Kuuliza si ujinga

Mr.Duttu

Member
Joined
Nov 7, 2015
Posts
91
Reaction score
57
Jamani mimi nahitaji kujua hivi pale Sea Cliff Hotel Masaki bei ya kuingia ni shilingi ngapi pamoja na bei za vinywaji pamoja na chakula kwa ujumla, mwenye experience ya eneo lile anipe detail vizuri.
 
Unataka Ukajitutumue VALENTINE DAY Na Hako Kademu Kako Kanakonuka Jasho Kama Vumba LA Samaki?
 
Jamani mi naitaji kujua ivi pale sea cliff hotel masaki bei ya kuingia ni shngapi pamoja na bei za vinywaji pamoja na chakula kwa ujumla mwenye experience ya eneo lile anipe detail vizur
Inategemea na wewe umejipanga vipi Mr Duttu. Ungeweka bajeti yako pia ingekuwa rahisi kukushauri. Maana pale Sea Cliff kuna restaurant zaidi ya moja ambazo unaweza kupata huduma za vyakula kwa bei nzuri tu.
 
Inategemea na wewe umejipanga vipi Mr Duttu. Ungeweka bajeti yako pia ingekuwa rahisi kukushauri. Maana pale Sea Cliff kuna restaurant zaidi ya moja ambazo unaweza kupata huduma za vyakula kwa bei nzuri tu.
Budget yangu ni kama elfu 80 tuu.
 
Kwa elfu 80 unaweza kwenda Spur pale utapata chakula kizuri na vinywaji kwa watu wawili. Au pia unaweza unaweza kwenda Double Tree ukapate buffet dinner for two very romantic na Upepo wa Bahari mzuri. Unaenda siku ya Wapendanao!?
 
Sea Cliff Village kuna Restaurant moja tu nyamafu wee!!!???? Soma uelewe, ndio maana nilimuuliza budget yake. Alipojibu ana hiyo hela nikamshauri aangalie hizo option mbili zinaweza kumfaa zaidi. Kwenda na familia outing sio issue limbukeni wewe. Umezoea kwenda kula chips kwa wapemba ndio maana unaona ni ujiko. Nisipoenda na familia yangu unataka niende na nani kenge wewe!??
 
Kwa elfu 80 unaweza kwenda Spur pale utapata chakula kizuri na vinywaji kwa watu wawili. Au pia unaweza unaweza kwenda Double Tree ukapate buffet dinner for two very romantic na Upepo wa Bahari mzuri. Unaenda siku ya Wapendanao!?
Spur pale IT plaza?
 
Kwa elfu 80 unaweza kwenda Spur pale utapata chakula kizuri na vinywaji kwa watu wawili. Au pia unaweza unaweza kwenda Double Tree ukapate buffet dinner for two very romantic na Upepo wa Bahari mzuri. Unaenda siku ya Wapendanao!?
Hapana siyo siku ya wapendanao n within this weekend
 
Nimecheka sana kuona mtu unataka kutoka out lakini mfuko wenyewe mwepesi ila unataka mambo mazito. Kuna shemeji yangu mmoja alitoka out na dume wake aliishia kushare burger na juice. Which jamaa ilimuharimu chini ya 5,000. Shemeji alifurahia kutolewa out na mpenzi wake na kujifunza sio kila mwanaume anaishi maisha ya maji yasio size yake.
 
Kula atakula ila kwa mawazo maanake wako wawili........
 
Mbona 80 inatosha kabisa,achenh kumtisha mwenzenu.
 
Kula atakula ila kwa mawazo maanake wako wawili........

Kama hatakunywa pombe, inatosha kabisa kwa wawili.

Light meal for light budget.

Kwenye menu, vipo vyakula vingi, sahani moja 16,000- 20,000 range.

Lakini pombe ndiyo itakuwa shida, Coke watapata.
 
Spur pale IT plaza?
Unaweza kwenda pale IT plaza pia. Ila mimi niliizungumzia ya Sea Cliff Village nikifikiri labda itakuwa convenient kwako kwa masuala ya umbali na usafiri, kwa sababu uliuliza juu ya Sea Cliff Hotel. Kila la heri mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…