Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,197
Wakuu moja kati ya mambo ambayo bado hatujafikia kukubaliana humu dani ni kama EL amefutwa kabisa kwenye siasa za Tanzania au kuna uwezekano kuwa ni mbogo aliyejeruhiwa tu, ambaye akirudi kutakuwa na kizungumkuti. Hii habari ni copy and paste thing, kama ni duplicate naomba mod iweke inapohusika, lakini naona ina thamani kidogo ya kusomwa. Kuna mawili matatu yanapatikana kwenye magazeti ingawa asili yake ni hapa lakini yanaweza kutusaidia kuelimisha.
*Yumo Naibu Waziri, wapinga ufisadi wataka watuhumiwa wang'olewe CCM
Daniel Mjema, Dodoma
WABUNGE wa CCM wameendelea kuparurana mbele ya kamati ya Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, huku baadhi wakimtetea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na wengine wakisema watuhumiwa wote wa ufisadi wavuliwe nyadhifa za ndani ya chama.
Mvutano huo umetokea wakati kuna malumbano makali yanayoendelea baina ya wabunge na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) juu ya kuwahoji (wabunge) kuhusu kupokea posho mbili kwa kazi moja.
Hii pia ni muendelezo wa malumbano yaliyopo kuhusu utekelezaji wa maazimo ya Bunge juu ya hatua za kuwachukulia maafisa waliotuhumiwa kuhusika na kashfa ya zabuni tata ya kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura iliyotolewa kwa Kampuni ya Richmond.
Mjadala huo mkali ulioanza saa 2:00 usiku hadi saa 7:30, huku baadhi ya wabunge wakichachamaa na kutaka baadhi ya vigogo ndani ya chama hicho wanaotuhumiwa kwa ufisadi wang鈥檕ke.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa kundi linalomtetea Lowassa lilijibu mapigo kwamba, hakuwa na makosa na mambo aliyotuhumiwa nayo yalitungwa kwa sababu ya wivu na uchu wa madaraka na kama njia ya kumwondoa katika nafasi yake.
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Makongoro Mahanga na Mbunge wa viti maalumu, Bernadeta Mushahushu waliiponda ripoti ya Richmond kuwa iliandaliwa kummaliza Lowassa kwa wivu na uchu wa madaraka wa baadhi ya wana-CCM.
Dk Mahanga ambaye ni Mbunge wa Ukonga, alisema ripoti hiyo ni feki huku akipendekeza Rais Kikwete aunde tume huru kupata ukweli akidai kuwa Lowassa alionewa.
Wabunge waliitaka CCM iache kukumbatia viongozi wasio waadilifu na kutaka wote walio na tuhuma wajiengue au waenguliwe ili kurejesha imani ya Watanzania kwa CCM na Serikali.
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, zimeeleza kuwa mbunge wa kwanza kuwasha moto alikuwa Christopher Ole Sendeka wa Jimbo la Simanjiro.
Inadaiwa kuwa mbunge huyo machachari alitaka Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa wawajibishwe kutokana na kuhusishwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi.
Lowassa na mawaziri wengine wawili walilazimika kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na kuhusishwa na kashfa katika mchakato wa Richmond.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa mbunge huyo alitaka pia kuenguliwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kwa kushindwa kusimamia chama kimaadili.
鈥淥le Sendeka alienda mbali na kusema pamoja na nia nzuri ya serikali ya JK kupambana na ufisadi, Makamba haonekani kuguswa na tatizo hilo," kilidai chanzo hicho.
Katika kikao hicho cha faragha, Mbunge wa Sumbawanga, Paul Kimiti aliwashutumu wabunge ambao ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), kwa kushiriki kumdhalilisha Spika wa Bunge, Samuel Sitta katika kikao chake kilichofanyika hivi karibuni.
Alisema Sitta ni kiongozi mahiri anayeliongoza Bunge kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizopo na kumshutumu Mbunge wa Bahi, William Kusila kwa kitendo chake cha kumwita Spika kuwa ni laini.
Kimiti alisema kama Nec ingemnyang鈥檃nya Spika kadi ya CCM na kumwondoa kwenye uspika, basi kauli ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere kuwa kusambaratika CCM kungeleta upinzani wa kweli na kwamba hapo ndipo chama imara cha upinzani kingezaliwa kutoka CCM.
