Kuna utajiri wa uhalali?

SteveJr99

Senior Member
Joined
May 13, 2019
Posts
141
Reaction score
302
Habarini wadau wa JF.

Miaka ya Hivi karibuni kumekuwa na Motivation speakers wengi wakiwa na Bidii ya kuwaaminisha watu Fanya hiki au kile ili uwe UTAJIRI.

Swali langu ni hili ni kweli kwamba Kuna UTAJIRI wa njia Halali YAANI yule mtu ambaye anajuhudi tu katika kazi/biashara yake/zake akawa tajiri like MILLIONAIRE PASIPO

βœ… Kwenda kwa Mganga
βœ… Kutoa Kafara
βœ… Kubeti
βœ… Kudhulumu mfano Kutolipa Kodi au Madili ya magendo
βœ… Kuiba
βœ… Kutenda dhambi mfano Ukahaba/Mishangazi
Na zingine zifananazo na Hizo πŸ‘†???
Katika kujibu zingatia Tofauti kati ya UTAJIRI na KUFANIKIWA!!

Anyone can be Succeed but Not Everyone can be RICH.
 
Waafrika tukija kwnye maswala ya utajiri swali la kwkuuliza ni kama kuna njia halali, badala ya mbinu zake

.sass unategemea utatoka link kwa shemu kwa mindset kama hizi
 
Upo mkuu bila chenga!
 
"In every Great fortune there is crime"Balzac. Anyway mleta mada , kasome riwaya ya the Godfather iliyoandikwa na Mario puzo. Huko utakutana na mwamba mmoja anaitwa Vito Corleone . Unaweza kupata sehemu ya jibu ya swali lako kuhusiana na dhana ya utajiri wa halali au haramu.
 
Utajiri wa Kihalali uko.

Sema unahitaji uwe na SUBIRA.

Haupatikan kwa haraka haraka kama Jinsi Vijana wanataka. It take YEARS of dedication and commitment.
 
Najitahid kutafuta sema hizi njia za uhalali kama ngumu hv πŸ˜†
Hapana pesa huwa inakuwa na nyakati na hizohizo nyakati zina njia so issue huwa ni kusoma nyakati na hizo njia!.
mfano wasanii wazamani wa bongo flavour walitengeneza njia ila nyakati ambapo mziki huu umekuja kuwa wa mafanikio zaidi ni sasa!.

kwa njia halali mafanikio unaweza usiyaone wewe, we utakula tu vidude vya hapa na pale ila kwa watoto wako ama wajukuu wanaweza kuja Kutengeneza mpaka wakatamani wakufufue uje uone!..πŸ˜‚

Mafanikio ya kiuhalali yapo sema yanataka kujitoa, uvumilivu na mara nyingi haya humtengeneza mtu kimaarifa sana!, huyu hata ukija kumpokonya akaanza zero baada yamuda utakuta kazalisha tena maana huyu maarifa na experience vimeshamvaa!.

upande wapili mafanikio yapo ya haraka na hatari, sema yanakuwa kama puto likiguswa na jani linapasuka na ndio basi tena halina hata maarifa yakuziba hilo tundu ili lijaze hewa tena!, vya haramu vitamu ila vinaua haraka!.
 
Sijui mkuu ila ninaowafahamu kuna gape la kipigaji waliliotea ndo wakatusua.

Utajiri na uthubutu huenda sambamba.
 
Utajiri unaanza Tsh ngapi?

Maisha matamu uweze kula unachotaka, kama una familia watoto waende shule vizuri wakiwa wamependeza, mama watoto apendeze, nyumbani wale vizuri na wewe uwe na uwezo wa kutakua mambo ya dharura.
 
Kwa Africa utajiri mwingi unasiri sana waulize akina mooooo au bareeeesa,,, watakuambia eti walikuwa wanauza ice cream, mwengine eti karanga,, mwingine mshona viatu na n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…