Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,579
- 161,432
KUNA USHINDI KATIKA KUNYAMAZA
Mfalme Suleiman anasema "Mithali : Mlango 17
28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima;Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu."
Mfalme Suleiman Ni miongoni mwa wafalme waliojaliwa hekima na ufahamu toka juu, anafahamu umhimu wa kunyamaza Tena anaona mtu akinyamaza hata Kama Ni mpumbavu ataonekana mwenye hekima .Ni jinsi gani kunyamaza kulivo na nguvu kunabadilisha hali ya upumbavu hadi hali ya hekima.
Wanandoa wanaachana kwasababu ya kushindwa kunyamaza ,wanandoa wanatoana meno kwasababu ya kushindwa kukubali kunyamaza.
Marafiki wanahitilafiana na hatimaye kuvunja urafiki kwasababu ya kugoma kunyamaza.
Ndugu wanafikia hatua ya kupingana kwasababu ya kukataa kunyamaza.
Mataifa yanafikia hatua ya kuingia kwenye Vita kwasababu ya kurushiana maneno.
Maneno yaliwaponza wayahudi ASILIMIA kubwa wakafia jangwani.
Mdomo uliponza Musa akajikuta anakosa fursa ya kuingia kanaani.
Kuna USHINDI KATIKA KUNYAMAZA.
Usiwalazimishe watu wajue unaweza nyamaza ,fanya wajionea ipo siku watakusifu wao wenyewe kwa vinywa vyao.
Usiwalazimishe watu wajue umeokoka nyamaza, siku ya mwisho parapanda likilia wakikuona umetwaliwa wataamini ,Ila watakuwa wamechelewa.
Nasema Tena nyamaza ,na Mungu atakukumbuka ,maana wanadamu Wana maneno Mengi lakini usikate tamaa chakufanya Ni kunyamaza tu
Mfalme Suleiman anasema "Mithali : Mlango 17
28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima;Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu."
Mfalme Suleiman Ni miongoni mwa wafalme waliojaliwa hekima na ufahamu toka juu, anafahamu umhimu wa kunyamaza Tena anaona mtu akinyamaza hata Kama Ni mpumbavu ataonekana mwenye hekima .Ni jinsi gani kunyamaza kulivo na nguvu kunabadilisha hali ya upumbavu hadi hali ya hekima.
Wanandoa wanaachana kwasababu ya kushindwa kunyamaza ,wanandoa wanatoana meno kwasababu ya kushindwa kukubali kunyamaza.
Marafiki wanahitilafiana na hatimaye kuvunja urafiki kwasababu ya kugoma kunyamaza.
Ndugu wanafikia hatua ya kupingana kwasababu ya kukataa kunyamaza.
Mataifa yanafikia hatua ya kuingia kwenye Vita kwasababu ya kurushiana maneno.
Maneno yaliwaponza wayahudi ASILIMIA kubwa wakafia jangwani.
Mdomo uliponza Musa akajikuta anakosa fursa ya kuingia kanaani.
Kuna USHINDI KATIKA KUNYAMAZA.
- Kunyamaza Kuna punguza hasira ya mtu unayejibizana naye
- Kunyamaza Ni njia ya kuficha madhaifu yako kwa watu Kama hasira,wivu, matusi etc
- Kunyamaza Ni njia ya kuwachanganya adui zako wasikujue wewe Ni Nani hasa? Msimamo wako?
- Kunyamaza Ni njia ya kumsubiria Mungu akujibu kwa wakti wake ...Maana kusema sema kunaweza kukufanya umlaumu au kumkufuru Mungu.
- Kunyamaza kunakupunguzia Maadui,,,, Kama ulikuwa hujui mtu mwongeaji anamaadui wengi kuliko mkimya.
Usiwalazimishe watu wajue unaweza nyamaza ,fanya wajionea ipo siku watakusifu wao wenyewe kwa vinywa vyao.
Usiwalazimishe watu wajue umeokoka nyamaza, siku ya mwisho parapanda likilia wakikuona umetwaliwa wataamini ,Ila watakuwa wamechelewa.
Nasema Tena nyamaza ,na Mungu atakukumbuka ,maana wanadamu Wana maneno Mengi lakini usikate tamaa chakufanya Ni kunyamaza tu

