Kutana na mwalimu aliyewapa mimba wanafunzi wanne wa shule ya msingi na mwalimu mkuu alivyomlinda

chinchilla coat

JF-Expert Member
May 16, 2016
5,107
10,969
Mwalimu wa shule ya msingi Busekwa wilaya ya Magu mkoani Mwanza Renatus Mkama anadaiwa kuwabebesha mimba wanafunzi wanne wa shule hiyo kitendo na kuwatelekeza kilichopelekea wanakijiji kutaka kumchomea nyumba mwalimu huyo,



Wanafunzi wa shule hiyo wanadai mwalimu huyo huwaita nyumbani kwake kwenda kumuoshea vyombo kisha ndio huwamalizia hukohuko

Mmoja wa wanafunzi waliobebeshwa mimba na kushindwa kuendelea na masomo licha ya kufaulu darasa la saba ni Mariam Bahati ambaye amezalishwa watoto wawili na kuachwa na anadai hakuwa na maamuzi kipindi hicho
Mwalimu huyo alipohojiwa anadai hizo ni tuhuma tu, Mkuu wa shule hiyo anatuhumiwa kumlinda mwalimu huyo kwa kuondoa majina ya wanafunzi hao katika daftari la mahudhurio kuficha ushahidi na amekiri mwalimu huyo kuwa na tabia hiyo lakini yeye aliidhibiti kwa kumlazimisha kuoa
 
hao wazazi wa hao wanafunzi nao ni tatizo. imawezekanaje binti apewe mimba hadi ajifungue halafu huyo mwalimu anaendelea tu na kazi na kuzidi kufanya ufuska wake badala ya kuwa yuko gerezani? kwani hilo eneo hakuna kituo cha polisi au mahakama hadi waamue kuchoma nyumba yake?
 
hao wazazi wa hao wanafunzi nao ni tatizo. imawezekanaje binti apewe mimba hadi ajifungue halafu huyo mwalimu anaendelea tu na kazi na kuzidi kufanya ufuska wake badala ya kuwa yuko gerezani? kwani hilo eneo hakuna kituo cha polisi au mahakama hadi waamue kuchoma nyumba yake?
VIJIJINI HUKO WATU HAWAJUI SHERIA NA HAKI ZAO, PIA NI WAOGA, HATA KAMA WANAJUA HAWATHUBUTU KUMCHUKULIA HATUA
 
Siku zake zinahesabika! Ila kuna kitu kama hicho kwenye jamii za vijijini...wazazi kama masikini wanaona afadhali aozeshwe yaishe! Nadhani serikali ya wilaya Magu wanapita pita humu watasikia!! .....
 
Hapa nishamuona jamaa yupo mahakamani na mkuu kapoteza kazi kama sio Cheo

Its a matter of Days tu.
 
Wangechoma tu nyumba yake moto maana mpAka sasa Hyo mwalimu hakuna hatua za kisheria amechukuliwa!
 
Hao wazazi hawana uchungu na watoto.
Hao walimu wangeshanyea debe sasa.
 
Back
Top Bottom