Kwa upande wake, Mushashu aliwabeza Wabunge wanaoitwa wapambanaji wa ufisadi na kudai kwamba vita ya ufisadi ni sera ya CCM na sio sera ya wabunge hao wachache.
Alidai wabunge hao hawajatumwa na CCM na kutaka wawajibishwe na kumshutumu mmoja wa wafanyabiashara nchini (jina tunalo) na vyombo vyake vya habari kwa kushirikiana na kundi hilo.
Mbunge wa Kalenga, Stephen Galinoma alilipongeza kundi hilo la wabunge wapambanaji wa ufisadi na kusema lengo lao ni takatifu na kumpongeza Sitta kwa kuliongoza Bunge kwa viwango.
Kwa upande wake, Mbunge wa Longido, Michael Lekule Laizer alisema CCM kimepoteza maadili na kuna ubaguzi ulioanza kujengeka ndani ya chama.
鈥淜una ubaguzi ndani ya chama katika kushughulikia wanachama wake鈥iongozi wanakaa kimya katika masuala ya msingi ya wananchi na kuwafanya wapoteze imani na serikali,鈥?chanzo chetu kilimkariri mbunge huyo.
Mbunge huyo alipendekeza kuwa viongozi wote wanaokabiliwa na tuhuma mbalimbali wapokonywe nyadhifa zao ndani ya CCM, kwani kuendelea kuwepo kwao kunakipaka matope chama.
Chanzo chetu cha habari kimepasha kuwa mbunge huyo alitahadharisha kuwa kama hatua za haraka hazitachukuliwa, CCM itagawanyika makundi mawili.
Alifafanua kuwa, mgawanyiko huo utatokea kwa kuwa kila kundi linaonekana kutoyumba katika misimamo yake, jambo ambalo ni la hatari sana katika mustakabali wa chama.
Kamati hiyo ya Mwinyi iliundwa na NEC ya CCM katika mkutano wake mjini Dodoma hivi karibuni, ili kuchunguza kiini cha mpasuko miongoni mwa wabunge wa CCM hali ambayo inatishia mshikamano wa chama hicho na serikali yake.
Wajumbe wengine wa kamati hiyo ambayo imekwishahoji makundi mbalimbali ya wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Abdulrahman Kinana.
Source Mwananchi 4 Nov 2009
*Yumo Naibu Waziri, wapinga ufisadi wataka watuhumiwa wang'olewe CCM
Daniel Mjema, Dodoma
WABUNGE wa CCM wameendelea kuparurana mbele ya kamati ya Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, huku baadhi wakimtetea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na wengine wakisema watuhumiwa wote wa ufisadi wavuliwe nyadhifa za ndani ya chama.
Mvutano huo umetokea wakati kuna malumbano makali yanayoendelea baina ya wabunge na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) juu ya kuwahoji (wabunge) kuhusu kupokea posho mbili kwa kazi moja.
Hii pia ni muendelezo wa malumbano yaliyopo kuhusu utekelezaji wa maazimo ya Bunge juu ya hatua za kuwachukulia maafisa waliotuhumiwa kuhusika na kashfa ya zabuni tata ya kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura iliyotolewa kwa Kampuni ya Richmond.
Mjadala huo mkali ulioanza saa 2:00 usiku hadi saa 7:30, huku baadhi ya wabunge wakichachamaa na kutaka baadhi ya vigogo ndani ya chama hicho wanaotuhumiwa kwa ufisadi wang鈥檕ke.
Hata hivyo, inadaiwa kuwa kundi linalomtetea Lowassa lilijibu mapigo kwamba, hakuwa na makosa na mambo aliyotuhumiwa nayo yalitungwa kwa sababu ya wivu na uchu wa madaraka na kama njia ya kumwondoa katika nafasi yake.
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Makongoro Mahanga na Mbunge wa viti maalumu, Bernadeta Mushahushu waliiponda ripoti ya Richmond kuwa iliandaliwa kummaliza Lowassa kwa wivu na uchu wa madaraka wa baadhi ya wana-CCM.
