IshaLubuva
JF-Expert Member
- Dec 4, 2008
- 250
- 11
Nyingi ya dawa tunazotumia baada ya kupata ushauri wa Tabibu huwa inaelekezwa kuzimeza mara tatu kwa siku kadhaa. Katika kumbukumbu zangu za kupakea maelekezo ya kutumia dawa kutoka kwa Wataalamu wa Afya na hata kwenye matangazo ya dawa yanayotolewa na Redio (za Tanzania na Kenya) neno "Kutwa mara Tatu (au Asubuhi, mchana na jioni)" limekuwa likitumika sana kuwaelekeza wagonjwa namna ya kutumia dawa za kutibu magojwa yanayowasumbua.
Kuna wakati nilijiuliza maana hasa ya kutwa mara tatu ni nini baada ya kukutana na dozi ya aina fulani ya dawa ambapo nilitakiwa kumeza vidonge kadhaa kila baada ya masaa mnane (8). Hapo nikaanza kuhisi suala la kuchanganya lugha kama hivi:
Kwa kiingereza tukisema "day" inaweza kuwa inamaanisha mchana (ambapo kwa kiswahili kingine ni kutwa) au siku nzima ya masaa 24 kwa maana ya mchana na usiku (Kutwa kucha).
Ningependa Wataalamu wa Tiba wanijulishe nini hasa maana ya Kutwa mara tatu; je ni asubuhi mchana na jioni au la?
Kuna wakati nilijiuliza maana hasa ya kutwa mara tatu ni nini baada ya kukutana na dozi ya aina fulani ya dawa ambapo nilitakiwa kumeza vidonge kadhaa kila baada ya masaa mnane (8). Hapo nikaanza kuhisi suala la kuchanganya lugha kama hivi:
Kwa kiingereza tukisema "day" inaweza kuwa inamaanisha mchana (ambapo kwa kiswahili kingine ni kutwa) au siku nzima ya masaa 24 kwa maana ya mchana na usiku (Kutwa kucha).
Ningependa Wataalamu wa Tiba wanijulishe nini hasa maana ya Kutwa mara tatu; je ni asubuhi mchana na jioni au la?