Gesi Kwanza
Member
- Feb 16, 2013
- 14
- 1
Kuna taarifa kuwa polisi mkoani Lindi wamezuia maandamano na mkutano wa hadhara ulioitishwa na chama cha CUF kujadili maazimio ya gesi yaliyotolewa na serikali.Pia kujua nini kinaendelea ktk mradi huo na ahadi ya kujenga viwanda vya mbolea na kufua gesi ghafi kabla haijasafirishwa. Je,serikali inapozuia wananchi kukusanyika na kujadili na kupeana habari inadhani ndiyo tiba ya kufanya wananchi wasiihoji serikali yao? Hawa watawala hawajui kama enzi za "ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI WA CHAMA" zimeisha? Wananchi wanataka kujua mustakabali wa maendeleo yao,watawala wanazuia hiyo ndio tiba?