Kustaafu kwa CAG Prof. Assad

Iruru

JF-Expert Member
Jan 27, 2014
1,470
2,864
Haraka sana baada ya kusikia hii habari ya CAG Asad kustaafu, cha kwanza sikushangaa na hii ni kwa sababu ya matukio kadhaa yaliyotokea hapo nyuma kati yake na Bunge/Serikali. Pamoja na mabishano mengi ambayo yamekuwepo ya kisheria miongoni mwa watu juu ya kama Prof. Assad alikuwa na haki ya kuteuliwa kwa kipindi cha pili na hii haki iko kikatiba ama kisheria, mimi likanijia wazo hili: Je, kustaafu uCAG kabla ya umri wake wa kustaafu ni nini implication ya hili kwa Assad binafsi? Je, kuna vimafao kidogo vinataka kuminywa hapa tofauti na kama angestaafu uCAG kwa sababu ya umri? Na je, huku kustaafu kwake, anastaafu uCAG tu au na ile kazi yake ya kufundisha pale Chuo Kikuu?

Kwa tabia za meko, pamoja na kutaka kuendelea kuficha kile ambacho asingependa kifahamike hasa matumizi ya pesa za walipa kodi, anaweza pia kuwa anataka kumuumiza Prof. Assad kama namana ya kulipiza kisasi juu yake.
 
Kupitia CV yake iliyowekwa humu jukwaani siku za huko nyuma, inaonesha wazi Prof. Assad ni mwanazuoni aliyebobea! Watu wa aina yake ni dhahabu. Ana uwezo wa kuishi na kufanya kazi na yenye malipo mazuri popote pale duniani.

Hata kama atafanyiwa figisu ili asiirudie kazi yake ya awali, bado nina imani dunia inamhitaji zaidi kuliko sisi tunavyomhitaji.

Prof. hana tofauti na Tido Mhando aliyepigwa figisu na JK baada tu ya uchaguzi mkuu wa 2010 pale TBC! Alipigwa chini kwa zengwe, na TBC ikadumaa moja kwa moja tokea wakati ule! Huku Azam ya miaka michache tu, ikaimarika chini ya uongozi wake makini.
 
Jiwe akitoka madarakani tutasikia mengi sana huenda akawa ndio rais aliyeiba sana kuliko wote.
 
Iruru,
Yawezekana akakosa kila kitu, si unajua meko anavyoongoza Jamhuri kwa matamko na mihemko?
 
Jiwe akitoka madarakani tutasikia mengi sana huenda akawa ndio rais aliyeiba sana kuliko wote
Na pia rais aliyepoteza pesa nyingi zaidi za walipa kodi, ngoja hayo madege yatakapoweka juu ya mawe, watu wananunua ndege kama ng'ombe wa kienyeji...tusubiri...ulizeni Kenya Airways, Air India, Tomas Cook, KLM, American Airlines na magwiji wengine wa anga eti biashara ya ndege ikoje? Mtajua nini kitatokea hapa kwetu.
 
Back
Top Bottom