Kutumbua majipu na future ya Tanzania

Robert edo

Member
Mar 9, 2015
44
5
Takribani imepita miezi mi nne tangu awamu ya tano kuingia madarakani na mjadala mkuu inayotikisa kwa sasa ni kile kinachoitwa "kutumbua majibu" wananchi wanashangilia na kuchekelea sana utumbuaji huko, hoja ni kwamba kumng'oa mtu na kumuweka mwingine kwenye taasisi ileile yenye udhaifu mkubwa haitasaidia kuleta mabadiliko.

Mabadiko ya kweli yataletwa na kubadilisha katiba tulionayo kwa kurejea pale ile rasimu ya Warioba hali kadhalika lazima sheria kandamizi zibadilishwe kwani ndizo huchangia vitendo vya ufisadi, mikataba kandamizi, pamoja kuminywa kwa haki za binadamu pamoja na utawala bora.

Tuepuke kuchekelea majibu na badala yake tudai kwa nguvu katiba mpya na kufutwa kwa sheria kandamizi kwa manufaa ya kizazi cha Leo na cha miaka 100 ijayo.
 
Takribani imepita miezi mi nne tangu awamu ya tano kuingia madarakani na mjadala mkuu inayotikisa kwa sasa ni kile kinachoitwa "kutumbua majibu" wananchi wanashangilia na kuchekelea sana utumbuaji huko, hoja ni kwamba kumng'oa mtu na kumuweka mwingine kwenye taasisi ileile yenye udhaifu mkubwa haitasaidia kuleta mabadiliko.

Mabadiko ya kweli yataletwa na kubadilisha katiba tulionayo kwa kurejea pale ile rasimu ya Warioba hali kadhalika lazima sheria kandamizi zibadilishwe kwani ndizo huchangia vitendo vya ufisadi, mikataba kandamizi, pamoja kuminywa kwa haki za binadamu pamoja na utawala bora.

Tuepuke kuchekelea majibu na badala yake tudai kwa nguvu katiba mpya na kufutwa kwa sheria kandamizi kwa manufaa ya kizazi cha Leo na cha miaka 100 ijayo.
Rasimu ya Warioba sio muarobaini wa matatizo yote waliyonayo watanzania
 
Siamini kwenye mkakati wa kutumbuana majipu. Wengi wanaotumbuliwa ni watumishi wa chini wasio na sauti. Wanasiasa wastaafu na watu maarufu wanapewa muda na heshima!
 
Hata kama Katiba ingetoka mbinguni, kama watekelezaji hawajibiki, wazembe, mafisadi, kutokuwa wazalendo, mambo yatabaki kuwa yaleyale!
 
Katiba mpya na hasa mapendekezo ya judge Warioba pamoja na mema yote yaliyomo haikubaliki kwa 7bu utekelezaji wake utakitoa ccm madarakani ie.. kutakuwa na haki na usawa jambo ambalo kinyume chake ndo kimekiweka ccm madarakani
 
Takribani imepita miezi mi nne tangu awamu ya tano kuingia madarakani na mjadala mkuu inayotikisa kwa sasa ni kile kinachoitwa "kutumbua majibu" wananchi wanashangilia na kuchekelea sana utumbuaji huko, hoja ni kwamba kumng'oa mtu na kumuweka mwingine kwenye taasisi ileile yenye udhaifu mkubwa haitasaidia kuleta mabadiliko.

Mabadiko ya kweli yataletwa na kubadilisha katiba tulionayo kwa kurejea pale ile rasimu ya Warioba hali kadhalika lazima sheria kandamizi zibadilishwe kwani ndizo huchangia vitendo vya ufisadi, mikataba kandamizi, pamoja kuminywa kwa haki za binadamu pamoja na utawala bora.

Tuepuke kuchekelea majibu na badala yake tudai kwa nguvu katiba mpya na kufutwa kwa sheria kandamizi kwa manufaa ya kizazi cha Leo na cha miaka 100 ijayo.

Kama mtu ni mwizi lazima uchukuliwe hatua, hio ndio sheria
 
Katiba mpya na hasa mapendekezo ya judge Warioba pamoja na mema yote yaliyomo haikubaliki kwa 7bu utekelezaji wake utakitoa ccm madarakani ie.. kutakuwa na haki na usawa jambo ambalo kinyume chake ndo kimekiweka ccm madarakani
Rasimu ya Warioba ilikuwa ni majanga makubwa! Serikali ya Muungano haina hata ardhi ya kujenga Ofisi, eti mpaka iombe kwa "Nchi Washirika!" CHADEMA/UKAWA sio watu wa kuachia nchi aiseee.....!
 
Rasimu ya Warioba sio muarobaini wa matatizo yote waliyonayo watanzania
Ila muorobaini wa matatizo ya Watanzania ni nini? Ukisema kufanyakazi, humo kwa Warioba kila kitu kimewekwa!
 
Kwa katiba ya sasa hatufiki popote, ufisadi ndio ajenda ya siri ya kila kiongozi.
 
Siamini kwenye mkakati wa kutumbuana majipu. Wengi wanaotumbuliwa ni watumishi wa chini wasio na sauti. Wanasiasa wastaafu na watu maarufu wanapewa muda na heshima!

Wakati mwingine tuache ujinga. Nisamehe sana kwa lugha hii. Mfano mmoja tu, Je aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa Pccb/Takukuru naye ni mtu wa chini chini??? Huyo naye katumbuliwa!!
 
Rasimu ya Warioba ilikuwa ni majanga makubwa! Serikali ya Muungano haina hata ardhi ya kujenga Ofisi, eti mpaka iombe kwa "Nchi Washirika!" CHADEMA/UKAWA sio watu wa kuachia nchi aiseee.....!
Kwani Warioba ni CDM!?
 
Back
Top Bottom