Kupokea simu ya Mpenzi/Mwenza pale inapokuwa karibu yako ni ruksa?

AshaDii

Platinum Member
Apr 16, 2011
16,190
18,078
Habari wana JF,

Kwanza nifurahi kwamba nipo miongoni mwenu na haswa katika kuwasilisha suala ambalo kila mmoja wetu linamgusa kwa namna moja au nyingine.

Mimi ni mdau wa MMU, napenda yale yote yanayohusisha mapenzi na mahusiano kwa namna moja ama nyingine. Leo hii ningependa tushirikiane katika kujadili mawasiliano kwa njia ya simu, pale inapohusisha mtu wa kati. (3rd party)

Kila mmoja ana maoni yake ya kupokea simu na yapo katika makundi haya:-

1. Kuna wanaokataa kwamba si sahihi

2. Kuna wanaokubali ni sahihi

3. Kuna wanaosema si sahihi hadi pale panapokuwa na sababu za msingi

Naomba kufahamu kutoka kwenu wana JF, mna msimamo upi na kwasababu zipi?

Tukumbuke, hii inaweza kutusaidia katika maamuzi na tafakuri kwa kila mmoja wetu inapokuja changamoto kama hii.

Msimamo wangu: Sina shida simu ikipokelewa na mtu ambaye sikutarajia wala sina shida shemeji yenu kupokea simu yangu.

Pamoja Saana!
 
Leo mvua itanyesha humu ndani.. AshaDii umerudi?! Welcome Back The Legend..

Tukiwaona wakongwe mnarejea kama hivi tunapata amani... MMU siku hizi kuna wahanga wengi wa mapenzi, vilio kila kukicha... Stress tupu.. Bora mrudi tu mwokoe jahazi!

Back to the topic..

Mimi ninadhani kupokea simu ya mtu ni vyema iwe kwa ruhusa yake... Awe mpenzi, asiwe mpenzi..
 
Simu ya mwenzako sometimes ni kama kitunguu.

Unapokuwa unakata kitunguu machozi lazima yatakutoka tu.

Mathalani kwetu wanaume, simu ya mwenzi wako inaweza kuwa na msg za kutongozwa...au akawa anapigiwa kutongozwa...unapokea kisha utalianzisha tu.

Stop it.
 
Simu ya mwenzako sometimes ni kama kitunguu.

Unapokuwa unakata kitunguu machozi lazima yatakutoka tu.

Mathalani kwetu wanaume, simu ya mwenzi wako inaweza kuwa na msg za kutongozwa...au akawa anapigiwa kutongozwa...unapokea kisha utalianzisha tu.

Stop it.
Kama mimi moyo wangu ndio mwepesi kabisa yaani..
Kuna kipindi nilikuwa nforwadiwa tu screenshots za mitongozo na mamsup nikamwambia stooop.. Maana moyo ulikuwa unaenda alijojo..
Stay away from simu ya mpenzi!
 
Kuitwa simu ya mkononi kunaendana na umiliki (here i mean Privacy) wa mwenye nayo.. Kuingia kwenye ndoa na kuwa mwili mmoja bado hakuhalalishi kuingilia kwenye upokeaji wa simu ya mkononi ya mmoja wapo katika hiyo ndoa..

