Nianze kwa kumshukuru Mungu kutuwezesha kuiona Siku hii nzuri ya leo.
Pamoja na hayo nimefedheheshwa sana na hujuma na upendeleo wanaopata Ccm toka katika vyombo mbalimbali hasa vilivyopo chini ya dola na vinavyohudumiwa na kodi ya watanzania.
Angalia vyombo vya habari vya umma, angalia mienendo ya vyombo vya usalama, angalia mienendo ya wafanyakazi wengine wa ngazi za juu Serikalini kote huko hofu ya kitu kiitwacho Ccm, chenye uwezo feki wa kuumba na kubomoa.
JE SASA TUFANYE NINI?
Kwa kuwa Mungu ni kwema tena ni mwenyehaki, na anayewatumia wanyonge walio dhaifu na vitu vinavyoonekana kuwa si kitu mbele ya wanadamu. Basi wale wote tunaoamini katika Mungu tuitumie Jumamos hii ya Leo 22/08/2015 na kesho tarehe 23/08/2015. Katika kumuomba mwenyezi Mungu ashushe mvua ya kutosha kupafanya jangwani ambapo Ccm wamepanga kufanya mkutano wao ili waendelee kututawala kwa hila pajae maji ya mvua na mkutano huo usifanikiwe.
KWA NINI MUNGU ATATUSIKILIZA.
1. Mungu wetu pia kaichoka Ccm kwa hiyo yupo upande wa mabadiliko, Mungu amekasirishwa sana na mauaji ya Albino, uporaji wa raslimali alizotupa taifa lake teule. Mauaji ya vikongwe, wachawi kuwa na nafasi kwenye Maisha ya baadhi ya wakuu wetu.
MUNGU AMESHUSHWA MPAKA KUFIKIA HATUA YA WACHAWI KUJIPA KAZI YA KUWALINDA WAKUU WETU.
HAKIKA MUNGU AMEKASIRIKA NA TENA AMEIPIGA CCM UPOFU.
2. Mungu Atatusikiliza kwa kuwa wanyonge ndio wanaoonewa katika nchi hii, fikiria wanawake wanaokufa kwa kukosa huduma ya uzazi wakati mwenyewe wakikohoa wanenda kutibiwa ulaya, angalia wanafunzi kutoka familia za kawaida wanaokosa mikopo ya elimu vyuo vikuu wanavyoangaika wakati watoto wao wanasoma shule za hali juu kwa kodi yetu.
MWISHO
Kila MTU mwenyewe mapenzi mema aombe japo kwa kutamka maneno machache kila unapopata wasaha.
"MUNGU TUNAOMBA MVUA DAR ES SALAAM HASA JANGWANI SIKU YA TAREHE 23/08/2015 . ILI ALBINO NA WATU WAKO WANYONGE KATIKA TAIFA LAKO WAKAPATE KUISHI KWA AMANI"
MUNGU WETU NI MWENYE NGUVU NAYE UWASIKIA WALE WAMWITAO KWA IMANI NA MATUMAINI
Pamoja na hayo nimefedheheshwa sana na hujuma na upendeleo wanaopata Ccm toka katika vyombo mbalimbali hasa vilivyopo chini ya dola na vinavyohudumiwa na kodi ya watanzania.
Angalia vyombo vya habari vya umma, angalia mienendo ya vyombo vya usalama, angalia mienendo ya wafanyakazi wengine wa ngazi za juu Serikalini kote huko hofu ya kitu kiitwacho Ccm, chenye uwezo feki wa kuumba na kubomoa.
JE SASA TUFANYE NINI?
Kwa kuwa Mungu ni kwema tena ni mwenyehaki, na anayewatumia wanyonge walio dhaifu na vitu vinavyoonekana kuwa si kitu mbele ya wanadamu. Basi wale wote tunaoamini katika Mungu tuitumie Jumamos hii ya Leo 22/08/2015 na kesho tarehe 23/08/2015. Katika kumuomba mwenyezi Mungu ashushe mvua ya kutosha kupafanya jangwani ambapo Ccm wamepanga kufanya mkutano wao ili waendelee kututawala kwa hila pajae maji ya mvua na mkutano huo usifanikiwe.
KWA NINI MUNGU ATATUSIKILIZA.
1. Mungu wetu pia kaichoka Ccm kwa hiyo yupo upande wa mabadiliko, Mungu amekasirishwa sana na mauaji ya Albino, uporaji wa raslimali alizotupa taifa lake teule. Mauaji ya vikongwe, wachawi kuwa na nafasi kwenye Maisha ya baadhi ya wakuu wetu.
MUNGU AMESHUSHWA MPAKA KUFIKIA HATUA YA WACHAWI KUJIPA KAZI YA KUWALINDA WAKUU WETU.
HAKIKA MUNGU AMEKASIRIKA NA TENA AMEIPIGA CCM UPOFU.
2. Mungu Atatusikiliza kwa kuwa wanyonge ndio wanaoonewa katika nchi hii, fikiria wanawake wanaokufa kwa kukosa huduma ya uzazi wakati mwenyewe wakikohoa wanenda kutibiwa ulaya, angalia wanafunzi kutoka familia za kawaida wanaokosa mikopo ya elimu vyuo vikuu wanavyoangaika wakati watoto wao wanasoma shule za hali juu kwa kodi yetu.
MWISHO
Kila MTU mwenyewe mapenzi mema aombe japo kwa kutamka maneno machache kila unapopata wasaha.
"MUNGU TUNAOMBA MVUA DAR ES SALAAM HASA JANGWANI SIKU YA TAREHE 23/08/2015 . ILI ALBINO NA WATU WAKO WANYONGE KATIKA TAIFA LAKO WAKAPATE KUISHI KWA AMANI"
MUNGU WETU NI MWENYE NGUVU NAYE UWASIKIA WALE WAMWITAO KWA IMANI NA MATUMAINI