Tetesi: Kuna viongozi wanaolipwa na serikali ya Misri ili tusitumie maji ya ziwa Victoria

RAY DONOVAN

Senior Member
Jul 2, 2015
153
147
016881298_40100.jpg




Kuna tuhuma kuwa baadhi ya viongozi wa awamu iliyopita na wengine wa awamu hii wako kwenye payroll ya serikali ya Egypt ili kuzima au ku sabotage kwa namna mbali mbali miradi ya kilimo cha Umwagiliaji na matumizi mengine ya maji toka ziwa victoria

Baadhi yao wako ndani ya idara mbali mbali za serikali na maslahi yao ni kwa ajili ya serikali ya Misri na sio Tanzania

Imefika mahala baadhi ya miradi imepigwa chini na watu wa idara ya mazingira kwa visingizio mbali mbali kuwa ili watanzania wasitumie maji ya aiwa victoria

Naomba wenye kujua undani wa haya madai watujuze kwa nini tumewekewa restriction kutumia maji wakati Ethiopia na Sudan wanaendelea na miradi mikubwa mikubwa ya Umwagiliaji na Mabwawa makubwa ya umeme na kadhalika huku sisi tunaambiwa kuwa maji kwenda Shinyanga na mikoa mingine haiwezekani kwa kiwango cha kutosheleza wananchi.

Huko juu Ethiopia wao wameamua kujenga na KUMALIZA kujengaBwawa la umeme kubwa kuliko yote Africa kwenye mto Nile ambao chanzo cha maji yake ni huku kwenye ziwa Victoria


SHERIA

Kuna watu watakuja hapa kukujazeni ujinga wao kuwa kuna mkataba wa 1929 ambao lazima sisi tuuheshim

Ukweli ni kuwa:

1. MKATABA ulikuwa kati ya serikali ya kikoloni ya UINGEREZA na MISRI

2. Kuna mkataba wa Vienna wa The Vienna Convention on Succession of States in Respect of Treaties, ibara ya 16, inasema kuwa mataifa huru au yaliyopata uhuru kama TANGANYIA/TANZANIA hayahitaji kurithi treaty obligations of its colonial power.

Someni mkataba wa Vienna ambao sisi ni signatory na link hii hapa:

http://legal.un.org/ilc/texts/instruments/english/conventions/3_2_1978.pdf











C2hd6jQXUAA9n_t.jpg:large


ges_velykaya_plotyna_efyopskogo_vozrozhdenyya_3d_2.png
 
Hii habari ni baridi na moto, yaani ulipoandika ulilenga irrigation agriculture then ukarukia maji hayajafika Shinyanga! Sina hakika kama anafahamu unachokiandika.
 
Lowasa tu ndie kiboko ya longolongo aliyatupilia mabali madai yao na kuamuru maji yatumike, now shinyanga wanafaidi maji ya ziwa victori.
Lowasa alilikuta tu aliyewakabili wamisri kuwa lilwalo na liwe Tanzania itatumia maji ya Victoria kupeleleka maji maeneo kame ya shinyanga alikuwa Mwandosya alipotamka Hilo misri wakasema Hilo tamko ni kutangaza vita Mwandosya akiwa waziri akakomaa wamisri WAKANYWEA NDIPO LOWASA akiwa waziri akatekeleza Yale aliyokomalia mwandosya.
 
Ni kweli hawa walikuwa wakiongozwa na Bernard Membe...........

Wa Sasa siwajui ila hawatafanikiwa.............
 
Tunasubiri wakitaka kukurupuka kupeleka maji nzega igunga manyoni singid na dodoma!! Hapo Nitaona kweli mwendokasi anayaweza!!!
 
Kaka uneongea wazo zuri na Mimi nilitaka nilete ili wazo hapa
Kwanini watu wa Mleba na vijiji vinavyoizunguka vyoote havina maji na mito midogo midogo wanayoitumia imekauka
Na ukiangalia sehemu kubwa ya Mleba imezungukwa na ziwa Victoria kweli kuna mkono wa MTU
Najiuliza hivi kweli mama wa pesa ya mboga alishindwaje kushughulikia ili swala??
Kwa watu wake
Sasa Mji wa Mleba maji ya taabu
Ukienda Rubya pamoja na ndo kuna hospital inayotumika km ya wilaya ila kwasasa hawana maji ya huakika ni hatari kwa afya za watu
Kuna shule ya sekondari ya Masister wamefikia mahara licha ya kuwa ya bweni wanahamulu wanafunzi wa kalibu anglau wachemsiwe maji ma kwao na hao watoto wa kike kila Mara hospital kwa ugonjwa wa UTI
Nkawa namlalamikia huyu mama kuwa anashindwa nini kuanzisha huu mradi anglau akaja kusaidiwa na serikali ?
Mama hamka watu wa vijijin wanataabika kwa maji hasa Mleba kusin kwa Mama wa pesa ya Mboga
 
Ziwa victoria ni chanzo kinachopeleka maji river nile, Ambapo misri ni final destination kama mpokeaji maji kutoka ziwa victoria.

Hivyo basi sisi watanzania tukiwa na project (irrigation schemes) nyingi kama hzi kiwago cha maji kitakacho kua kinapotea kila siku kitakua kikubwa, Na kupelekea kiwango cha maji kupungua nchini misri.
Tukumbuke kwamba maji hadi yafike misri yanipita sudani na uganda ambapo pia yatatumika katika miradi mbalimbali.

Egypt ni nchi inayotegemea sana kilimo(large scale agriculture) kwa kutumia njia ya umwagiliaji.

Hitimisho.
Egypt ili wafanikishe kilimo cha umwagiliaji wanategemea maji kutoka victoria kupitia mto nile.
Kiwango cha wingi au uchache wa maji mto nile unategemea sana utumiaji wetu maji sisi watanzania.
 
Ziwa victoria ni chanzo kinachopeleka maji river nile, Ambapo misri ni final destination kama mpokeaji maji kutoka ziwa victoria.

Hivyo basi sisi watanzania tukiwa na project (irrigation schemes) nyingi kama hzi kiwago cha maji kitakacho kua kinapotea kila siku kitakua kikubwa, Na kupelekea kiwango cha maji kupungua nchini misri.
Tukumbuke kwamba maji hadi yafike misri yanipita sudani na uganda ambapo pia yatatumika katika miradi mbalimbali.

Egypt ni nchi inayotegemea sana kilimo(large scale agriculture) kwa kutumia njia ya umwagiliaji.

Hitimisho.
Egypt ili wafanikishe kilimo cha umwagiliaji wanategemea maji kutoka victoria kupitia mto nile.
Kiwango cha wingi au uchache wa maji mto nile unategemea sana utumiaji wetu maji sisi watanzania.

Mkuu:
Kwa hiyo sisi hatuna haki ya matumizi ya hayo maji, kwa sababu tutaleta upungufu.

Je tukichukua kutoka kwenye vyanzo au mito inayo ingiza kwenye ziwa victoria bado tutakuwa hatuna haki?
 
Back
Top Bottom