rasmi.
Wewe hujui manufaa na faida za Muungano
 
Hawawezi maana huu muungano tumeapa kuulinda mpaka kwa tone la mwisho la damu zetu

Muungano uliopo kishirikina sintoshangaa ukilindwa kwa kafara ya damu. Huu muungano na mwenge wa uhuru, ni mambo ya kishirikina ya wazi hapa nchni. Ili Tanganyika yetu iwepo, haya mambo lazima yafikie mwisho.
 
Mwaka huu tutasikia mengi.

Haki, uhuru na maendeleo ndiyo habari mjini. Kama mgombea wenu hajui umuhimu wa hayo, na atangulie Chatto kuchunga ng'ombe tu.

Habari ndiyo hiyo.

Hatudanganyiki!
 
Labda kwa maoni yako muungano una manufaa gani? Yaani ikitokea muungano umevinjika bara wataathirka nini? Au Zanzibar itakosa nini, tuache kuaminishwa kijinga. Hizi ni enzi zingine manufaa yaliyokiwepo wakati huo hayapo tena hivi sasa. By the way, utakuwa siyo muungano wa kwamza kufa. Tumeona miungano ya maana ikifa hapa duniani sembuse huu wetu.wengi mnaogopeshwa tuu kuvunjika bila kunua madhara yake.
 
Ilani ya Chadema ni kuwa na serekali tatu
Hiyo ya kuvunja muungano sijui umeokota wapiView attachment 1563608

IMG_20200908_204916.jpg

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom