Kwa Dada Zangu Na Mama Zangu

Kwa Dada Zangu Na Mama Zangu

Ambiele Kiviele

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
15,271
Reaction score
29,934
Amekutext Inbox

Ukamuuliza we nani?

Akaujibu jina

Ukamuuliza umepata wapi namba yangu?

Akakujibu, nimepata kwa group

Ukachukulia poa tu

Amekuomba urafiki facebook

Umeangalia picha zake

Anaendesha Range

Anaonekana ni jamaa mwenye uwezo

Umemkubalia urafiki

Amekutumia text inbox

Umemjibu

Amekuomba out

Mkapanga kuonana

Ukajikwatua mwenyewe

Ukajipulizia na marashi ya kunukia vyema

Ukaweka na make-up na weave mpya.

Akakuchukua kwa ajili ya lunch kwa hotel

Akakuagizia na soft drinks

Mkawa na muda mzuri pamoja

Akakushika mkono

Akakufanya uwe unacheka muda wote kwa vituko vyake

Ukampenda

Ikawa kama umemjua kwa miaka

Akakuchukua kwenda kwake

Akaweka mazingira ya wewe kujisikia upo kwako kwa kukuruhusu ulale kitandani kwake

Akakubusu kimahaba

Ukapenda jinsi alivyo romantic, nguvu na ujasiri

Ukajisikia secure ukiwa nae

Ukajua kuwa unachoenda kufanya sio sahihi lakini ukajisikia poa tu

Ukamwambia atumie kinga, akakuambia it's too late.

Ukamkubalia na hukutaka kumsumbua.

Akakuambia anakupenda na hukusita kumwambia unampenda pia.

Baada ya kumaliza akafungua friji na kukunywesha maji ya kunywa. Ukajihisi hapa mume nimepata

Ukajihisi ni mwanamke special

Atakuwa ndio yeye uliyekuwa ukimuota siku zote.

Ukavua nguo

Mkafanya

Ukavaa nguo.

Akakuchukua mpaka sehemu zinakopaki taxi

Akakubusu katika shavu.

Nimekuwa na muda mzuri na wewe akakueleza.‍♂

Akakupa Tsh 100,000.

Ukatabasamu na kumwambia nitakuona kesho.

Akabaki kimya. Taxi uliyopanda ikaondoka.

Ndani ya taxi hukuacha kutabasamu

Ukafika nyumbani kwenu na kumwandikia text watsapp kwamba umefika salama.

Yupo online lakini hakujibu text yako

Ukaamua kumtext tena, hakujibu!

Dakika chache baadae humuoni watsapp unaona kivuli tu. AMEKUBLOCK!!

Siku, wiki, miezi ikapita ukaanza kujisikia homa homa, mchovu, uzito umepungua na utando mdomoni

Ukaenda kituo cha afya

Ukapima

Nusu saa baadae daktari anaingia.

Pole sana dada yangu daktari anakuambia.

Una maambukizi ya virusi vya UKIMWI na ni mjamzito vile vile.

Mimba, HIV+????

HOW??

Hauelewi

Inakuumiza sana, hauamini.

Unaenda nyumbani.

Ukiwa na hofu kubwa.

Unaona kifo hichi hapa

Unatazama angani, na unauona mwisho wako huu hapa. Unajuta kumuamini mtu kirahisi hivyo.

DADA ZANGU NA MAMA ZANGU MSIWE KAMA HUYU, ISHI VIZURI, ACHA KUTAMANI MATERIAL THINGS. KUWA MWANAMKE AMBAE UNAMSIMAMO

ISHI MAISHA YANAYOMPENDEZA MWENYEZI MUNGU PEKEE NA SIO BINADAMU.

SIJAKATAZA MSIAMINI WACHUMBA WA FACEBOOK na WHATSAPP ila Biblia inasema (msiamin kila roho ila zichunguzen hizo roho kama zimetokana na Mungu). Mke + mme mwema anatoka kwa Bwana
 
Back
Top Bottom