Kutumbua watumishi mnaongoza na makamera, bunge gizani!

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,864
Kuna kiongozi fulani aliyekuwa amezuia fedha za kampeini ya kunawa mikono zisifanye kazi hiyo badala yake zijenge vyoo ktk stend moja wilayani kwake. Nilijaribu kumshauri kwamba fedha hiyo si ya serikali na mara zote wafadhiri hutaka fedha zao zitumike kwa matumizi waliyopanga.

Mkuu huyo wa wilaya hakunielewa akasema "potelea mbali hiki ni kipindi cha uteuzi na ninyi mnanipa sifa. Ntaita TBC hapa nionekane nimetumbua jipu kwa bwana mkubwa"! Tulifungasha virago vyetu na kurudi na wafadhiri wakaamrisha turudishe hela yao.

Lengo langu haikuwa kuwapa kisa hicho bali kuwaonyesha upande wa serikali unavyotumia vibaya vyombo vya habari na hasa chombo cha umma kujitangaza ktk vitu vya 'hovyo' na kuacha maslahi mapana ya nchi. Mbaya zaidi wabunge wa Ccm wako kimya

Hivi ninyi wabunge wa Ccm hamuoni jinsi gani mnaingizwa mkenge na upande wa serikali yenu? Mkuu wa wilaya akitaka kumsimamisha kazi nesi jimboni kwako anawaita TBC anauza sura, we mambo yako uliyofanya jimbo wananchi hawatakiwi kuyaona alafu unagonga meza!
 
Mkuu hata mimi nimeshangaa sana...Nchi ya MAZUZU hii. Ukiwaambia waeleze sababu za kuzuia bunge lisioneshwe livu, hawana majibu.
 
Mkuu hata mimi nimeshangaa sana...Nchi ya MAZUZU hii. Ukiwaambia waeleze sababu za kuzuia bunge lisioneshwe livu, hawana majibu.
Ukondoo wetu utaisha lini? hata wale wanaodhani wananufaika ni waathirika bila wao kujua. Hasa wabunge wa Ccm
 
Rais alishajibu huo uharo. Wacha mafisadi watumbuliwe hadhatani. Kwani bungeni kuna nini cha maana zaidi ya uharo tu?
 
Ukondoo wetu utaisha lini? hata wale wanaodhani wananufaika ni waathirika bila wao kujua. Hasa wabunge wa Ccm
Mlijaribu wakati wa kampeni mkashindwa. Mtaweza sasa? Hivi yule mzee wenu wa kujinyea yupo wapi siku hizi?
 
Rais alishajibu huo uharo. Wacha mafisadi watumbuliwe hadhatani. Kwani bungeni kuna nini cha maana zaidi ya uharo tu?
Bungeni uharo are you serious?Au unatetea ugali wako badala ya maslahi ya taifa kwa ujumla.
 
Ukiona nchi inaongozwa na viongozi wanaotaka au kupenda "media attention" kiongozi au viongozi wa namna hii hawana "vision" (maono) na wako karibu kufikia ukomo wa fikra zao. huwezi kuongoza nchi kwa miaka mitano kwa staili hii lazima wanachi watashtuka tu mbona tunaona viongozi wanasema wanatumbua majipu ilhali maisha yetu yanazidi kuwa magumu.Hivi hivi mwaka utakatika mwanachi hajaona hata kisima cha maji kijijini kwake hapo ndio watajiuliza hivi majipu ni nini?Mwanachi wa kawaida anahiaji huduma bora za afya, maji safi na salama, elimu bora kwa watoto wake, huduma nzuri za fedha ikiwemo mikopo yenye riba nafuu, barabara nzuri, zana za kilimo,uvuvi na huduma nzuri za mifugo, Badala ya serekali kuhangaika na mambo haya wao wamebaki na maigizo ya kuonyesha sura kwenye maruninga utadhani KAOLE.
 
Mnataka wawalimuke mkitoka

Mkirudi mbona awawaonyeshi??
 
Back
Top Bottom