Dk Mahanga ambaye ni Mbunge wa Ukonga, alisema ripoti hiyo ni feki huku akipendekeza Rais Kikwete aunde tume huru kupata ukweli akidai kuwa Lowassa alionewa.
Wabunge waliitaka CCM iache kukumbatia viongozi wasio waadilifu na kutaka wote walio na tuhuma wajiengue au waenguliwe ili kurejesha imani ya Watanzania kwa CCM na Serikali.
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, zimeeleza kuwa mbunge wa kwanza kuwasha moto alikuwa Christopher Ole Sendeka wa Jimbo la Simanjiro.
Inadaiwa kuwa mbunge huyo machachari alitaka Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa wawajibishwe kutokana na kuhusishwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi.
Lowassa na mawaziri wengine wawili walilazimika kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na kuhusishwa na kashfa katika mchakato wa Richmond.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa mbunge huyo alitaka pia kuenguliwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kwa kushindwa kusimamia chama kimaadili.
鈥淥le Sendeka alienda mbali na kusema pamoja na nia nzuri ya serikali ya JK kupambana na ufisadi, Makamba haonekani kuguswa na tatizo hilo," kilidai chanzo hicho.
Katika kikao hicho cha faragha, Mbunge wa Sumbawanga, Paul Kimiti aliwashutumu wabunge ambao ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), kwa kushiriki kumdhalilisha Spika wa Bunge, Samuel Sitta katika kikao chake kilichofanyika hivi karibuni.
Alisema Sitta ni kiongozi mahiri anayeliongoza Bunge kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizopo na kumshutumu Mbunge wa Bahi, William Kusila kwa kitendo chake cha kumwita Spika kuwa ni laini.
Kimiti alisema kama Nec ingemnyang鈥檃nya Spika kadi ya CCM na kumwondoa kwenye uspika, basi kauli ya Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere kuwa kusambaratika CCM kungeleta upinzani wa kweli na kwamba hapo ndipo chama imara cha upinzani kingezaliwa kutoka CCM.
Kwa upande wake, Mushashu aliwabeza Wabunge wanaoitwa wapambanaji wa ufisadi na kudai kwamba vita ya ufisadi ni sera ya CCM na sio sera ya wabunge hao wachache.
Alidai wabunge hao hawajatumwa na CCM na kutaka wawajibishwe na kumshutumu mmoja wa wafanyabiashara nchini (jina tunalo) na vyombo vyake vya habari kwa kushirikiana na kundi hilo.
Mbunge wa Kalenga, Stephen Galinoma alilipongeza kundi hilo la wabunge wapambanaji wa ufisadi na kusema lengo lao ni takatifu na kumpongeza Sitta kwa kuliongoza Bunge kwa viwango.
Kwa upande wake, Mbunge wa Longido, Michael Lekule Laizer alisema CCM kimepoteza maadili na kuna ubaguzi ulioanza kujengeka ndani ya chama.
鈥淜una ubaguzi ndani ya chama katika kushughulikia wanachama wake鈥iongozi wanakaa kimya katika masuala ya msingi ya wananchi na kuwafanya wapoteze imani na serikali,鈥?chanzo chetu kilimkariri mbunge huyo.
Mbunge huyo alipendekeza kuwa viongozi wote wanaokabiliwa na tuhuma mbalimbali wapokonywe nyadhifa zao ndani ya CCM, kwani kuendelea kuwepo kwao kunakipaka matope chama.
Chanzo chetu cha habari kimepasha kuwa mbunge huyo alitahadharisha kuwa kama hatua za haraka hazitachukuliwa, CCM itagawanyika makundi mawili.
Alifafanua kuwa, mgawanyiko huo utatokea kwa kuwa kila kundi linaonekana kutoyumba katika misimamo yake, jambo ambalo ni la hatari sana katika mustakabali wa chama.
Kamati hiyo ya Mwinyi iliundwa na NEC ya CCM katika mkutano wake mjini Dodoma hivi karibuni, ili kuchunguza kiini cha mpasuko miongoni mwa wabunge wa CCM hali ambayo inatishia mshikamano wa chama hicho na serikali yake.
Wajumbe wengine wa kamati hiyo ambayo imekwishahoji makundi mbalimbali ya wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Abdulrahman Kinana.
Source Mwananchi 4 Nov 2009