Zesh
JF-Expert Member
- Apr 27, 2017
- 15,381
- 24,979
Hahaahah kwa mawifi ndiooooUnataka kutapika?
Hahaahah kwa mawifi ndiooooUnataka kutapika?
Hongera sana mkuuu kwa kuona kitu kikubwa alichonacho mkeo sio wanaume wote wenyemacho ya kuona kitu anachofanya mkewake na kumsifia na kumpa sapotiNdungu wana Jamvi nimeleta kwenu uzi huu ili tuweze kuuchambua, natumai humu wamo walioowa na wanaotarajia kuoa. Hapa utajifunza
Mke wangu mimi ni darasa la saba, mimi nimemaliza chuo kikuu ni mhasbu nafanya kazi benki na nina mshahara mkubwa tu. Nilikutana na mke wangu kipindi kaja kuchukua mkopo wa Biashara yake, wakati huo nilikua afisa mikopo. Alinielezea kuhusu Biashara yake, plan zake na namna alivyoanza Biashara nilimuambia ondoka uje kesho. Lakini alipokua anaondoka nilimuita dada mmoja rafiki yangu na kumuambia nitamuoa yule dada, yule ndiyo mke wangu. Hakuamini lakini nilimtongoza nikampata na sasa hivi ni mke wangu.
Ana akili sana huyu mwanamke, kabla ya kumuoa nilikua nisshafanya kazi miaka tisa, nilikua na Gari tena ya mkopo na kiwanja tu. Nilijua sina akili kama yeye hivyo nilimuongezea mtaji kwenye Biashara yake na kumaucha afanye miujiza yake maana mimi naiita miujiza. Sasa hivi ndoa yangu ina miaka sita, tuna nyumba mbili, viwanja vitatu maduka mawili makubwa ambayo tunasimamia wote na vitu vingine vingi. Ingawa majina ni yetu wote lakini hakuna chakwangu hapo.
Mwaka jana mke wangu aliniambia kuwa anataka kuwajengea wazazi wake, nilimuambia poa. Kwetu kuna nyumba kubwa tu ambayo tulijenga na ndugu zangu na nahudumia kama kawaida. Alipoanza kujenga nikaona ndugu zangu kama nyuki, wanavamia na maneno, kunijaza kuwa nimetekwa sijui na maujinga ujinga mengi. Mama naye alianza kumchukia mke wangu mara aniambie kamuongelesha vibaya, mara aniambie hivi mara vile, mara ghafla kabila eti kisa wachaga ataniua sijui nini alikuja hana kitu huku anapendeza.
Baada ya kelele nyingi niliona hii itakuja kuniletea shida. Siku moja nilienda nyumbani, nikaomba kuongea na Mama, alianza kuniambia manano mengi nikamsikiliza sana nikamuambia. “Mama hivi kabla ya kuoa nilikua na nini?” Alinyamaza kisha akaniambia Gari, nikamuuliza na sasa hivi? Akataja vile vichache anavyovijua, nilimtajia na vingine vingi ambavyo havijui akabaki kushangaa. Akaniambia tatizo hushirikishi ndugu zako nikamuambia kwani walishiriki kuzichuma. Nilimuambia;
“Mama nakupenda sana, ila jua kuwa sina akili kama mke wangu nikimuacha yule mwanamke kesho keshokutwa nitakua kama fala flani hivi sina kitu na yule mwanamke hata nikimuacha na laki moja tu mwakani ni milionea. Nauchukuia sana umasikini hivyo kawaambie wanao kuwa wakiendelea kumsumbua mke wangu basi hata kwangu hawatakanyaga. Kujifanya wananiheshimu halafu wanamdharau mke wangu ni unafiki. Mke wangu simuachi, kwao haachi kujenga kama unataka nyumba Mama nilishakujengea hao ndugu watafute vyakwao na wenza wao!”
Mama aliongea sana akilalamika kuwa nimetekwa akili nikamuambia wewe ni Mama yangu hata ukinitukana siwezi kuacha kukuhudumia kwani ni kazi yangu lakini siwezi kumuacha mke wangu, ila waambie wanao kuwa wakimsumbua mke wangu nitasahau kuwa tumezaliwa tumbo moja. Mama aliongea, akaongea lakini niliondoka. Walijua kama natania wakidhani kama nimelishwa limbwata, ile nafika nyumbani mke wangu nakuta hajachangamka, nilimuuliza tatizo ni nini hakuniambia alisema yuko sawa.
