Kuna tofauti kati ya VISA na Pasport?

Kuna tofauti kati ya VISA na Pasport?

Kama raia wa Tanzania ni haki yako kupata passport .
Passport inakuwezesha wewe kusafiri na kukutambulisha umetokea wapi.
Ila Visa unawekewa ndani ya passport, ukitaka kwenda nje ya nchi,unaenda ubalozi wa nchi husika na kuwekewa visa.
Huwezi kwenda Marekani au Ulaya pasipo na Visa na passport .

Alihitaji kufahamishwa hivi...sio kebehi
 
Passport(hati ya kusafiria) inakuwezesha kutambulishwa uraia, kupata msaada kwenye balozi ya nchi yako unapokuwa ugenini.
Visa: Kibali cha kuingia na kuishi kwa kwa kujishughulisha au kutojishughulisha na shughuli yeyote ya kiuchumi unapokuwa ugenini inayotolewa kabla hujafika nchi husika au baada ya kufika nchi hiyo...
 
Jamani nashukuru sana.ukweli niliku sielewi.
Ila nauliza tena.gharama ya VISA huwa ni kiasi gani kwa wastani? Na je huwa inausubufu kupata au ni maelezo yako:?

Gharama ya visa, urahisi wa upatikanaji wake (usumbufu) unategemea vitu kama;
Aina ya visa ie. Ya kitalii, biashara, diplomasia nk.
Muda utakaokaa huko ugenini.
Mahusiano ya nchi yako na nchi unayotaka kuizuru mf.. Tz hatuna ubalozi wa Ethiopia so itabidi utafutie visa Kenya ( na hatupo kwenye list ya visa on arrival tukiwa Ethiopia) hivyo gharama itakuwa kubwa.
Uharaka wa hyo visa ( the express the expensive) na sababu nyingine walizochangia wadau
 
Nashukuru sana jamani sasa nimepata kuelewa..
 
Hakuna haja ya matusi/lugha za kejeli. Ahsanteni mliojibu mmesaidia na wengine. Mnaonesha u-great thinker wenu.
 
acha ushamba. vsa unaipata ktk ubaloz wa nchi unayoenda. passport unaipata ktk wzara ya nchi yko na huwez kutembelea nchi bla kua n vsa wala passport vyte muhm

Sasa unataka aachaje ushamba Bila ya kumuelimisha,acha majigambo haha wewe mwenyewe Kuna mengi huyajui ila hakuna anayekuita mshamba,ushamba ni kujifanya unajua huku hujui,
 
Viza ni vile vi daftari vidogo tulivokua tunatumia shule zamani...ila liwe na mistary midg na midg..ukifika ubalozi wa kijiji husika wanagonga muhuri....akuna cha maana tna.
 
Pasport ni hati ya kusafiria ambayo unapewa na nchi yako na visa ni ruhusa ya kuingia nchi nyingine.kuna nchi unaweza kupata visa unapo wasili na zingine kabla ya kuondoka nchini kwako.
 
Kama raia wa Tanzania ni haki yako kupata passport .
Passport inakuwezesha wewe kusafiri na kukutambulisha umetokea wapi.
Ila Visa unawekewa ndani ya passport, ukitaka kwenda nje ya nchi,unaenda ubalozi wa nchi husika na kuwekewa visa.
Huwezi kwenda Marekani au Ulaya pasipo na Visa na passport .
Mkuu kwa bahati mbaya sana nadhani passport sio haki ni 'privilege' (Mnisaidie kiswahili cha hili neno)
 
Passport ni utambulisho wa Utaifa wako. Vissa ni kibali cha kuingia taifa unalotarajia kwenda.
Wakati mwingine passport haihusiani na utambulisho wa uraia. Ni document inayoonesha nchi fulani imekubali kuwa custodian wako japokuwa mara nyingi hupewa raia zaidi kuliko wageni.
 
acha ushamba. vsa unaipata ktk ubaloz wa nchi unayoenda. passport unaipata ktk wzara ya nchi yko na huwez kutembelea nchi bla kua n vsa wala passport vyte muhm

Kwani ni lazima umuite mshamba?kwani we ulizaliwa unajua kila kitu?mueleweshe tu kwa utaratibu...kwani we unajua kila kitu duniani?
 
Swali la nyongeza, Je mgeni kutoka ulaya au Marekani, akitaka kuja Tanzania atapewa Vissa?
 
Swali la nyongeza, Je mgeni kutoka ulaya au Marekani, akitaka kuja Tanzania atapewa Vissa?


Mgeni lazima atimishe masharti yaliowekwa na serikali kwa mgeni kuruhusiwa kuingia Tanzania.

Mgeni anaweza kuomba viza ubalozi wa Tanzania, Marekani, au akaomba visa uwanja wa ndege, Tanzania, au kwa njia ya posta, Marekani.

Kwa raia wa EU, anaweza kuomba visa katika ubalozi wa Tanzania nchini kwake, au kama hamna, anaweza kuomba kwa njia ya posta, Ubalozi wa Tanzania ulio karibu na nchi yake.

Kwa baadhi ya raia , unaweza kuomba uwanja wa ndege pia unapowasili (visa on arrival).

Masharti ya serikali ni kuwa na pesa za kutosha, uwe na anuani na simu ya sehemu unayokaa, tiketi ya ndege ya kurudi kwenu na pasi iwe ina zaidi ya miezi 6 kabla kuisha.

Unaweza kuomba multiple entry au single entry viza, viza ya kwenda katika mkutano (business visa) au ya kutalii/ kuona ndugu.

Kwa wageni, ukitaka kukaa zaidi ya siku 90, lazima uombe permit ya kuishi Uhamiaji.

Raia wa Marekani ni $100 kwa viza za kitalii za siku 90.

Raia wa Uiingereza ni poundi 40 ($65) kwa viza za kitalii za siku 90.

Ukiridhisha masharti yao, unaweza kupewa permit kutoka Uhamiaji, ya "spouse" kama umeowa/umeolewa na raia wa Tanzania, permit za kufanya shughuli za kidini, permit za kufanya biashara na kadhalika.
 
Passport ni kibali cha kuingia nchini na visa ni kibali cha kukaa nchini
 
Passport unaipata wizaran unapotoka na visa unaipata kweny ubaloz wa nchi unayokwenda
 
Una miaka mingapi?

Umesoma shule ipi?

Nnakuomba nijibu hayo nikupe ushauri.

Unauliza maswali gani hayo ya kimizengwe ya CCM. Badilika mama, mwenzio kauliza swali very simple, wewe unauliza maswali kama vile ametangaza nia kwa tiketi ya CCM. Hagombei uongozi ndani ya chama chenu huyu. Kwani umri na shule vina uhusiano gani na passport ????
Sidhani kama wewe kabla ya leo ulikua unajua tofauti ya passport na VISA.
 
Back
Top Bottom