Kura yangu si ya majaribio…!!!

Kura yangu si ya majaribio…!!!

Dupe

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2013
Posts
1,668
Reaction score
813
Watanzania wenzangu habari zenu za asubuhi…!!!

Baada ya kutafakari kwa kina juu ya hatma ya uchaguzi huu wa October 25 2015 nimeamua kuja kuwasihi wananchi wenzangu tutambue kuwa kura zetu si za majaribio…!!

Tusikae kujidabganya eti ngoja nimjaribu huyu uenda kajirekebisha ilo kosa kubwa kwenda kumjaribia kiongozi ambae atakaa miaka 5 akikuumiza tu…!!

Watanzania tulishaambiwa njia hii inasimba…!!! Nasi twajua njia hiyo inasimba, je utafanya majaribio ya kupita eti ukijiongopea uweza simba kalala uenda asinione?

Naomba tutafakhari kwa mapana watanzania juu ya hatma ya taifa na simba ni simba tu hawezi geuka mbuzi, tusipige kura kwa majaribio, tutafalhari kwa mapana yake tuangalie nyuma then angalia mbele alafu uchukue maamuzi sahihi…!!!

EWE MTANZANIA, TUMIA HAKI YAKO OCTOBER 25 KUMPATA KIONGOZI BORA NA SIO BORA KIONGOZI… TAKE CARE
 
aliekutuma mwambie amechelewa hapa edo tuu
 
Watanzania wenzangu habari zenu za asubuhi…!!!

Baada ya kutafakari kwa kina juu ya hatma ya uchaguzi huu wa October 25 2015 nimeamua kuja kuwasihi wananchi wenzangu tutambue kuwa kura zetu si za majaribio…!!

Tusikae kujidabganya eti ngoja nimjaribu huyu uenda kajirekebisha ilo kosa kubwa kwenda kumjaribia kiongozi ambae atakaa miaka 5 akikuumiza tu…!!

Watanzania tulishaambiwa njia hii inasimba…!!! Nasi twajua njia hiyo inasimba, je utafanya majaribio ya kupita eti ukijiongopea uweza simba kalala uenda asinione?

Naomba tutafakhari kwa mapana watanzania juu ya hatma ya taifa na simba ni simba tu hawezi geuka mbuzi, tusipige kura kwa majaribio, tutafalhari kwa mapana yake tuangalie nyuma then angalia mbele alafu uchukue maamuzi sahihi…!!!

EWE MTANZANIA, TUMIA HAKI YAKO OCTOBER 25 KUMPATA KIONGOZI BORA NA SIO BORA KIONGOZI… TAKE CARE
Mkuu mbona hueleweki...unahangaika weeeee..unazunguka weeee.....nikwambie tu Lowasa tutamchagua wewe chagua ulichokiamini...Kura za majaribio ni lazma kila jambo linamwanzo wake...ccm haikujiingiza tu yenyewe ilipigiwa kura wakijipa moyo kwamba ngoja tuwape tena wenda mambo yakawa safi

Lkn kadiri wanapopigiwa kura nakuaminiwa nivyo walivyozidi kuwa mazuzu,uwizi wa wazi kabisa unafanyika,ghiliba kejeli dharau nk..Hatma ya Serikali yeyote ipo kwa wapiga kura.kwanza tunajaribu na km inavutia basi tunaiacha...ikiboronga tunaiondoa kwa system ile ile tuliyoiingiza nayo....sasa we unakuja na porojo zako hapa za kigamba gamba bila kutambua ni kizazi gani unachoteta nacho...wezi nyinyi.. uploadfromtaptalk1441341170480.jpg
 
Tumeshabaribu miaka 50 imeshindikana kwahivyo hakuna ubaya wa kujaribu kwingine kwa miaka mitano..Lowassa atosha
 
Hakuna kura ya majaribio ,mwaka huu kuna maamuzi magumu ambayo Watanzania wanataka kuyapitisha ,kama ni kujaribu wamesharibu zaidi ya miaka 50 na ahadi walizokuwa wakipewa ni zilezile na sasa wamegundua tatizo sio mtu tatizo ni mfumo mzima wa Chama tawala ,mfumo ambao umejikita katika umimi,usisi mimi na mwanangu na jamaa yangu ,na zaidi kulindana,wewe kama humo basi utakuwa mwenye kusubiri saaaana.

Mwaka huu wananchi wa taifa hili la Tanzania majaribio yao wanayahamisha ,hivi umeshajaribu kwa miaka hamsini na kujenga tamaa na matumaini bado unaenda kujaribu hukohuko kama utakuwa huna wazimu utakuwa na kitu gani ?
 
