Kuvuja kwa Mitihani Tanzania

Mlangaja

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
579
218
Leo tena mitihani ya veta imevuja. Hivi utamaduni wa kuvuja kwa mitihani hapa Tanzania utakwisha lini? Miaka nenda rudi tatizo lipo pale pale. Hivi wahusika wa mitihani huwa wanawajibishwa? Hawa ni watu walioaminiwa na kupewa ofisi na serikali ya Tanzania wasimamie. Hivi wanaposababisha hasara kama hii wanajisikiaje?
Kweli Tanzania ina namna nyingi za ufisadi. Kwangu ufisadi huu wa kuvujisha mitihani ni mbaya mno. Kama taifa lazima tutafute mwarobaini wa tatizo hili. Na kwa kweli wahusika ingefaa wachukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa vizazi vijavyo.
 
Mm nahisi pengine vyombo wanavyowekea vyote vinavuja; ko watafute namna ya kuvikarabati... Sheet hii ndio Tz bhana hatuishiwi mbinu....!!!
 
Mitihani ya maisha huku kwetu imevuja pia. Tz kuna matatizo kweli
 
:p:D:cool::confused::(:mad:
 

Attachments

  • 207833_7b2e4f5c37a2ac7921c63fd42e37010b.jpg
    207833_7b2e4f5c37a2ac7921c63fd42e37010b.jpg
    34.5 KB · Views: 63
Vyuma vimekaza.. Mkulu kaongeza mshahala kidogo... Kinachofuataa hakuna namna... Pesa kwanzaaa...
 
Ni hasara sana kwa Taifa. Vijana wengine wakati wa likizo wanalima ili kujipatia ada, wengine wanafanya kazi kwa vitendo vile wanavyojifunza nk. Kama taifa kuna uozo mwingi sana unapaswa kisafishwa.
 
Back
Top Bottom