Kilongwe
JF-Expert Member
- Feb 7, 2008
- 423
- 115
Siku za hivi karibuni kumetokea habari kuhusu mwanya uliopo kwenye Adobe Acrobat na Adobe Reader ambao unawawezesha mahacker kutengeneza code na kuziweka kwenye mtindo(format) wa pdf huku wakizipamba kwa jina zuuuuri,pindi ufunguapo tu basi imekula kwako kwani hizo code zitajirun na kushusha minyoo na virusi kwenye kompyuta yako itakayomuwezesha hacker kuitawala kompyuta yako bila wewe kujua.
Hii ni hatari mno kwani wengi wetu tumekuwa tukiamini kuwa hauwezi kukutana na virusi au minyoo kwenye faili kama la Adobe.
katika kukabiliana na hili Adobe wametoa ushauri wa kiusalama kwa watumiaji wawe makini katika kipindi hiki wanaendelea kutafuta ufumbuzi wa tatizo.
AfroIT inawashauriwanajamii kuwa makini la hili pia kufuata ushauri uliotolewa na Adobe APSA10-02, Vilevile unaweza kutumia Microsoft's Enhanced Mitigation Toolkit (EMET) ambayo inakuwezesha kujilinda na uvamizi kama huu ambao kwa lugha ya kitaalamu tunauita uvamizi wa siku ya sifuri(Zero-day exploit),hii ikimaanisha mianya ayopatikanika kwenye programu bila mtengenezaji kujua.
Unaweza kupata maelezo ya ziada kwa kutembelea Microsoft Security Research and Defense blog.
Timu nzima ya AfroIT itakuletea update pindi mbalimbali za masuala ya kiusalama.
Hii ni hatari mno kwani wengi wetu tumekuwa tukiamini kuwa hauwezi kukutana na virusi au minyoo kwenye faili kama la Adobe.
katika kukabiliana na hili Adobe wametoa ushauri wa kiusalama kwa watumiaji wawe makini katika kipindi hiki wanaendelea kutafuta ufumbuzi wa tatizo.
AfroIT inawashauriwanajamii kuwa makini la hili pia kufuata ushauri uliotolewa na Adobe APSA10-02, Vilevile unaweza kutumia Microsoft's Enhanced Mitigation Toolkit (EMET) ambayo inakuwezesha kujilinda na uvamizi kama huu ambao kwa lugha ya kitaalamu tunauita uvamizi wa siku ya sifuri(Zero-day exploit),hii ikimaanisha mianya ayopatikanika kwenye programu bila mtengenezaji kujua.
Unaweza kupata maelezo ya ziada kwa kutembelea Microsoft Security Research and Defense blog.
Timu nzima ya AfroIT itakuletea update pindi mbalimbali za masuala ya kiusalama.