Mleta mada nimekuelewa vzr,Ni bora upite njia yenye simba mmoja kuliko kupita njia yenye SIMBA 100.Mh edo anasemwa kwa richmond!Ni sawa alikuwa waziri mkuu na vipi kuhusu hawa
Dowans
Meremeta
Mikataba mibovu ya gesi na mafuta
Ndege ya rais
Buzwagi
Maji safi na salama
NIMEWEKA KWA UCHACHE TU,YAPO MENGI NAWE WAJUA.NI BORA TUMCHAGUE EDO KWAN YEYE ATAONGOZWA NA CHAMA NA SIO JPM AMBAYE ANATAONGOZWA NA MFUMO NA SHIDA ILIYOPO NI KULE KWA JPM KILA KITU KIPO MEZAN KWAMBA UKIWA RAIS MWANANGU MPE SEKTA YA MADIN USIMSAHAU HUYU MPE UWAZIR WA FEDHA N.K
NJOO HUKU MLETA MADA ACHANA HAO WALIOTUONGOZA TOKA UHURU LAKINI HALI NI MBAYA KILA KONA NA USIWE NA UPOFU WA KILA SIKU UNAMSEMA MTU KWA KOSA MOJA ILO WATOTO WA PWANI WANALIITA NI GUBU.MBONA SWALA WETU WAMETOLOSHWA WENGI TU NA WALA HAUJALIVALIA NJUGA??MBONA TEMBO WETU WANAULIWA KILA LEO NA WALA HAUJAPIGA KELELE?
n.b;Hakuna msafi ndani ya ccm na ndio maana ninafananisha na ukoo wa panya!
 
kitu kimoja tunakosea watanzania ni kujadili backgrounds za watu instead ya wanavyovisimamia sasa katika ilani zao . Chaguamtu atakaye simamia katiba bora katiba nzuri ndio uongozi na utawala bora tukumbuke ata tulie vipi ela zetu tulizoibiwa richmond aziwezi rudi kwani sheria airuhusiwa kufilisi mtu pia nyumba za serikali zilizouzwa kwa bei ya mboga aziwezi rudi pia na ata deni la bilioni 900 lililotokana na ucheleweshaji wa malipo ya mkopo katika wizara ya ujenzi na bilioni 45 za mradi wa maji monduli zote aziwezi rudi . Wangapi mnajua hizo fedha za kujenga viwanda zitatoka wapi kama si kwa kukuza deni la nchi na je tutasomaje bure wakati ata madawati atuna mashuleni tujadili mambo ya msingi aya mengine tuyaache backgrounds kila mtu anayo mbaya duniani nobody is perfect compare sasa hizo bilioni 900 kutokana na uzembe na hizo bilioni 150 kutokana na richmond
 
Mjasiriamali wa ukweli haogopi matokeo ya uamuzi wake (risk taker)

Edo Lowassa mbele kwa mbele, Viva UKAWA
 
Ni kweli kabisa, njia ya ccm imekuwa na simba wengi na wamezaliana kwa miaka 54, inatupasa sio kupiga kura ya majaribio bali kura ya mabadiliko.
 
Hawa jamaa wakiwa wanataka kitu huwa wanajivesha huruma kweli na kujifanya binadamu ngoja washike mpini ndo mtawajua wao nani! Tuliwaona bunge la katiba walivyokuwa na kiburi, dharau ghiliba na kejeli nachofurahia huku uswahilini watu washaelewa bado wachache sana ambao tatizo lao kubwa ni hofu
 
nkwel siwezi kujaribu kwa ccm kwamba magufuli anaweza badilika. kama ukawa kua na wabunge tu tumeweza jua mengi kura kwa lowasa na wabunge wa ukawa miaka zaidi ya 50 nchi imewashinda atujaribu tena kwani tuna taka viongozi saivi. na so viongozi tulowachoka katika mfumo uliochoka na mfumo uliojaa rushwa. amina
 
Nakumbuka hii post mpaka nacheka yani … nilishasema watanzania tusijaribie kiongozi kwa maana ata yesu alijaribiwa na shetani akiambiwa kama kweli we ni mwana wa Mungu basi jirushe kwenye mnara huu na Baba yako atatuma malaika waje kusaidie usiumie na Yesu akamjibu kuwa Mungu hajaribiwi …!!

Nashukuru watanzania kwa kunielewa
 
Back
Top Bottom