UNACHUKUA HATUA GANI UNAPOMKOSEA MPENZI WAKO?
Kwenye maisha hakuna binadamu mkamilifu, kila mtu anamadhaifu yake, madhaifu haya ndiyo husababisha watu kutofautiana, kukoseana.
. Unafanya nini mara baada ya kuona mwenzio hajaridhika, umekosea na umemkosea? 
Nadhani ni vema kuomba msamaha, hapa naongea na wanaume, kwa mwanamke ni rahisi kuomba msamaha lakini ni aghalabu sana kwa wanaume kufanya hivyo, nadhani panahaja ya kukumbushana, wala si dhambi, baba omba msamaha umkoseapo mwenza wako.
Kuomba msamaha ni ibada tosha, ni hekima na ni jambo la heshima kwa mkeo, ni kumpa heshima mwenza wako nafsini, hata Mungu anakubariki uombae msamaha. Ni rahisi sana, tamka "nisamehe".
Ukishaomba msamaha, mzigo unabaki kwa muombwa, unabaki kwa uliyemuomba, aruhusu wepesi moyoni mwake ama la, na hakika anapokusamehe yeye pia hupata Thawabu mbele ya Mungu, "Yatupasa kusamehe". Samehe bila kuhesabu ni mara ngapi umekosewa, utabarikiwa sana.
Nakusihi kijana, Baba, usiruhusu mwenza wako achukie bila kumtaka radhi, haijalishi ni namna gani ulihusika kwenye tukio, omba msamaha, tafuta amani, ni upendo huu.
Sawa umetengana na mkeo, ulichukua hatua gani kabla ya mwenza wako hajakuzira na kughadhabika moja kwa moja? Ulifanya jitihada gani kunusuru uhusiano wenu? Hukutaka hata kuomba radhi? Heshima yake iko wapi!!?
Akiondoka na ihali ulijishusha ,ukampandisha yeye kwa kumuomba msamaha, kila kitu utakiacha mikononi mwake, akusamehe ama akache, ni juu yake, wajibika kwa kuomba msamaha, nusuru penzi lako kwa kuomba msamaha kwa mwenza wako.
Utaoa mara ngapi, utabadirisha mara ngapi? Jifunze kuendeleza uhusiano wako, jifunze kuwa mwanaume kamili bila kuendekeza kiburi ama dharau kwa mwenza wako, ndoa ni Baraka !
Umeombwa msamaha, bado unajawa na kiburi, chuki, wala hutaki kumpa nafasi mwenza wako! Unataka afanye nini kunusuru uhusiano wenu? Haipaswi kuhesabu idadi ya misamaha, hata wazaz wetu walipitia njia hizi ndefu, na ndiyo maana wapo pamoja mpaka sasa! Ukiombwa msamaha ruhusu nafsi yako ipumue, samehe.
Unakataa kutoa msamaha na kukatisha uhusiano ! Kwa kosa la namna gani!? Utampata wapi huyo unayemwita ni mkamilifu ? Zaidi utaishia kubadirisha vitanda na nyumba ! Nakukumbusha kutoa msamaha....
Unajua maana ya mwenzio kukuomba msamaha? Akikuomba, ukakengeuka, naye atageuka, atateseka na mwisho wa siku atazoea na huwezi kuja kupata nafasi tena moyoni mwake, tusamehane.
Tuombane msamaha, tutoe msamaha, tusamehane saba mara sabini.
Na;
Ambangile, B
Instagram, ambangile_b
Kwenye maisha hakuna binadamu mkamilifu, kila mtu anamadhaifu yake, madhaifu haya ndiyo husababisha watu kutofautiana, kukoseana.
. Unafanya nini mara baada ya kuona mwenzio hajaridhika, umekosea na umemkosea? 
Nadhani ni vema kuomba msamaha, hapa naongea na wanaume, kwa mwanamke ni rahisi kuomba msamaha lakini ni aghalabu sana kwa wanaume kufanya hivyo, nadhani panahaja ya kukumbushana, wala si dhambi, baba omba msamaha umkoseapo mwenza wako.
Kuomba msamaha ni ibada tosha, ni hekima na ni jambo la heshima kwa mkeo, ni kumpa heshima mwenza wako nafsini, hata Mungu anakubariki uombae msamaha. Ni rahisi sana, tamka "nisamehe".

Ukishaomba msamaha, mzigo unabaki kwa muombwa, unabaki kwa uliyemuomba, aruhusu wepesi moyoni mwake ama la, na hakika anapokusamehe yeye pia hupata Thawabu mbele ya Mungu, "Yatupasa kusamehe". Samehe bila kuhesabu ni mara ngapi umekosewa, utabarikiwa sana.
Nakusihi kijana, Baba, usiruhusu mwenza wako achukie bila kumtaka radhi, haijalishi ni namna gani ulihusika kwenye tukio, omba msamaha, tafuta amani, ni upendo huu.

Sawa umetengana na mkeo, ulichukua hatua gani kabla ya mwenza wako hajakuzira na kughadhabika moja kwa moja? Ulifanya jitihada gani kunusuru uhusiano wenu? Hukutaka hata kuomba radhi? Heshima yake iko wapi!!?

Akiondoka na ihali ulijishusha ,ukampandisha yeye kwa kumuomba msamaha, kila kitu utakiacha mikononi mwake, akusamehe ama akache, ni juu yake, wajibika kwa kuomba msamaha, nusuru penzi lako kwa kuomba msamaha kwa mwenza wako.
Utaoa mara ngapi, utabadirisha mara ngapi? Jifunze kuendeleza uhusiano wako, jifunze kuwa mwanaume kamili bila kuendekeza kiburi ama dharau kwa mwenza wako, ndoa ni Baraka !

Umeombwa msamaha, bado unajawa na kiburi, chuki, wala hutaki kumpa nafasi mwenza wako! Unataka afanye nini kunusuru uhusiano wenu? Haipaswi kuhesabu idadi ya misamaha, hata wazaz wetu walipitia njia hizi ndefu, na ndiyo maana wapo pamoja mpaka sasa! Ukiombwa msamaha ruhusu nafsi yako ipumue, samehe.

Unakataa kutoa msamaha na kukatisha uhusiano ! Kwa kosa la namna gani!? Utampata wapi huyo unayemwita ni mkamilifu ? Zaidi utaishia kubadirisha vitanda na nyumba ! Nakukumbusha kutoa msamaha....

Unajua maana ya mwenzio kukuomba msamaha? Akikuomba, ukakengeuka, naye atageuka, atateseka na mwisho wa siku atazoea na huwezi kuja kupata nafasi tena moyoni mwake, tusamehane.
Tuombane msamaha, tutoe msamaha, tusamehane saba mara sabini.

Na;
Ambangile, B

Instagram, ambangile_b
