Kusafilisha matunda nje

Kusafilisha matunda nje

Twin_Kids

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2016
Posts
4,217
Reaction score
5,975
Ni tumaini langu wote wazima.
Naomba mwenye uelewa na hili jambo anifahamishe.
Ni certificate gani inayohitajika,na inatolewa wapi kwa ajili ya kusafilisha matunda nje ya nchi.

Natanguliza shukurani
 
aisee hii process kjwa kweli ni complicated mno mno !kuna vibali si chin ya 4! had uje upimwe udongo mara water contents jaman niligive up !kila la heri nenda kwanza TAHA watakusaidia !
 
TFDA customer care number zao naona zimefungiwa halafu wameziacha tu pale wanashindwa hata ku update namba mpya
 
aisee hii process kjwa kweli ni complicated mno mno !kuna vibali si chin ya 4! had uje upimwe udongo mara water contents jaman niligive up !kila la heri nenda kwanza TAHA watakusaidia !
Matunda na Mbogamboga nyingi/mengi yanayouzwa Gulf Countries yanayotoka Africa hutoka Uganda.

Sisi Tanzania Kila Kiongozi/Sera zetu anachangia/zinachangia Umasikini wa raia na maisha kuwa magumu zaidi...

Na Jana Pogba ndo anaomba Watanzania wavumilie tu, mpaka lini.

Ili hari kama tungebadirisha Sera zetu, kuondoa urasimu tungebadirisha hari za watu wetu.

Roho imeniuma ulishindwa kufanya biashara kwa sababu ya sera mbovu na ukiritimba wa Viongozi na wafanyakazi wa umma.

Na hakuna anayejari.
 
Matunda na Mbogamboga nyingi/mengi yanayouzwa Gulf Countries yanayotoka Africa hutoka Uganda.

Sisi Tanzania Kila Kiongozi/Sera zetu anachangia/zinachangia Umasikini wa raia na maisha kuwa magumu zaidi...

Na Jana Pogba ndo anaomba Watanzania wavumilie tu, mpaka lini.

Ili hari kama tungebadirisha Sera zetu, kuondoa urasimu tungebadirisha hari za watu wetu.

Roho imeniuma ulishindwa kufanya biashara kwa sababu ya sera mbovu na ukiritimba wa Viongozi na wafanyakazi wa umma.

Na hakuna anayejari.


Kweli kabisa mkuu. Wataalam wa kusaidia uhamasishaji wa hizi biashara wanaishia kufanya maonyesho mnazi mmoja tu.

Tazama rutuba iliyozunguka nchi yetu lakini huwezi kwenda kijijini ukakuta wanakijiji wamepimiwa udogo wao na wakaambia udongo wao unafaa kwa kilimo mfano Red cabbage. HAKUNA KITU KAMA HIKI TANZANIA

Utaalam umewekwa kwenye vitabu vinauzwa town na watanzania hata kusoma gazeti ni wavivu ukiachilia mbali hiyo idadi ya wanaojua kusoma na kuandika. Utaratibu wa kupata vibali na kufuata utaratibu kwa wanaothubutu umejaa ukiritimba , usumbufu, urasimu na kukatisha tamaa kabisa. Mbali na hayo pesa inatakiwa itumike kuvipata bila kusahahu kupoteza muda mrefu sana na nguvu nyingi zinapotea.

Wako wapi wahitimu wa soil kutoka SUA na kwingineko. Nani anawaajiri nani anawatumia? Sio soil tu bali pia wataalam wote wa KILIMO BIASHARA.

Watanzania bado hatujui kulima kabisa utadhani ni nchi isiyo na udongo mzuri ni mfano wa nchi yenye ardhi iliyopigwa mabomu na kuharibika sasa haifai kwa kilimo . Na sasa tunakimbilia kwenye viwanda tena viwanda vyenyewe tunavihesabu kuanzia level ya vyerehani vitatu.

Nchi hii inachosha sana ndio maana wakazi wengi wa nchi wameishia kupiga viroba tu maarifa yameisha kwenye nguvukazi ya kijana wa sasa. Wanahitaji msaada wa kuwakwamua kuingia kwenye KILIMO BIASHARA . Wengi wamehitimu kazi hakuna wengi hawajaenda shule kabisa na nguvu wanazo

Na kichwa ngumu kapewa fimbo anatandika wimbo wa VIWANDA tu. Hana habari nani anaitikia na haitikii yeye anaimba tu kwa masauti ya kutisha na kuogofya.

Kilimo cha biashara sifuri kiwanda kitapata nini? Waganda wanakausha hadi ndizi , samaki na maparachichi wana export tazama sisi.
Viwanja vya ndege vinaboreshwa ili kubeba watu tu. Ardhi yetu tumeikalia inakaa bure kabisa. Natmani kufikiria kuwa hali ya hewa ya Tukuyu inaweza kuotesha aina flan ya maua uoe uwanja wa songwe ukatumika vizuri . Ila nani wa kufanya hayo. Wote tumeketi mkao wa kusbiri VI-WONDER .
VIWANDA myfoot [emoji21][emoji21]
 
Matunda na Mbogamboga nyingi/mengi yanayouzwa Gulf Countries yanayotoka Africa hutoka Uganda.

Sisi Tanzania Kila Kiongozi/Sera zetu anachangia/zinachangia Umasikini wa raia na maisha kuwa magumu zaidi...

Na Jana Pogba ndo anaomba Watanzania wavumilie tu, mpaka lini.

Ili hari kama tungebadirisha Sera zetu, kuondoa urasimu tungebadirisha hari za watu wetu.

Roho imeniuma ulishindwa kufanya biashara kwa sababu ya sera mbovu na ukiritimba wa Viongozi na wafanyakazi wa umma.

Na hakuna anayejari.
~

asante mkuu
 
nilisumbuka mie sin ht hamu

Nimefungua corner nauza maziwa fresh na mgando kutoka shambani kwangu sijasindika nauzia wapita njia kwa kipimo cha glass moja moja . . Juzi kati hao TFwereva wakapita wakakuta kijana kavaa safi kabisa apron yake na kofia wakaanza mikwara iko wapi leseni ya TFwereva. Can you imagine? Nilipoambiwa nikashangaa maana nilienda ofisini kwao kabisaa wakaniambia kwa kuwa sifanyi usindikaji sihitaji leseni kutoka kwao. Yaani hawa TFDA pasua kichwa
 
Nimefungua corner nauza maziwa fresh na mgando kutoka shambani kwangu sijasindika nauzia wapita njia kwa kipimo cha glass moja moja . . Juzi kati hao TFwereva wakapita wakakuta kijana kavaa safi kabisa apron yake na kofia wakaanza mikwara iko wapi leseni ya TFwereva. Can you imagine? Nilipoambiwa nikashangaa maana nilienda ofisini kwao kabisaa wakaniambia kwa kuwa sifanyi usindikaji sihitaji leseni kutoka kwao. Yaani hawa TFDA pasua kichwa



duh !sasa ikawaje !aisee ukiritimba umezidi
 
Back
Top Bottom