Kupuuza migogoro ya ardhi nchini ni kutamia bomu

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Aug 12, 2011
7,140
14,678
Migogoro ya ardhi hapa nchini imekithiri na imefikia hatua ya umwagaji damu.
Migogoro hii imegawanyika katika makundi mawili; wakulima na wafugaji na wananchi na wawekezaji.


Migogoro hasa ya wananchi na wawekezaji ambayo imechukua sura mpya na inaleta tafsiri kuwa serikali yetu kuwa siyo ile ya 'mgeni njoo mwenyeji apone', bali mgeni njoo mwenyeji asulubike.

Katika maeneo mengi hapa nchini, tayari kumeshatokea uvunjifu wa amani uliosababisha damu kumwagika na hata kutokea vifo. Vurugu hizi zimetokea hata kwenye maeneo ambayo udugu na kuvumiliana vilitawala na hakuna mtu aliyedhani zingeweza kutokea. Hata hivyo, bado sizioni jitihada za haraka za kumaliza migogoro hii ambazo zimeshachukuliwa na serikali yetu.

Badala yake najionea hatua za kujaribu kuahirisha matatizo haya jambo linaloweza kutuletea maafa makubwa baadaye.
 
Ni kweli tunaatamia bomu, nakumbuka niliwahi kusoma makala yako moja kuhusu ripoti ya Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za ardhi – HAKIARDHI ya January 30, 2009, iliyoonyesha hali halisi ya migogoro ya ardhi jinsi ilivyokithiri hapa nchini, ambapo inaonekana kuwa migogoro ya ardhi kati ya makundi mbalimbali ya watumiaji imekuwa ikiongezeka kila kukicha.

Vipi kuhusu ripoti hiyo hudhani kama ikifuatwa itasaidia kupunguza migogoro hii?
 
Ni kweli tunaatamia bomu, nakumbuka niliwahi kusoma makala yako moja kuhusu ripoti ya Taasisi ya Utafiti na Utetezi wa Haki za ardhi – HAKIARDHI ya January 30, 2009, iliyoonyesha hali halisi ya migogoro ya ardhi jinsi ilivyokithiri hapa nchini, ambapo inaonekana kuwa migogoro ya ardhi kati ya makundi mbalimbali ya watumiaji imekuwa ikiongezeka kila kukicha.

Vipi kuhusu ripoti hiyo hudhani kama ikifuatwa itasaidia kupunguza migogoro hii?
Wa kuifuata ripoti hiyo nani, serikali hii?
 
Back
Top Bottom