So sio vizuri kimaadili, kikanuni kimaisha, kiutawala, kiutemi kupokea simu ya mkononi ya mwenzi katika ndoa au mahusiano bila ya ridhaa..
 
~~~>>>Msimamo wangu:

Naruhusu simu yangu kupokelewa na mke wangu na ye pia napokea simu zake.

Sababu:
#1. Mke ni mshauri wangu mkuu.... Hivyo sidhani kama kuna Jambo la kumficha ama kunificha .....

#2. Ni vyema nikapokea simu zake ili kama ana Uchafu wake niutambue mapema ili niweze kuchukua maamuzi mapema.. Kuliko kuhofia kuishika simu yake kwa kuhofia kuyajua anaowasiliana nayo.
 
Kabisa....
Leo mvua itanyesha humu ndani.. AshaDii umerudi?! Welcome Back The Legend..

Tukiwaona wakongwe mnarejea kama hivi tunapata amani... MMU siku hizi kuna wahanga wengi wa mapenzi, vilio kila kukicha... Stress tupu.. Bora mrudi tu mwokoe jahazi!

Back to the topic..

Mimi ninadhani kupokea simu ya mtu ni vyema iwe kwa ruhusa yake... Awe mpenzi, asiwe mpenzi..
 
Habari wana Jf,


Kwanza nifurahi kwamba nipo miongoni mwenu na haswa katika kuwasilisha suala ambalo kila mmoja wetu linamgusa kwa namna moja au nyingine.

Mimi ni mdau wa MMU, napenda yale yote yanayohusisha mapenzi na mahusiano kwa namna moja ama nyingine. Leo hii ningependa tushirikiane ktk kujadili mawasiliano kwa njia ya simu, pale inapohusisha mtu wa kati. (3rd party)

Kila mmoja ana maoni yake ya kupokea simu na yapo katika makundi haya:-

1. Kuna wanaokataa kwamba si sahihi

2. Kuna wanaokubali ni sahihi

3. Kuna wanaosema si sahihi hadi pale panapokuw na sababu za msingi

Naomba kufahamu kutoka kwenu wana Jf, Mna msimamo upi na kwasababu zipi?

Tukumbuke, hii inaweza kutusaidia ktk maamuzi na tafakuri kwa kila mmoja wetu inapokuja changamoto kama hii.

Msimamo wangu: Sina shida simu ikipokelewa na mtu ambaye sikutarajia wala sina shida shemeji yenu kupokea simu yangu.


Pamoja Saana!
Asee....!! Ndio wewe au kuna mtu kaazima account yako. Karibu mkuu

Suala la mtu kupokea simu isiyokuwa yake sio sawa hata kidogo na ndio maana ikaitwa cellular phone. Yaani labda kama kuna ulazima saaana hata kama ni mpenzi wako.
 
Interest.

Nashukuru for the acknowledgement. I am humbled. Nafurahi kurudi pia.

Nakubaliana na wewe. Na ndiyo maana kuna umuhimu wa kuwa makini katika maamuzi ya mahusiano na mtu ulo nae na kujenga msingi wa heshima.

Kama anakujeshimu hadi kapokea ina maana hiyo ni simu ambayo haina madhara ama implication yoyote. Inapotokea anataka kuweka mazoea ya kila mara shida ndiyo hapo.


Leo mvua itanyesha humu ndani.. AshaDii umerudi?! Welcome Back The Legend..

Tukiwaona wakongwe mnarejea kama hivi tunapata amani... MMU siku hizi kuna wahanga wengi wa mapenzi, vilio kila kukicha... Stress tupu.. Bora mrudi tu mwokoe jahazi!

Back to the topic..

Mimi ninadhani kupokea simu ya mtu ni vyema iwe kwa ruhusa yake... Awe mpenzi, asiwe mpenzi..
 
Huna haja ya kupokea sim ya mtu.

Binafsi sijawahi kupokea au kusoma sms.

Note: kwa wapenzi ukiona no inaita zaidi ya mara 5 sio buree mara nyingi anakuwa ni mchepuko wake. Hapa chaguo ni lako kupokea au kupotezea
 
Mwenza wangu ana uhuru na simu yangu 100%, anaweza kuchukua kuangalia kilichomo kwenye simu, kupokea simu yangu kama nipo mbali na kunipatia ujumbe, anaweza kusoma sms zangu n.k

In short, hatujawekeana mipaka kwenye simu zetu, sioni mantiki ya kuishi na mtu, mnafanya mengi ya sirini ila tatizo liwe kwenye uhuru wa simu.
 
Back
Top Bottom