Kuondoa kodi kwenye malighafi ya mawese ni ufisadi

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,402
4,064
Katika muendelezo wa kuwabeba mafisadi au kuwa watumwa wa wawekezaji uchwara, Serikali kupitia budget ya 2009/10 wanataka kutoa msamaha wa kodi kwa semi-refined oil hususana ya mawese kutoka nje kama malighafi wakati tunayo alizeti ambayo nyingine huishia mashambani au kuozea kwenye ghala.

Kama huyo mwekezaji anaona mafuta ya mawese ni mali kwanini asilimishe hayo mawese Kigoma na kutoa ajira hapa hapa nyumbani? au ndio hivyo uchaguzi unakaribia hivyo hela ya kukwepa kodi kwenye hiyo raw material ndio mafisadi watakapopitia na kupata mitaji ya kuwekeza kwenye mabenki yao na biashara nyinginezo wakati wananchi wanahitaji hiyo kodi kwa ajili ya zahanati, shule na barabara?
 
Naomba Watanzania na Wah. Wabunge wenye uchungu na Taifa letu msiishie kujadili suala la NGO's na Mashirika ya Dini kufutiwa misamaha, chonde chonde jamani suala la kuondoa ushuru kwenye mafuta ghafi ya mawese na kupunguza ushuru unaotozwa kwenye nguo za mitumba yahojiwe kwa kina na ikiwezekana Mkulo alazimishwe kurejesha kodi hizo kama ilivyokuwa awali.

Kwa taarifa tu ni kuwa hakuna mafuta ghafi yanayoingizwa nchini kutoka nje ila mafuta yanayoletwa ni yala ambayo yamekuwa refined na wanachofanya wajanja hawa ni kujaza kwenye madumu na kuuza tu. No value addition na hakuna ajira inayopatikana kwa njia hiyo ila athari kubwa iko kwenye uchumi wetu hususani wakulima ambao kila siku tunaimba wimbo wa kuwainua pasipo vitendo. Msimamo ulikuwa ni kuendelea kutoza ushuru wa 10% kwa mafuta ghafi yanayoagizwa kutoka nje, sijui uamuzi wa kufuta umetoka wapi ama ni maamuzi binafsi ya Mkulo.

Suala la kupunguza ushuru kwenye mitumba naona nalo limekaa vibaya. Lengo hasa la kupunguza ushuru kwenye mitumba ni nini? Ama kuna wajanja wanataka kuingiza mazagazaga yao kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu. Je! uamuzi huu unaendana na azma iliyopo ya kuinua viwanda vya ndani pamoja na wakulima wa pamba ama kuna ajenda ya kuendelea kuwamaliza wakulima pamoja na viwanda vichache tulivyonavyo? Waungwana naomba tuyaangalie haya mambo kwa upana zaidi, something fishy is behind this!
 
Last edited:
hili li serikali letu mpaka linatia kichefuchefu, tulidhani vijana wangefanya tofauti lakini kumbe na wao ni watoto wa mafisadi. Sasa mkulo ndo wale wazee wa 47 tutegemee nini? nauwaziri kapewa kwa ushemeji? Mimi najipa imani tu kwamba ipo siku haya yote yatakuwa historia japo si kizazi hiki!!
 
Back
Top Bottom