Nilihisi kitu nikachukua simu yake, nikaangalia meseji mdogo wangu wakike alikua akimtukana mke wangu kuwa amenilisha limbwata mpaka imefikia hatua namtukana Mama yangu, mara ataondoka tu laana itamshika na mambo kibao. Nilichukua simu ya mke wangu na kumpigia, alipokea hata kabla ya salamu alianza kutukana na vitishi kibao. Nilimuambia kuwa “Inaelekea Mama hakukupa ujumbe wangu vizuri ukauelewa, nilisema atakateendelea kumsumbua mke wangu nitasahau kama ni ndugu yangu, basi wewe nimesahau!”
Nilikata simu na sikumtafuta, ilikua mwaka jana, yeye yuko chuo nilikua namlipia mimi kila kitu nikakata kabisa, nikamuambia sitatoa. Mama akapiga simu akalia lakini nikakataa, mke wangu alinibembeleza sana kumsamehe lakini wapi nilimuambia sitaki. Nilifanya makusudi ili wajue kuwa namaanisha, mwaka huu wote ada aliyelipa ni mke wangu, hawakuniambia lakini najua kwani Mama ndiyo alikua anapiga anamuomba na pia sasa hivi akitaka matumizi anamuomba Mama ili Mama aniombe nimpe.
Najua zinaenda wapi lakini nawacheka tu. Itoe Post yangu kwani mdogo wangu anakusoma sana ajue nimemsamehe ila ajue kuwa mke wangu ni jembe. Ana akili ya Biashara ambayo mimi sina, nina ya darasani tu ila Biashara huyu mwanamke hapana, wakati mimi nikiangalia laki moja naona raundi kadhaa za nyama choma na washikaji , yeye laki moja anaona mtaji wa Biashara. Nimuambie tu mdogo wangu najua bado yeye na Mama wanaamini nimelogwa, hapana ishu sitaki tu umasikini nikimuacha huyu mke wangu anaondoka na mali zake sitaweza kuziendelea na hata nikiwapa nyinyi hamuwezi kuziendeleza!
NB: Kuna wanaume wengi wanafanikiwa kupitia migongo ya wanawake lakini niwachache wanaweza kukubali kama umemkubali huyu basi endelea kufuatulia
Sijui ndugu huwa mnamatatizo gani hasa wadada
Ukiishi na mkeo vizuri,kwa furaha,amani,upendo,upendo wa vitendo lazima mfanikiwe tuuuaseh pole sana, mke ana nafas yake na ndgu wana nafasi zao, wasiingliane ktk haki.
Jambo la pili ndoa ni watu wawili...
Akupe mmoja alafu anayefuata nipewe Mimi...nimeshaweka bookingDuh jamaa yangu nilengesheee mdogo wake wallah nipo serious duh kuna wanawake jaman majembe yaani huyo ukianza kumla mambo mpaka unajihisi maupako ila Kuna wengine ukiwa unawala mambo unajihisi mamikosi.
Kweli kabisa mkuuTamu zaidi ya asali
Kiko sawa mkuuAiiise na mimi nina kichaga changu ni kiform four leaver sijui kitakuwa kama mke wako
Zitumie mkuuMosi ulimuinterview (pale bank)
Pili ukamuamini (kuamua kumuoa)
Tatu ukampa nafasi ya kuprove kile kilichomo ndani yake (fikra zake)
Nimekubali mbinu zako
Hapana mkuu, ni mchango wangu tu. Naangalia nafasi za wote wawili.Wewe mbona kama shemeji mtu? Comment yako imejaa chuki hivi
Sawa mkuu ila cdhani kama mkuu atapendaAkupe mmoja alafu anayefuata nipewe Mimi...nimeshaweka booking
Kama itakavyokuwa ndoa yetu handsomeHakika, ila hasa mwanaume ukiweza kutambua kuwa ndoa ni yako na kwanini ulimchagua mkeo. Ndoa ni tamu sana.
Inatakiwa msimamo haswaa... Ukilegea tuu ndoa inayumbaNilitukuza ndugu wa mke wangu walipotamka kuwa nyumba hii amejenga ndugu yao mbele ya mama yangu. Ndugu hatari sana kwa ndoa