Chabrosy
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 2,636
- 3,162
Ukoloni ukiuweke kwa mwanamke mtadumu sana Mura.Binafsi nilikua mwepesi sana wa kumuomba msamaha mpenzi wangu hasa pale nilipokua na uhakika kwamba mimi ndie niliesababisha tafrani na wakati mwingine hataka kama kosa sio langu nilijishusha ili tu maisha yaendelee kama kawaida....kuna wakati nilikua siwezi pitisha wiki bila ya kumsemesha mwenzi wangu pindi tunapikua tumekosana.....nadhani mwenzangu alikariri vibaya na aakachukulia kama mimi dhaifu sana...baada ya kuona hivyo nikasema sasa ngoja nimuoneshe huyu mwanamke kwamba mimi ni mwanaume kamili na nina misimamo yangu....ilifika wakati nikawa naweza kukaa hata mwezi mzima bila kumcheki na maisha yakawa yanaenda kama kawaida....yeye ndio akawa anahangaika kunitafuta baada ya kuona kimya kingi kila tunapokosana
Nihitimishe tu kwa kusema kwamba, tunapokua kwenye mahusiano tuache mambo ya kutingishiana kiberiti mana hujui ni siku gani mwenzi wako atakua amechoka kabisa vituko vyako hata kama anakupenda kiasi gani.
121.